Mkulo, Maige, Ngeleja kikaangoni TAKUKURU

Mkulo, Maige, Ngeleja kikaangoni TAKUKURU

Invisible

JF Admin
Joined
Feb 26, 2006
Posts
16,286
Reaction score
8,447
Wakuu,

Taarifa zilizopenya kwenye viunga hivi zinadai kuwa mawaziri walioachishwa kazi [Mkulo, Maige na Mzee wa Megawatts (Ngeleja)] wako kikaongoni Takukuru na kwamba kila siku lazima waripoti saa tatu asubuhi.

Inadaiwa Mkulo kakutwa na Vogue 2 na Land Cruiser 2 zote mpya hata nylon hazijatolewa kwenye magari yenyewe nyumbani kwake Mikocheni.

Mzee wa Megawatts (Ngeleja) kashfa yake ni ya zile Benz zake alizoleta na Air Cargo na madudu mengine wizarani.

Maige kauza Vitalu vya walafi serikalini kawazidi akili wenzake (isichukuliwe kama namtetea)

Habari zaidi zitafuatia...
 
Eti, haiwezekani wakatolewa hadharani kwa wananchi wenye hasira kali wakamaliza game? mbona vibaka wa simu na kuku huwa wanakutana na wananchi wenye hasira kali? hawa vipi hawaingii kwene category hii? laiti wezi wa kuku nao na wale wa simu wangekuwa wanachunguzwa na Takokuru haki ingepatikana bila ya ncha ya upanga
 
Nasubiri kwa hamu kuona mwisho wa hiyo sinema mpya in town kwa hisani ya CCM. Uliwahi kuona wapi mtuhumiwa wa wizi kwa mali za umma akiandikiwa tena hundi eti kwa kimombo cha GRATUITY?
 
Thanks Invisible, hower i dont have confidence on TAKUKURU.

Well may be this time TAKUKURU will not disappoint.

Let me keep my fingers crossed.
 
na huyu Maige alivyokuwa analalamika kwa Michuzi na hadi kuweka mistari ya biblia kumbe hana lolote anatafuta fadhila
 
Kuwa kiongozi wa watu inabidi uwe muadilifu sana... Wanatumia kodi zenu na rasilimali za watanzania kujinuisha wao na familia zao huku wengine tukifa kwa matatizo chungu nzima...

MUNGU hakumpa uwaziri Mkulo, Megawatt eta'l na akamfanya baba yangu kuwa mkulima kule kijijini kwetu halafu maisha yaishie hapo...lazima na ipo siku Mungu ataweka usawa miongoni mwetu...na siku hiyo yaja....
 
hii ni muvi nyingine ambapo sasa kesi ya nyani inapelekwa kwa ngedere
 
hii ilipokuwa inaitwa takuru tulisema haina meno tukaiongeza ku nyingine ili iwe na meno,sasa ili iweze kuwapata na hatia hawa jamaa nashauri iongezewe meno iwe kama simba, iitwe takukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukukuru.

Nimeweka ku 32 ambayo ni meno ya mtu mzima kwa sababu hayo mawili yalishashindwa.
 
Hosea aliwahi kuuliza UDSM kuhusu kesi za ufisadi akajibu " a dog can not bite his boss but atleast can bark at him"
Tumeshazoea ngonjera zao na hakuna jipya..
 
Takukuru is Toothless hata miba ya Samaki hawawezi kuivunja wataweza hiyo Mifupa ya Ng'ombe.

Takukuru wenyewe wala Rushwa hawana lolote hapo ni Changa la macho wa Watanzania
 
mie nadhani kwa hawa watu tutumie hukumu ya sharia kuwahadhibu hawa mafisadi.
 
usiingie wala kuitoa hii thread. tutakua tunaweka updates hapa. nasikia charles ikerege naye kasimamishwa kazi na bodi ya tbs.
 
Mkulo, Ngeleja, Maige ni kivuli cha CCM. Takukuru ni tawi la CCM. Hosea ni mwanachama hai wa CCM. Toka lini mtu akakimbia kivuli chake?. Takukuru haina ubavu wa kuwachukulia hatua akina Mkulo. Akina mkulo na Lowasa nani kafanya madudu ya kutisha ndani ya Tanzania?. Je Lowasa amefanywa nini na Takukuru?.

Umefika wakati wa kutumia risasi kukomesha na kufagia uchafu ndani ya Tanzania. Tungewapiga risasi wezi wetu wa EPA, Richmond, Deep Green, Meremeta, Rada na Kiwira akina Mkulo wasingefanya madudu.
 
Uzoefu wangu na nchi hii unanikataza kuamini kuwa kuna lolote litaenda kutokea hapo......

Ahsante kwa taarifa Robot langu
 
Vogue mbili?na VX 2 si ulafi tuu huo!
Mimi nkiwaona hao jela ndo ntakuwa na imani
 
Back
Top Bottom