mkopo wa BAYPORT mnauonaje?

mkopo wa BAYPORT mnauonaje?

Al shabab

Member
Joined
May 21, 2011
Posts
71
Reaction score
6
jamani nauliza hawa jamaa wanaaminika?kama uliwahi kopa kwao naomba taarifa pls!
 
kuwa makini na mashirika madogomadogo yanayokopesha! kuna kesi nyingi sana zinatangazwa kwenye magezeti kuhususiana na udhulumaji wa hayo makapuni!
 
Watu mnalalamika bila kuwa na evidence.. Mnajua ni kwanini wana-riba kubwa.. Watanzania kibao hatuna utamaduni wa kukopa na kulipa.. Na ndio sababu ni vigumu sana kwa mwananchi wa kawaida kupata mkopo bank zenye riba afadhali..
Tatizo si uelewa wa walimu.. Naomba jamaa aliyewatukana walimu ajaribu kufanya research ndogo sana.. Ndio atoe kauli hiyo..
 
Hizi microfinance bayport, blue, platnam finka etc wanatoa mikopo kwa riba ya juu kwa sababu nao wanakopa bank ili wawakopeshe ninyi, ni kweli bayport ni wakweli within 24 hrs unapata aprovel ya mkopo wako, riba yao iko juu sana ila ukiwa na shida fasta unapata. binafsi sikushauri kama unakopesheka kwenye bank bora uende bank maana wateja wengi wanaokopa knye hizi micro finance ni wale wasio kopesheka tena bank.
 
watanzania kila kitu mnaponda tu mara oooh ni kampuni ndogo ...
mnajua kuwa bayport ni MNC company?
BML: Home
next time tujaribu kufanya research sio kutoa maoni kuhusu tusichokijua..
 
Sijakopa huko lakini kuwa makini sana hakuna mtu aliyekopa huko marambili

Utaambiwa Riba ni 6% kumbe hiyo ni kila mwezi, Hivyo 72% kwa mwaka. Kama umekopa mkopo wa miaka 3 zidisha 72% mara tatu. Bora uende benki upigwe riba 20-22% kwa mwaka au jiunge na SACCOS.

Kama utakopa tafadhali turudishie taarifa baada ya mwaka mmoja.
 
weeee,usithubu kabisaaaaaa,baypot,faidika,finca cjui na vinini vingne hovyo kbs,.mi nlikopa pale milioni moja tu mwaka 2008 yan mpaka sasa wanakata kwny mshahara sh 36 elfu na cjui ntamaliza lini,.nikifuatilia wananiambia bado kidogo,yan koma kbs usiende huko
 
watanzania kila kitu mnaponda tu mara oooh ni kampuni ndogo ...
mnajua kuwa bayport ni MNC company?
BML: Home
next time tujaribu kufanya research sio kutoa maoni kuhusu tusichokijua..

Tunazijua hizi Taasisi za Fedha hatubahatishi,tulikwisha fanya research ndio maana tu conclude moja kwa moja,mimi binafsi simshauri mtu kwenda huko,JINO KWA JINO NA DIDIA wamemalizia au kama na wewe huwaelewi denda katika ofisi zao na upate taarifa juu ya riba zao tena jifanye mjinga uliza tu nikikopa 700,000.00 narejesha ngapi,baada ya hapo fanya mahesabu ni asilimia ngapi utawafahamu.
 
ktk kampuni ambazo sitaki kuzisikia hadi naingia kaburini ni hao ulio wataja,mzazi wangu ni mwalimu,alikopa kwa hao jamaa kiasi cha laki 7,cha kushangaza hawa jamaa walikata pesa hadi ikafika jumla ya 2m na hata baada ya mda kufika wa kulipa deni wao waliendelea kukata hadi mkurugenzi aliingilia kati kwa kuwaandikia barua ya kusitisha makato.

hawa jamaa achana nao kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa,hata kama unatatizo la kufa mtu ni bora uende kukopa kwa mtu laki kwa kulipa laki na nusu kuliko hao jamaa,utajuta kukopa
 
1.Finca
2.Platnum Credit
3.Blue Finance
4.Easy Finance
5.Bayport

Waulize walimu watakwambiaaaa!!

Walimu bwana ni tatizo la kitaifa,na hawa jamaa ndio kimbilio lao huko, wakielewa kuwa hawana ufahamu wa mambo ya riba,ila sasa waliokopa mala moja hao walimu huwa hawarudi tena huko maana wanakuwa wamepewa somo kwa vitendo
 
Beyport ni kampuni ya mama Anna Mkapa na kweli ni wezi hata bungeni Mh. Ereasto Zambi alishatoa mararamiko yake lakini hakuna aliemsikiliza
 
Walimu bwana ni tatizo la kitaifa,na hawa jamaa ndio kimbilio lao huko, wakielewa kuwa hawana ufahamu wa mambo ya riba,ila sasa waliokopa mala moja hao walimu huwa hawarudi tena huko maana wanakuwa wamepewa somo kwa vitendo

Hao Jamaa wameteka soko la walimu kweli,kila mwalimu kashachinjwa na hao watu!
 
Back
Top Bottom