MIZANIA Mkojo wa Ngamia ni salama kutumika kama dawa kwa binadamu

MIZANIA Mkojo wa Ngamia ni salama kutumika kama dawa kwa binadamu

Taarifa hii imeachwa katika mizani ya wasomaji wapime uzito wa hoja za kila upande

1770040072551.png
 
Tunachokijua
Shirika la afya duniani inaeleza kutokana na uwepo wa tiba mbadala ambayo hutumika kwa wingi zaidi nchini Saudi Arabia ambapo moja ya desturi za kawaida ni matumizi ya mkojo wa ngamia peke yake au kuchanganywa na maziwa ya ngamia kwa ajili ya kutibu saratani, jambo ambalo mara nyingi huungwa mkono na imani za kidini.

Kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa na WHO "Use of camel urine is of no benefit to cancer patients: observational study and literature review" Mkojo wa ngamia haukuonesha faida yoyote ya kitabibu kwa wagonjwa wowote wa saratani, na huenda hata ulisababisha maambukizi ya magonjwa ya kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu. Uhamasishaji wa mkojo wa ngamia kama tiba ya jadi unapaswa kusitishwa kwa sababu hakuna ushahidi wa kisayansi unaounga mkono matumizi yake.

Wagonjwa wote waliofanyiwa uchunguzi wa radiolojia kabla na baada ya matibabu yao kwa kutumia mkojo wa ngamia. Wote walitumia mchanganyiko wa mkojo wa ngamia na maziwa ya ngamia, na muda wa matibabu ulianzia siku chache hadi miezi 6. Walitumia wastani wa mililita 60 za mchanganyiko wa mkojo/maziwa kwa siku. Hakukuonekana faida yoyote ya kitabibu baada ya matibabu; wagonjwa 2 walipata brucellosis, maambukizi ya bakteria yanayotoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu kupitia matumizi ya maziwa yasiyochemshwa, nyama isiyopikwa vizuri, au kwa kugusana na majimaji ya wanyama walioambukizwa.

Wagonjwa kumi na mmoja walibadilisha mawazo na kukubali matibabu ya kawaida ya kupambana na saratani, na wagonjwa 7 walikuwa dhaifu sana kupokea matibabu zaidi; walifariki kutokana na ugonjwa huo.

Lakini baadhi ya tafiti (Is camel’s urine friend or enemy? Review of its role in humanhealth or diseases)zinaeleza kuwa msingi wa kidini wa matumizi ya mkojo wa ngamia katika matibabu unatokana na imani kwamba kuna ushahidi unaoaminika kuwa Mtume Muhammad (SAW) alishauri kutumia mkojo wa ngamia kutibu maumivu ya tumbo wakati huo. Mkojo wa ngamia unasemekana kuwa na sifa za kupambana na kisukari, saratani, bakteria, virusi na fangasi. Pia unasemekana kuwa na athari za kulinda ini (hepato-protective) na kuboresha afya ya mfumo wa moyo na mishipa ya damu.

Ndio kwa Waislamu hili halina shida walikuja watu wawili kwa Mtume wakamwambia wanaumwa na tumbo mtume akawaambia wakachukue mkojo wa ngamia wakanywa na maradhi yakawaondoka
 
Kwa mjibu wa utafiti ambao umefanywa na Shirika la Afya Duniani (WHO) mwaka 2023 na mamlaka za afya duniani zinaonya dhidi ya matumizi ya mkojo wa ngamia likinukuu katika utafiti wake kuwa Hakuna ushahidi wa kisayansi unaothibitisha kuwa mkojo huo unaweza kutibu magonjwa kwa binadamu. Badala yake, unywaji wa mkojo mbichi huweka watu katika hatari ya kupata magonjwa hatari kutoka kwa wanyama (zoonotic diseases).

Kwa kuzingatia utafiti ambao umefanywa na shirika la afya dunian unabainisha sababu mbalimbali ambazo zinaonesha kuwa matumizi ya mkojo wa ngamia hayafai kwa binadamu kama ifuatavyo.

Ukosefu wa Msingi wa Kisayansi: Ingawa kuna tafiti za awali za maabara (kwenye seli au wanyama) zinazoonesha uwezekano wa dondoo za mkojo kupambana na vimelea, tafiti hizi hazijawahi kuthibitishwa kwa binadamu kupitia majaribio rasmi ya kliniki.

Hatari ya MERS-CoV na Bakteria: WHO inahusisha unywaji wa mkojo na maziwa mabichi ya ngamia na kuenea kwa virusi vya korona vya Mashariki ya Kati (MERS-CoV). Pia, matumizi yake yamesababisha maambukizi ya Brucellosis, ugonjwa mkali wa bakteria.
Kando na taarifa hizo pia kumekuwepo na Matokeo ya Kitabibu ambapo Uchunguzi kwa wagonjwa wa saratani waliotumia mkojo wa ngamia kama tiba mbadala ulionyesha:

Wagonjwa wote walifanyiwa uchunguzi wa radiolojia kabla na baada ya matibabu yao kwa kutumia mkojo wa ngamia. Wote walitumia mchanganyiko wa mkojo wa ngamia na maziwa ya ngamia, na matibabu yalikuwa kuanzia siku chache hadi miezi 6. Walitumia wastani wa mililita 60 za mkojo/maziwa kwa siku. Hakuna faida ya kimatibabu iliyoonekana baada ya matibabu; wagonjwa 2 walipata ugonjwa wa brucellosis. Wagonjwa kumi na mmoja walibadilisha mawazo yao na kukubali matibabu ya kawaida ya kuzuia uvimbe na 7 walikuwa dhaifu sana kupata matibabu zaidi; walikufa kutokana na ugonjwa huo.
 
Back
Top Bottom