Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,393
Kuna wanawake ambao kwa lugha ya mazoea tunasema wamewatawala waume zao. Yaani wao ndio wenye kauli ya mwisho katika nyumba na pia hutumia vibaya madaraka hayo kwa kuwanyanyasa waume zao. Akina mama wa aina hii ni rahisi sana kwao kusababisha baadhi ya watoto wao kuja kuwa mashoga.
Inakuwaje?
Baadhi ya watoto hawa ni wale wa kiume hujikuta wakimtazama baba yao kama mwanaume aliyeshindwa na hutafsiri kushindwa kwake kama kasoro ya uanaume. Katika mkabala huo watoto hawa hujikuta wakiatamani kuwa kama mama zao, kwani mama zao ni mashujaa wao na kwao kuwa mwanamke kuna maana ya madaraka, kutoa amri na kuheshimiwa zaidi. Mtoto hujenga na kuamini mambo hayo ndani ya fikra zinazofahamika kama Subconscious Mind, ambazo ni fikra au mawazo yasiyopumzika na yanayotunza kumbukumbu zote kwa matumizi ya baadae ya binadamu. Kwa kawaida watoto huwa hawajui kwamba ndivyo fikra zinavyoamini kwani Subconscious Mind hufanya kazi bila mhusika kujua.
Kwa kuwa ndivyo mtoto anavyoamini ndani ya fikra zake, mtoto hujikuta akiwa karibu zaidi na mama na kujaribu kumuiga mama yake kuliko baba yake ambaye anamuona kama mnyonge. Kwa hiyo mtoto huyu wa kiume ataanza kufanya mambo yote ya kike kwani kwake uke ni ushujaa. Hata wenzake anaoshirikiana nao mambo ya kufichaiansiri watakuwa ni wanawake. Kujibainisha kijinsia itakuwa vigumu sana kwake. Hii ni kwa sababu kwa nje atakuwa anajiona kuwa ni mwanaume, ingawa kwa ndani anajihisi kuwa ni mwanamke na atakuwa anapendelea kuwa hivyo.
Mwanasaikolojia mkongwe na maarufu duniani, Dennis Coon, ambaye katika kitabu chake , Introduction to Psychology amekusanya na kuzikagua nadharia mbalimbali kuhusu chanzo cha ushoga, anakiri kwamba nadharia ya malezi inaonekana kuwa na mashiko zaidi. Anasema mama "Mbabe" na mwenye kumwendesha mwanaume na kuutweza utu wake na heshima ya uanaume wake anaweza kabisa akujikuta akiwa na watoto wa kiume wanaojibainisha naye na kuukimbia uanaume wa baba yao. Watoto kama hawa sio ajabu wakiwa mashoga………………….!
Inakuwaje?
Baadhi ya watoto hawa ni wale wa kiume hujikuta wakimtazama baba yao kama mwanaume aliyeshindwa na hutafsiri kushindwa kwake kama kasoro ya uanaume. Katika mkabala huo watoto hawa hujikuta wakiatamani kuwa kama mama zao, kwani mama zao ni mashujaa wao na kwao kuwa mwanamke kuna maana ya madaraka, kutoa amri na kuheshimiwa zaidi. Mtoto hujenga na kuamini mambo hayo ndani ya fikra zinazofahamika kama Subconscious Mind, ambazo ni fikra au mawazo yasiyopumzika na yanayotunza kumbukumbu zote kwa matumizi ya baadae ya binadamu. Kwa kawaida watoto huwa hawajui kwamba ndivyo fikra zinavyoamini kwani Subconscious Mind hufanya kazi bila mhusika kujua.
Kwa kuwa ndivyo mtoto anavyoamini ndani ya fikra zake, mtoto hujikuta akiwa karibu zaidi na mama na kujaribu kumuiga mama yake kuliko baba yake ambaye anamuona kama mnyonge. Kwa hiyo mtoto huyu wa kiume ataanza kufanya mambo yote ya kike kwani kwake uke ni ushujaa. Hata wenzake anaoshirikiana nao mambo ya kufichaiansiri watakuwa ni wanawake. Kujibainisha kijinsia itakuwa vigumu sana kwake. Hii ni kwa sababu kwa nje atakuwa anajiona kuwa ni mwanaume, ingawa kwa ndani anajihisi kuwa ni mwanamke na atakuwa anapendelea kuwa hivyo.
Mwanasaikolojia mkongwe na maarufu duniani, Dennis Coon, ambaye katika kitabu chake , Introduction to Psychology amekusanya na kuzikagua nadharia mbalimbali kuhusu chanzo cha ushoga, anakiri kwamba nadharia ya malezi inaonekana kuwa na mashiko zaidi. Anasema mama "Mbabe" na mwenye kumwendesha mwanaume na kuutweza utu wake na heshima ya uanaume wake anaweza kabisa akujikuta akiwa na watoto wa kiume wanaojibainisha naye na kuukimbia uanaume wa baba yao. Watoto kama hawa sio ajabu wakiwa mashoga………………….!