Mkimzingua ataunda chama chake

Kila mtu anahaki ya kutoa maoni yake. Kumpinga mtu kwa jambo fulani sio kumchukia. Kikubwa ni kuzingatia maslai ya Taifa.

Hili kundi limeibuka na kumkejeli Rais Samia Suluhu kwa kila hatua anayofanya. Uwepo wake ni takwa la kikatiba; sasa mlitakaje?
 
 
Hiki kipindi uzuri tunaofaidika ni wengi kuliko zaman make ishakuwa zaman hatuna namna
 
Ni wakati sasa urudi kwenye kazi yako origin. Teheheheeeee.

Siasa wachie wenyewe.


Samia aunde chama na nani? Au unataka arudi kisiwani?
Hizi ndio hoja za washindwa badala ya kujadili hoja wanamjadili mtoa hoja
 
Akifanya hivi atakuwa amezingua hasa!

Namwona Samia kama yule Joyce wa Malawi mwingine.

Amekosa subira sana.

Alitakiwa ajipange vizuri, na aanze na yale mabovu kabisa ya Magufuli kabla ya kujihusisha na haya yatakayomletea shida kubwa sana, na kufanya kazi yake iwe ngumu zaidi.

Nauliza: Haraka yote ni ya nini, si anayo miaka minne na ushee kujiimarisha vyema?

Lakini kuna somo kubwa kwetu hapa katika haya na Magufuli na Samia. Mfumo wetu wa utawala wa nchi ni mbaya kweli kweli. Yaani mtu mmoja anaingia, anabadilisha chochote anavyotaka, bila ya vikao wala nini?

Hii ni nchi au ni jalala?
 
acha mikwara mbuzi wewe eti kuna watu wamepewa hela nyooka raia hawataki kuona tunarudi tulikotoka kwenye utawala wa upigaji wa enzi hizo wameshaonjeshwa utamu wa kujitegemea na matokeo chanya kuonekana kwa vitendo na siyo maneno

enzi za porojo ziliisha enzi za jk sasa hivi watu wanataka matokeo
 
Na wewe ni mmojawapo? Maana hata ulichoandika hakiakisi mada husika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…