Kuweza kumpa MwanaAfrika Mashariki mwezetu jawabu murua na lenye kutosheleza,ni vema turejee kidogo Historia ya Elimu yetu kidogo na pia harakati za ndani ya nchi yao.
1.Serikali ya Tanzania, chini ya Utawala wa awamu ya Kwanza ilitilia mkazo umuhimu wa kupandikiza hisia, fikra na mitazamo ya kizalendo kwa nchi yetu na hata kwa bara la Afrika kwa ujumla,chini ya dhana ya Pan Africanism.Tutakumbuka,kuwa, Nyerere na Nkurumah ndio waliokuwa mstari wa mbele katika harakati za kulifanya bara la na Afrika kuwa moja.
Wakisukumwa na hisia,matamanio na mitazamo ya Ki-Pan Africanism,watunga sera ,mitaala na mihustari na vitabu,katika somo uraia ,kabla yake somo la Elimu ya siasa na hata katika somo la historia walitilia maanani umuhimu wa wanafunzi kupata uelewa wakina na wa kutosha juu ya bara la Afrika.Si ajabu wanafunzi tena katika ngazi ya Elimu ya msingi ,wa miaka ya nyuma kidogo kuweza kutaja majina ya viongozi wa nchi mbalimbali katika bara la Afrika kama vile Ahmed Ben Bela wa Algeria,Robert Mugabe wa Zimbambwe, Nkurumah wa Ghana ,Kenyata na Moi ,wote wa Kenya,Mobutu wa Zaire na hata Bedel Bokasa wa CAR.Ni wazi, madhui ya somo la Elimu ya Uraia na Historia hapa nchini yamechangia Watanzania kuwa na hamasa ya kutaka kujua yanayojiri katika nchi jirani na zetu.
2.Huko nyuma,nchi ya Kenya ilifanya bidii za makusudi kuifanya radio ya KBC iweze kusikika katika nchi mbali mbali ikiwemo hapa nchini kwetu.Hatua hiyo,ilitufanya tuweze kufuatilia ,kujua na kuelewa yaliyokuwa yakijiri ndani ya nchi hiyo na hata kujua majina ya baadhi ya miji ndani ya nchi hiyo.Hata sasa,hata baada ya umaarufu wa redio hiyo kupungua,bado,tunaendelea kufuatilia na kutaka kujua yanayojiri kwao.