kimacho,
Mkuu, kwanza pole sana sana sana kwa unayopitia ...
Lakini, nikutie moyo na kukuondoa shaka - suala lako sio geni, ndoa kama ndoa karibia zote ni ngumu sana na ndio maana kwa sisi wafuata kristo tulishauriwa kama tunaweza kuishi katika usafi wa kiimani then tusioe kabisa.
Katika ndoa kuna vipindi vigumu na vipindi vizuri sana, I mean kuna vipindi vyote na siku zote uamuzi wa kuoa is the biggest risk a human can take so namini hata wewe hukutegemea kuwa it will be a piece of cake - huu sasa ndio muda wa kuonesha ukomavu wako na kama kweli ulistahili kuwa mume.
Ushauri wangu:
1. Kwanza, kaa chini tena, sehemu tulivu na bila jazba na dai kuujua ukweli wote
2. Jipe muda wa kutosha sana kupumzika na kulifikiria hili kwa umakini ukichukulia tayari kuna mtoto/watoto, kwa kuanzia fanya utaratibu wa kuthibitisha kama kweli first born ni wako au lah - Believe me jibu la swali hilo litarahisisha maamuzi mengine yote coz nionavyo, msingi wa yote yanayoendelea ni hilo.
3. Mwisho, ukishajua kama mtoto ni wako au lah - usisahau kuusikiliza moyo wako, maisha ni mafupi sana.