Mke wangu kanibadilikia baada ya ndoa.

Hallow!!!!!!!!!! sasa wewe mtu huna uhusiano naye wowote, uongee naye kwenye simu, huyo huyo siku hiyo hiyo anakutakia Gnite. Hivi ingekuwa ni mke wako anafanya hivyo si ungekuja na post ya kuuliza kama mke wako hakusaliti kweli wewe???? hata ningekuwa mimi pasingetosha loh!!!!!!!!!!!
 
kaka hilo ni kosa kubwa sana. Mimi nimejifunza siwezi kuwa na msichana mwingize ama kuzoeana na demu mwingine zaidi ya msichana wangu tu. thats all. So nakushauri uachane kabisa na wasichana wengine ukiwazoea ama wanakupigia ama nini utaipoteza ndoa. Hapo mke wako hana kosa na yupo so right wewe omba msamaha na focus kwa mke wako tu .
I hope you are not serious, right?
 
quote_icon.png
By Saint Ivuga
kaka hilo ni kosa kubwa sana. Mimi nimejifunza siwezi kuwa na msichana mwingize ama kuzoeana na demu mwingine zaidi ya msichana wangu tu. thats all. So nakushauri uachane kabisa na wasichana wengine ukiwazoea ama wanakupigia ama nini utaipoteza ndoa. Hapo mke wako hana kosa na yupo so right wewe omba msamaha na focus kwa mke wako tu .

I hope you are not serious, right?

hayupo serious huyu hajaoa /olewa huyu!
 
Mambo ya good night toka kwa mdada mwingine yanatoka wapi?ingekua ni mkeo katumiwa g9t na mwanamume mwingine ungejiskiaje??? Acha mazoea yasiyo na mipaka na vibinti vingine na ndoa yako itadumu

Hata mimi imenishtua kidogo, yaani kutakiana usiku mwema na mdada bila mahusiano yoyote, inatatiza.
 
Hali zenu wana JF, imenibidi nitumie jukwaa hili ili kuweza kupata ushauri wa busara na hekima. Mimi nimekua na mahusiano na msichana mmoja hivi kwa takribani miaka 6 hivi na hatimaye mwanzoni mwa mwaka tukakubaliana kuingia ktk ndoa. Kimsingi tumeishi vizuri sana kipindi chote cha uchumba wetu potelea mbali matatizo madogo madogo ambayo ni ya kawaida ktk mapenzi, lakini kilichonifanya kuanzisha huu uzi ni kwamba toka nianze kukaa nae mwezi wa 7 amekua na tabia ya kunichagulia marafiki wa kuwasiliana nao kwny simu kitendo ambacho kinanikera sana na tabia hii hakua nayo mwanzo, sms ikiingia anataka awe wa kwanza kusoma hata simu yng ikiita anataka aone nani anapiga na jana nilipigiwa simu na rafiki tu wa kike na yeye alikua nje akifua nguo baada ya kusikia nikiongea kwny simu alikuja dirishani ili kusikiliza mazungumzo yetu na kiukweli yalikua ni mazungumzo ya kawaida ya kutakiana hali cha ajabu yeye akakasirika na kudai kwanini nawasiliana na wasichana nikamwelesha lakini bado, na ikaingia sms ya gd9t tu ya hy hy msichana basi ndo ikawa tabu akaninunia mpaka mda huu hatujaongea nae hata chakula nimekula hotelini. Sijawahi kumcheat hy mwanamke lkn kwake naonekana namcheat daily, nimeongea nae kuhusu hili suala hadi nimechoka. Naomba mnishauri nifanye nini maana nimeishavunja urafiki na watu wengi na nimebadili laini hadi watu wananishangaa lakini kwake hy haitoshi. Nampenda sana lakini huu mwenendo wake umenichosha.

Pia na yeye alikuwa anacheat kabla ya ndoa. mwizi akikutana na mtu mwingine huwa na wasi wasi wa kuibiwa. usipomsikiliza anachotaka atarudi kwenye koloni lake la zamani na ataongezea na mengine mwisho wa siku atakuletea HIV. Kaa naye umueleweshe juu ya mahusiano yako na rafiki zako. Na muoneshe imani juu ya hao watu. Ukiona hamuwezani zaidi MUACHANE. kwani utapata mwenza mwingine.
 
Mimi USHAURI WANGU NAUTOA FRM EXPERIANCE!!!!!! My Broo nae kabla ya kuoa alikua SWEETIE wa mademu kibao, na hata kuchangia harusi walichanga kinomaaa! Sasa baada ya kuoa si ndio IKAWA KASHESHE!!! Bi dada kila simu ikiita ANAVIMBA KAMA KOBRAAAA! Tukamshauri awe Dk 3 Mbele!!!! Sasa wale SWEETIE umewaambia unaoa nao hawana tabu na mtu, na wamekuchangia, huwezi KUKATA MAWASILIANO GHAFLA!!! Na wengine ni wateja wazuri coz anafanya BUSINESS TOKA CHINA!!!! SULUHISHO TULILOFIKIA NI KUWA NA SIMU MBILI, TENA KAMUONESHA MKEWE, MOJA YA BUSINESS, INALALA KWENYE GARI, NYINGINE YA PERSONAL NDO ANAINGIA NAYO MATRIMONIAL ROOM! LOLEST! Tena Bi Dada alipigwa biti kuwa ASIIZOEE ZOEE ILE SIMU YA BUSINESS KABISA, HIYO PERSONAL AKITAKA ASHINDE NAYO, AKAAMBIWA KAMA ANATAKA WALE MAWE HUMO NDANI ACHEZEE BUSINESS CONECTIONS AND NETWORKS!!! Hahahaaaaaa! Simu anaitaka kuikagua, Kula mawe haweziii, ALISONYAJE KIMYA KIMYA!!! Sasa na wewe UMEWEKEE MKEO MIPAKA!!!! LOL! (Mimi sikuombi kukagua, NAKULIA TIMING TU! IKIINGIA KWENYE 18 ZANGU, NAMBA TATA ZOTE NAZIKOPI, WALA SIKUULIZI, NAZITAFUTIA LINE YA MAGUMASHI!!! UTAISOMA KIMYA! KIMYA! KILA NAYEMSHUKU ATALIJUA JIJI KUWASILIANA NA WEWE! LOLEST!!!)
kwikwikwiwkiwkwiwkwi timing to ndio dili ukitaka usigombane na watu mi jana niliona mlolongo wa sms kama chating kwenye IPAD ile nimechungulia akiwa kaishika akaificha alafu kama kakasirika kwanini nimechungulia nikasema subiri langu kichwani nkaamka saa nane nikachukua ile IPAD nikatoka sebuleni nikafunga mlamngo kwa nje ,kwenda nakuta ni mlolongo wa sms alizokuwa anahamisha pesa kwa simbanking niliumbukajeeeeeeee shost nikajirudia mdogoooooooooooooo kwikwiwkiwkwi
 
I hope you are not serious, right?
mfundishe huyu dogo dada yangu kungwi wanafikiri zile hongera za 13yrs universaryulipewa watu wanaenda na mambo yao ya zamani kwenye ndoa !!!!!wacha yote huko hiyo ni new life bana
 
kaka hilo ni kosa kubwa sana. Mimi nimejifunza siwezi kuwa na msichana mwingize ama kuzoeana na demu mwingine zaidi ya msichana wangu tu. thats all. So nakushauri uachane kabisa na wasichana wengine ukiwazoea ama wanakupigia ama nini utaipoteza ndoa. Hapo mke wako hana kosa na yupo so right wewe omba msamaha na focus kwa mke wako tu .

Ni kweli kama anaweza hivyo, lakini ndoa ni furaha jamani endapo utashindwa kuongea hata na wale kinadada unaofanyaga nao business vizuri mtakula nini sasa jama? na je wife nae haongei kabisa na wanaume? mie naona tatizo ni moja tu kwa bwana kaka, haujamfanya mkeo ajisikie yeye ni namba moja, nakiri sie wadada baadhi tunaudhaifu wa kujisikia insecured kama haujisikii unapendwa, nakuhakikishia hata uache kuongea na wasichana wooote bado migogoro ya kutoaminiana haitaisha. Somewhere something is not right wala sio hapo kwenye kuongea na wasichana, chunguza na ufanyie kazi utaona maajabu, Mfanye mkeo ajisikie unampenda na pia aelewe kuwa unaouhuru wa kuwasiliana na watu wengine au na wewe unamkataza kuongea na wakaka?
 
Pole miezi saba tu migogoro imeshaanza ? Bidada hajiamini?

Mungu awapiganie
yaani mi nachokaaaaa, nikisiaga hivyo! kwa kweli inashangaza, mi nakumbuka nilivyoolewa ile miaka miwili ya mwanzo ilikuwa ni full raha, yaani huwa nawish kuturn back the days, japo sasa miaka imesogea ila matatizo yapo na raha pia zipo! so kaka UVUMILIVU ni kitu cha kwanza kwenye ndoa yenu, kile kilichowafanya mkadumu miaka 6 ya uchumba, BASI HICHO HICHO KIWAPIGANIE MILELE, BILA KUACHANA! amen!
 
Pole sana ama kweli ndoa ndoano, ongea na wazee wa hekima kutoka upande wa mkeo ili wamkanye kuhusu tabia hii maana kiukweli inakera na haikuachi huru.
 
huyo ndugu yangu kaa naye chini chini ya marafiki zake mueleza hali hiyo alafu sijui anafanya kazi au mama wa nyumbani mimi hata mke wangu alikuwa na tabia hiyo ,lakini baada ya kukaa na watu mbalimbali akabadirika
 
Ndugu ndoa sio rahisi sana kama watu wengi tuvyofikiria, ndoa nitofauti na wapendanao wakawaida (yaani girl & boy friends) cha muhimu mkuu jaribu kubadili tabia, na kuanza maisha mpya MATAKATIFU (yaani mwili mmoja), yale mambo ya kwenye Face Book yaache kabisa, fungua ukurasa mpya wa maisha yenu mapya, MARAFIKI sawa, lakini MKEO ni zaidi ya kila kitu, hiyo simu yako ni nzuri nani mbaya katika maisha ndoa. (husikubali kuwa mtumwa wa simu) Ndiyo maana kuna swala ili - kwamba wapenzi wengi wakiwa mwili mmoja na kufunga ndoa wanaachana na line zao za simu za zamani ili kuepuka upuhuzi unaoweza kujitokeza kwa namna moja au nyingine, unaoletwe na simu za mikononi (kwa vi TOY Girl & toy boy) Mkuu mpende sana mkeo, yeye anakupenda sana ndiyo maana anakufatilia sana, muonyeshe upendo wako kweke. Mwanamke akihamua kupenda anapenda kweli. Mpe nafasi mwenzio na maisha yenu yatakuwa mazuri tu.

Ahsante kwa ushausi wako mzuri na uliojaa hekima ndani yako.
 
Du! Nimekupenda buuuureeeee!

Yani huyu anatafuta tumhurumie wakati amekosea.

Unaongea na mwanamke kwenye simu...haya labda ni business; unakata simu huyo mwanamke anaona maongezi hayakutosha anakutumia na sms ya good night juu...maana yake ilikuwa usiku. Hatuendi hivyo.
Hii inaonyesha huyo mwanamke alokupigia anataka kukuonyesha kuwa anakujali wakati wewe huna shida ya wa kukujali...you have a wife; mwambie naye atafute mume aache kukusumbua.


Wewe umezoesha hao wanawake sijuhi rafiki zako vibaya...inabidi wajue wewe ni mume wa mtu na hauko available for whatever reason iwe charting au kupigiana simu usiku.



kaka hilo ni kosa kubwa sana. Mimi nimejifunza siwezi kuwa na msichana mwingize ama kuzoeana na demu mwingine zaidi ya msichana wangu tu. thats all. So nakushauri uachane kabisa na wasichana wengine ukiwazoea ama wanakupigia ama nini utaipoteza ndoa. Hapo mke wako hana kosa na yupo so right wewe omba msamaha na focus kwa mke wako tu .
 
Back
Top Bottom