Mke wangu hataki wageni

Mke wangu hataki wageni

swali alilokuuliza mkeo ni la msingi mno,wewe mimba unaijua?Mimi nakuongezea swali,shughuli ya kumhudumia mzazi unaijua?halafu Huyo mama wa binti mjamzito nae hana akili.unawezaje kuruhusu mwanao akajifungulie ugenini kirahisirahisi tu!
 
Mleta Mada hueleweki yaani unampokea Mwanamke aje ajifunguli kwako na hujui kapewa Mimba na nani
halafu Mwanamume mzima ukamkande maji Mzazi?

Ushauri wangu FUKUZIA MBALI watu wa namna hii kwani unaweza kukuta Mimba ina mushkeli au Kesi kibao
Baba kampa Mimba mwanae sasa anataka kuficha soooo
 
Sijaona kosa la huyo mkeo,maana hukumshirikisha.
 
Heri wewe umeliona hili

kuna watu hawajielewi. wewe ubebe tu watu uwapelekee wengine mizigo. ili iweje?
si waende wakapange gesti waishi?

pale META-Mbeya kuna wasukuma na wamasai wanatokaga chunya huko vijijini kabisa na siku zikikaribia wanajisogeza mjini na kupanga gest/vyumba maeneo ya karibu na hospitali zai ya miezi miwili wanasubiria tu mpaka mama akijifungua wanarudi kijijini.

huyu ndugu wa huyu jamaa ni limbukeni. utamtoaje mke wa mtu kwa mumewe umpeleke kwa rafiki yako?
unajuaje wanaendelea kupeana kama kawaida?
ndio maana mke wa jamaa kachomoa kwani itabidi aanze kulea huyo binti, mume wake na mama mkwe naye atataka aje.
na inavyoonesha huyo binti hata nguo hawezi kujifulia hivyo litakuwa jukumu la mke wake.
kwanza usikute mimba yenyewe ndio ina wiki nne tu ambayo hata uhakika wa kuwa itaendelea kuwepo haupo
 
unafanya uamuz wa kumpokea mama mjamzito ukae nae mpk ajifungue bila kumshirikisha wife???? unajua kero za kumhudumia mama mjamzito/aliejifungua?? mheshimu mke wako na kubali ulikosea.....pia mwombe msamaha kwa kukurupuka!!
 
Unaposema mkeo hapendi wageni unatumia kigezo hicho cha kukataa mjamzito? Au huwa unakataa na wengine?? Usimlazimishie majukumu yasiyomuhusu!! Kama unataka kumridhisha mshikaji wako pangishia hao wageni gest karibu na Hosp!! Ila ujue jukumu unalotaka kujibebesha ni kubwa sana!! Kwenye kujifungua kuna mambo mengi mazito!! Sitaki kuyataja itakutisha ila mkeo mweke mbali na hili na usimuhukumu!! Yupo sahihi kabisa vile haukumshirikisha tangu mwanzo
 
Wakuu,

Kisa chenyewe ni hiki;

Mwenzenu mke wangu hasomeki. Mimi nina rafiki yangu tangu enzi hizo tuko primary. Huyu jamaa yangu, binti yake kaolewa na sasa ni mjamzito. Kama mnavyojua ujauzito wa mtoto wake wa kwanza huyu rafiki yangu kapagawa kushinda Mkwe wake.

Wanaishi bush, sasa ameniomba binti take aje akae kwangu ili ajisubilishe kujifungua katika hospital nzuri town.Ombi lake lilikuwa la maongezi kwa njia ya simu, mimi kwa haraka haraka bila kumshtua/kumwambia mke wangu nikakubàli.

Nilipofika nyumbani nikamweleza ujio wa wageni hawa. Aisee sikutegemea, mke wangu aliwaka kama Mbogo, na kuanza kuniambia wewe mimba unaijua?

Akakomaa kuwa hataki kuwaona hapa.

Sasa wakuu, wenye wapenzi hii issue ni i handle namna gani? Manake jamaa nimeshamuahidi, sasa kumwambia asije naona soo.

Nipeni mawazo wandugu

hujamshirikisha toka mwanzo, nyumba ni ya wawili.... Mgeni wa siku moja haina tatizo, lakini mgeni wa kuja kukaa daah,
Lakini Jitahidi kuwa mkorofi, Wanaume tunapaswa kuwa wapole kiasi na wakorofi kiasi kuleta heshima, siyo kila anachosema mkeo unaitikia tuu...hapana. Yashanitokea, unakuta mwanamke anasema kabisa baba fulani ni mpole mpaka anakera...Onyesha msimamo.
 
Sijui kwanini wanawake hawapendani... Sijui kwakweli....

Mmh mkuu inataka moyo sana, niliwah kukaa na jamaa yake Mume Wangu alivyojifungua hizo kaz nilizokuwa nafanya za mzazi ni shida, kufua nguo za mzazi alizochafua leba ,nikisema hiv wazaz wananielewa, halafu yule bint alikuwa anakula viporo bas ile nguo ilikuja na m... ,karud home habadilish ped mpaka mnguo zinachafuka, kiufup alikuwa mchafu, mvivu, mwez mzima namfanyia kila kitu ,
 
Wewe ungeletewa taarifa na mkeo kua kuna mtoto wa rafiki ake anakuja kujiangalizia ujauzto kwako ungekubali?
 
Usimlaumu mkeo kwa sababu ulitakiwa kumshirikisha kabla na yeye pia ili achukue mamuzi yake. Mimba siyo mchezo, hajii kukaa tu huyo hapo kama unavyodhania wewe. Kuna mambo mengi sana, na huo mzigo wote wa uangalizi utakuwa juu ya mkeo.
 
Sijui kwanini wanawake hawapendani... Sijui kwakweli....

tunapendana sana ila mkee wa jamaa hajiamini tena ni mchoyo anazani mjamzito atamaliza chakula. Tena baada ya kujifungu atamlisha ugari na makande mpaka akome so wajiongeze.
 
tunapendana sana ila mkee wa jamaa hajiamini tena ni mchoyo anazani mjamzito atamaliza chakula. Tena baada ya kujifungu atamlisha ugari na makande mpaka akome so wajiongeze.

mimi siwezi kumlazinisha mke wangu kubeba majukumu ya mke wa mtu mwenye wazazi, wakwe, wifi zake na wake wenzie.
huo utakuwa ni upuuzi naufanya.
mwisho wa siku mtakuja kulipwa majungu tu.
mke wangu atahudumia ndugu zangu tu tena sio kwa kumlazimisha.
hivi umewahi kuzaa au kuhudumia mzazi? ndio maana wanapendaga watu wazima wawepo nyumbani kwani kazi zingine ni busara na hekima ndio inawaongoza
 
Unajua mwanaume kama mleta uzi na wenzie wanaotetea wanajua wao wakileta kiroba cha unga maharage basi...miguu juu makalio chini...

Shughuki yote ya hudumu humuangukia mkewe.....lawama kwa mkewe...mabaya na mazuri mkewe......

Hivi wanajua uzazi wanausikia????

Na kwa nini mzazi ahudumiwe na watu baki????



mimi siwezi kumlazinisha mke wangu kubeba majukumu ya mke wa mtu mwenye wazazi, wakwe, wifi zake na wake wenzie.
huo utakuwa ni upuuzi naufanya.
mwisho wa siku mtakuja kulipwa majungu tu.
mke wangu atahudumia ndugu zangu tu tena sio kwa kumlazimisha.
hivi umewahi kuzaa au kuhudumia mzazi? ndio maana wanapendaga watu wazima wawepo nyumbani kwani kazi zingine ni busara na hekima ndio inawaongoza
 
Mmh mkuu inataka moyo sana, niliwah kukaa na jamaa yake Mume Wangu alivyojifungua hizo kaz nilizokuwa nafanya za mzazi ni shida, kufua nguo za mzazi alizochafua leba ,nikisema hiv wazaz wananielewa, halafu yule bint alikuwa anakula viporo bas ile nguo ilikuja na m... ,karud home habadilish ped mpaka mnguo zinachafuka, kiufup alikuwa mchafu, mvivu, mwez mzima namfanyia kila kitu ,
Pole sana. Kumbe umeolewa.... kwanini bado wajiita miss miss nuru??
 
Last edited by a moderator:
Kulea mzazi ni shughuli tena shughuli pevu afu haishirikishi mwanaume. Kumpa mkeo kazi ya kulea mzazi tena sio ndugu yenu bila makubaliano sio fair...
 
Hata mimi ningemwambia wife wangu angenifanya hivyo hivyo. Utaletaje mjamzito asiyewahusu nyumbani kwenu tena bila kupata ushauri wa wife wako? Huyo rafiki yako hana ndugu wa kike? Huyo mwanaume hana ndugu zake? Hapo huna cha kumlaumu wife wako umechemsha baba
 
Ni kweli kabisa kiasili wanawake hatupendani japo mimi namshukuru Mungu sijawahi kumchukia mwanamke yoyote.Kaka unaposema mke wako hapendi wageni hicho kichwa cha mada hakiendani na maudhui,umeanzaje kukubali kumpokea mtu ambae mhudumiaji mkuu atakua mkeo bila kumwambia mkeo?Mfano ni sawa na yeye kumpokea mwanafunzi wa chuo kikuu aliekosa mkopo wewe umlipie miaka mitatu wakati yeye ni mama wa nyumbani.Sijui kama unanielewa ila kumhudumia mjamzito au mama aliyejifungua ni issue ingine kabisa mkuu.Hao rafiki zako waambie tuu kwamba mkeo anasafiri kwa hiyo wewe ni mwanaume huwezi kutoa huduma ya kike.Inabidi udanganye tuu maana hakuna namna nyingine
 
Title kubwaaaa,eti "Mke wangu Hataki wageni"
Wewe na huyo rafiki yako wote mna matatizo,huyo bint hana mama? Anakubalije mwanae akajifungulie ugenini?
Huyo bint Si ameolewa? Kwa nini Baba ndio awe anahaha kumtafutia bint kwa kujifungulia?
 
Back
Top Bottom