Mke wangu hataki kunisamehe. Nifanyeje?

Simpi talaka yoyote hata iweje kwa sababu nyingiii kikubwa wanangu wasipata anko mpya maana waifu nae anavyopenda mchezo wetu wa wakubwa dah
We jamaa ni msengerema boya boya fulan hivi, unajifanya gentleman kumbe ni ushubwada tu wewe kila anaekupa ushauri unamwijia juu,

Unaulizwa umemfanyia kosa lipi ili tupate kukushauri kulingana na uzito wa kosa, unabaki kutukana watu tu.

Kwa akili zako za kindezi hizo yawezekana hata hao watoto siyo wako. Na huko aliko sasahivi acha apelekewe moto tu mpaka akili zitakapo kukaa sawa.
 
Habari wakuu wa kaya

Nina account humu ila imebidi nifungue nyingine sababu tunafahamiana na baadhi ya watu humu na mimi ni mjuaji yani mbele za watu napenda kuonekana mwanamke hawezi kunipelekesha.

Nimemkosea mke wangu wa miaka 7 ya ndoa. Miaka 7. Tuna watoto wawili. Amegoma kunisamehe ameondoka, naumia kuwaza kuna mwanaume anaweza kummliki.

Msinishauri nijikaze, siwezi siwezi siwezi kuona kuna mwanaume atakuja kuwa anatambulika kama baba au uncle kwa wanangu, nasema siwezi. Ameacha kila kitu nyumbani ina maana kuna mtu ataenda kumnunulia vingine au? Nimejenga ila sioni faida ya kuishi kama watoto wangu hawazunguki nyumbani hapa na kelele zao.

Siamini kuzaa nje ovyo ovyo najua madhara yake. Nifanyaje arudi mama Doreen wangu. Amenivumilia mno. Najisikia vibaya sana naishi kama mhuni tu nyumbani. Nifanyeje arudi. Nizeeke mwenyewe au mtu mpya hapana hapana.

Mtakaotukana tukaneni tu, nahitaji njia za kumrudisha.

Yupo kwao
nenda kwa sangoma, amrudishe, muamini mungu kama hauna shida "MTU MZIMA MWENYE MVI KICHWANI" aliniambia haya maneno
 
Habari wakuu wa kaya.

Nina account humu ila imebidi nifungue nyingine sababu tunafahamiana na baadhi ya watu humu na mimi ni mjuaji yani mbele za watu napenda kuonekana mwanamke hawezi kunipelekesha.

Nimemkosea mke wangu wa miaka 7 ya ndoa. Miaka 7. Tuna watoto wawili. Amegoma kunisamehe ameondoka, naumia kuwaza kuna mwanaume anaweza kummliki.

Msinishauri nijikaze, siwezi siwezi siwezi kuona kuna mwanaume atakuja kuwa anatambulika kama baba au uncle kwa wanangu, nasema siwezi. Ameacha kila kitu nyumbani ina maana kuna mtu ataenda kumnunulia vingine au? Nimejenga ila sioni faida ya kuishi kama watoto wangu hawazunguki nyumbani hapa na kelele zao.

Siamini kuzaa nje ovyo ovyo najua madhara yake. Nifanyaje arudi mama Doreen wangu. Amenivumilia mno. Najisikia vibaya sana naishi kama mhuni tu nyumbani. Nifanyeje arudi. Nizeeke mwenyewe au mtu mpya hapana hapana.

Mtakaotukana tukaneni tu, nahitaji njia za kumrudisha.

Yupo kwao
Ulimkuta na bikra zote 2?
 
Huyu jamaa hajajiua kweli mbona yupo kimya.

Huyu jamaa alimuomba kwa mparange tu siyo bure
 
Una uhakika unajutia?

Una hakika unauhitaji msamaha na hautorudia?

Inaonekana vitendo vyako vilimchosha na vikasababisha majeraha ya moyo. Sasa ikiwa unajutia kweli je unaweza kusali??

Ushauri: Rudi kwa Bwana Mungu. Embu tulia muombe Mungu msamaha kwa makosa uliyofanya. Katika toba ndipo kuna msamaha wa dhambi.

Jisacrifice omba toba tena kwa kufunga ikiwezekana. Ulishaichezea ndoa kwa kutoiheshimu. (Ndoa na iheshimiwe na watu wote..)

Kaa katika machozi kwa Mungu. Then ukishasikia nafuu muombe Mungu amrudishe mke wako. Sasa huku unamuomba Mungu huku unamtafuta physically. Yani rohoni na mwilini. Mtafute tu. Msalimie, mjulie hali, kila unapomtafuta omba msamaha. Mwambie umejutia kweli.

Anza kumtongoza upya. So huku unaomba mbele za Mungu ili ambadilishe moyo wake, huku unamtongoza. Ulishamess up so maybe jaribu hii njia.,..na Mungu aendelee kukuelekeza cha kufanya.

Wapendwa tuiheshimu ndoa, tuipende ndoa...tumuogope Mungu wapendwa.

#go
WAIFU AMERUDI NYUMBANI RASMI JANA IJUMAA. Niliusikiliza na kuufuatilia ushauri wako ulinigusa sana. Nilijifunza kumrudia Mungu huku naendelea kumtafuta mara kwa mara kwa meseji,vocha,watoto wangu niliwapelekea zawadi. Nikiri sitarudia tena kumkosea heshima na kuharibu nyumba yangu. Nimeamka mapema kuwaandalia breakfast matata after stealing the 'SHOW' na kummaliza kabisa.
 
Una maneno makali sana kiufupi nimekosea kweli si mara moja yani mara nyingi kila aina ya jambo baya unalojua. Kiukweli kanivumilia yani atachukua mkopo anisaidie huku na kule japo yeye ana mshahara mdogo mpk tumetulia sasa hivi.

Niliamua kuuchuna kutomtafuta na yeye kimyakimya nimepeleka maua ofisini kwake asubuhi leo kuchunguza nasikia yamewekwa reception kwao. Kweli?? Huyu nani anamfundisha?hata kama amenichoka sio hivi. Nimemiss familia yangu kutoka moyoni,inanitesa sana hii nimepata uhuru wote duniani kuachwa lakini sitamani hata mijitu mingine da maishaaaa
Piga chini oa mwingine(😅😅si huwa unashauri wenzio hivi?)
 
WAIFU AMERUDI NYUMBANI RASMI JANA IJUMAA. Niliusikiliza na kuufuatilia ushauri wako ulinigusa sana. Nilijifunza kumrudia Mungu huku naendelea kumtafuta mara kwa mara kwa meseji,vocha,watoto wangu niliwapelekea zawadi. Nikiri sitarudia tena kumkosea heshima na kuharibu nyumba yangu. Nimeamka mapema kuwaandalia breakfast matata after stealing the 'SHOW' na kummaliza kabisa.
Wow wow wow a very powerful testimony.

Guys come and see what The Lord has done for this brethren.

Jamani namuinua Mungu kwa ajili yako mpendwa. Jina lake Bwana libarikiwe sana.

Wapendwa nadhani tunaona jinsi Mungu anavyojibu tukimtafuta kwa moyo wote. Neno linasema kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana akiomba kwa bidii. Rafiki here decided kuiacha dunia. Akashut sauti zote zilizomsogeza mbali na Bwana.

He decided kurudi msalabani. Wapendwa wengi wetu tumepoteza, tumeharibika kisaikolojia kwa sababu ya wrong choices we made. Kuna ambao kiroho wamekufa kabisa they simply don care, neema ya Bwana ikawazukie.

Lakini kama in one way or another ulishamess up somewhere, good news Mungu yupo hapa. Jamani Mungu anakusikia. Turudi kwa magoti na machozi anajibu. Em refer to the story ya mwanampotevu. Lakini baba ake akampokea kwa furaha.

Kila mmoja leo kwa nafasi yako..kaa tafakari wapi ulianguka..tutubu tumrejee bwana naye atatusamehe, ataturestore...atatufanikisha katika nyakati sahihi.

The word of God says Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa BIDII wataniona.

#GodisGoodguys#
 
Bila kusahau

Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha na kuomba, na kunitafuta uso na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao na kuiponya nchi yao 2Nyak7:14

So people lets be compelled kuutafuta uso wa Mungu. I assure you hashindwi na chochote. Many of us tumefungwa kwenye lango la muda. We think like time is running. Sonultimately we make wrong choices. Na zinatucost sana. Lakini nani azijuaye nyakati zake?

Tujitie nguvu katika Bwana na tumuombe Mungu kuyajua na kuyatenda mapenzi yake ili shetani asipate hatia ya kutushtaki.

#sorrynimepreachonyourthread#
 
Kawaida ilivyo muombe mungu aliyemuumba aulainishe moyo wake aweze kurudi akutambue kama wewe mumewe....!
Kama kashindwa kukusamehe basi hata ibada zake hazina malipo yoyote)Kwanini asisamehe ikiwa mwenyezi mungu anasamehe viumbe wake?
Kila mwanadamu ni mkoseaji ila mbora niyule mwenye kukubali kosa akaomba msamaha
 
Back
Top Bottom