Mke wangu hanisikii

naogopa ku mwambia umwache yasije nitokea yaliyonikuta huko nyuma. mwaka juzi mdogo wangu alioa mke kutoka mikoani, sasa alipomuowa yule mke akawa na vitimbi vya ajabu ajabu na mara anadai huyo mme siyo chaguo lake, ndani pakawa hapakaliki na mimi mwenyewe nikaona kweli ndani hakuna maelewano. siku moja mdogo wangu akawapigia wazazi wa yule mke wake akawaelezea kila kitu. wale wazazi walipompigia mtoto wao (mke wa dogo), mwanao akawajibu hivi...kwani baba we ndio umeolewa huku? msinilazimishe kuishi na mtu ambaye mm simtaki. hapo na mm nilikuwa naskia na naona hiyo movie...hapohapo nikachukua uamuzi wa kumshauri dogo amuache. sikujua kuwa dogo alikuwa anaomba ushauri wa kumfukuza mke wake ili hali bado anampenda, wakienda kitandani wanabembelezana. baade dogo kanambia..aah, nimeamua nimsamehe amesema atajirekebisha, ngoja tuone itakuwaje hapo baadae.
then wakaanza kuishi wote na mimi niliyetoa ushauri wa kuachana nikaanza kuona aibu. pamoja na kuwa wanaishi lakini wanaishi maisha ya bora liende..mwanamke ni mchungu kama pilipili, namuonea sana huruma dogo maana ile siyo ndoa ni ndoano.
ndio maana nasema msimshauri amwache huenda anampenda sana na nyie atawashangaa kwa ushauri wenu maamuzi ya mwisho anayo yeye...maana ndiye anayefinywa...


Katika washauri wa makmbo ya ndoa wewe unastahili...TEAMO huwa ana msimamo kama wako.
HATUJUI ANACHOMPENDEA- SO HATUWEZIMSHAURI AMUACHE.

On second thought............mtoa mada ameomba tumshauri namna ya kumwacha mkewe au amelalamika tu kuwa mke hamsikilizi???

Kaa chini ongea na mkeo, mweleze usiyoyapenda na yeye akueleze anayoyataka, muya-table na kupanga namna ya kuyatekeleza. Mawasiliano ni muhimu MUME na MKE COMMUNICATION ni muhimu sana.
 
amezoea kuachika huyo haoni ajabu kwa hilo ndo hulka yake akimchoka mume hamthamini kama mume bali anakuona kama hawara tu,kuna jamaa anamzuzua hakawii kureplace position yako mkuu,utabembeleza yataisha lakini yatarudi tena wakati mmeshazaa na kuwapa watoto taabu ya dual citizenship
 
Kama hasikii unamsemesha wa nini? Mpe Ishara

Kunguru Hafugiki Mwachie haraka sana akajitafutie popote unapoteza muda fasta changamka...
 
Huyo mwanamke anataka umsaidie ila hatumii njia nzuri ya kukuomba msaada, hana maana achana nae tafuta mwingine. usikute karudiana na mumewe wa kwanza
 
Ulikurupuka ndugu yangu! Mwenzio kaacha hata hujajua kaacha kwa sababu gani? wewe ukanyakua visivyonyakulika! sasa unalo! Kwa kuwa huna mtoto naye bora umuache mapema maana utachakachuka mpaka basi
 
katikaa vitu vigumu ni kuowaa mke au mume aliachikaa...wengi wanaachikaa kwa visirani huyo wako chunguza aliachika kwa kitu gani...je kweli alipewa talaka au ndo alichomoka tu akakupata ukavuta ndani sasaa hivi unaliaa.pole sanaaa...ila sio ndoa hiyo ndoano
 
katikaa vitu vigumu ni kuowaa mke au mume aliachikaa...wengi wanaachikaa kwa visirani huyo wako chunguza aliachika kwa kitu gani...je kweli alipewa talaka au ndo alichomoka tu akakupata ukavuta ndani sasaa hivi unaliaa.pole sanaaa...ila sio ndoa hiyo ndoano

Hivi huwa unasikitikaga nini mpendwa?
 
Sikubali nikae kimya....mwanajamii nina hofu na wewe waweza kuwa chanzo cha tatizo lako na hasa katika uteuzi wa huo ubavu wako je, ulipata nini sababu ya yeye kuachika na mume wa kwanza?huenda alishindana nae kitabia upo?...na jingine la kutambua sio watu wote wanatakiwa kuoa au kuolewa huenda Mungu alipanga wakae bila waume au wake na ndio maana katika uteuzi yapaswa umshirikishe Allah{swt} ili upate kilichobora okey naomba ujue hujaja hapa duniani kupata tabu kama ni ndoa ya ruhusa kuacha mwache abaki kwa dada yake na talaka imfuate huko..na kama ndoa ya kutokuacha na yeye aliachwa basi si mke wako ni wa yule aliyemwacha..... nadhani niache ukumbi wakati huo huo nahisi kama ulimpenda sana maana kisheria kutoa mimba ni kuua na kuua ni mada kwasababu ameua hata sindwa kukua hata wewe.TAKE CARE MAN..
 
Achana naye huyo,atakuua bure!mwenzio nilishaweka nadhiri ya kutokuoa aliyeachika ama aliyekwishazaa!

Kuna walioolewa wakaachika kwa sababu za msingi na kuna wasioolewa bado ila wana mahusiano sawa na walioolewa tu isipokuwa hawajakwenda kuhalalisha. Kuna waliozaa watoto wakalea na kuna wanaotupa watoto vyooni kila kukicha ama kuwatupa wakishawazaa lakini mi naona wote ni wale wale tu.

Sasa tofauti hapo ni ipi? Cheti kwamba aliolewa ama alama gani kwamba hakuwahi kuolewa? Na wale wanaozaa wanalea kwa utu na mapenzi wanabaki na watoto wao wakionekana wapo duniani, na wale wanaotoa mimba na kutupa watoto, kwako hapo tofauti ni ipi?

Muombe Mungu akusaidie vinginevyo, vigezo hivi ulivyoweka utajikuta umeangukia huko huko kubaya zaidi, kwa kudhani njigi si njege kumbe tui la nazi na maziwa.
 
Pole sana,hongera yataka moyo kuoa mwanamke aliyeisha achika kwa mumewe kwanza.......

Nakushauri tulia na jipange vizuri kukabiliana naye.....huo ni mwanzo tu,kama alimuacha wa kwanza akakupata wewe then anajua aweza mpata/kama si anaye mwingine.......

Muombe Mungu akulinde na aondoke salama,huna mke,una mwanamke unayeishi nae chini ya dari moja.......let her go....forgive....move on!!!!

Na kama yuko kwa dada yake na dada yake haoni tatizo,then hata ndugu zake hawana busara au labda hawakutaki......kama unampenda sana mpe muda uone,mshirikishe Mungu na wazazi na ndugu zako pia,watakushauri.

Wala si hivyo hayo ni mawazo yako mazuri tu but kunawatu wanaachka na wanaolewa na wanaishi vyema na waume zao. huyu anamatatizo yake tu
 
pole sana man ila kuachana ni suala la ninyi wenyewe tunaweza kukushauri hapa na bado baadae tukaona umemtafuta na mnaendelea kugonga mwanzo masuala ya mahusiano huwa ni magumu sana kuamuliwa na watu wa nje!!!ila kama aliolewa akaachika nashangaa kwanini ameshindwa kujifunza namna ya kuishi na mume sometimes ni kuvumiliana na kubebeana mizigo huwa ni hatari sana hasa mmoja wenu anapojifanya kidume kwa mwenzake!ila nakuaminia najua utaweka sawa tu mambo kama ni kweli kuna mapenzi ya dhati kati yenu!
nimeoa mwanamke aliyeisha olewa zamani na akaachika, maelewano na masikilizano ndani ya nyumba mwanzo yalikuwa mazuri, ukorofi ukaanza ghafla, akashika mimba akaenda itoa kisha akadai imetoka yenyewe, safari za kwenda kwao zikawa haziishi , na vitu vyake alivyokuja navyo kwangu akawa anahamisha kidogo kidogo kila nnapokuwa sipo.

Nilipomuuliza akadai yeye kuna mtu amemuazima pesa na ili akasome ndio kaamua na yeye amuazime vitu vyake kisha akimaliza kusoma ataenda kuvigomboa, nikamuuliza mbona mimi hukunishirikisha ktk hilo japo vitu ni vyako, basi kuanzia hapo ni makeke tu na hivi huyo hakufai achana nae kama aliishaachika na hakujifunza sasa wewe unaendelea nae wanini na katoa mimba yako hakuna upendo hapo tafuta mwingine au unampenda bado maana masuala ya mapenzi huwa ni magumu sana tunaweza kukushauri na bado tukashangaa umekiuka ushauri wetu!niongeapo yuko kwa dada yake yapata wiki na zaidi hakuna ugomvi zaidi ya hilo suala, jana ananiambia uko kimya hali ya kuwa unajua nahitaji kwenda kusoma huku sina hela nikueleweje, NIMEMWAMBIA KAMA UNAJUA MIMI NI MUMEO NAWAJIBIKA KWA HILO NI VIPI UKAE KWA DADA YAKO ...?

NIMEKATA MAWASILIANO NA YEYE KAKAA KIMYA ..........
 
HUMFANYI VIZURI NDIO MAANA ANALETA DHARAU,FANYA MAZOEZI YAKUNGONOKA UNGONOKE KIUKWELI ATATULIA Mwenyewe
 
Duu hiyo ya kutoa mimba ni kali... Au ndo watoto walionekana kwenye shimo moja karibu na Mwananyamala hospitali???? Huyo mke achana nae kabisa anza maisha mapya mzee. Kila la heri
 
Pole mkuu inawezekana huyo bibie ana kasumba na wanaume pia yuko ambaye anayemfanya awe dilema ila hawezi kukuambia ndio maana umekata mawasiliano na yeye yupo kimya kwani kwa upande wake ndicho alichokuwa akikihitaji
 
avatar31740_17.gif
You are very wise!
 
Pole sana mkuu.
Ni wazi ushapewa ishara ya kutokupendeka pale alipoichopoa mimba yako.
Pili mwanamke au mwanamme akishaachika/kuacha laima tuwe makini kuchunguza kabla ya kujiingiza katika mahusiano ya mapenzi. Mfupa uliomshinda Fisi mbwa atauweza? Alifika kwako kuja kuchuma then ale kona. "She was there only to use you then dump you" ndo maana nadai anataka aende shule hali yuko kwa dadake.:msela:
 
nimeoa mwanamke aliyeisha olewa zamani na akaachika, maelewano na masikilizano ndani ya nyumba mwanzo yalikuwa mazuri, ukorofi ukaanza ghafla, akashika mimba akaenda itoa kisha akadai imetoka yenyewe, safari za kwenda kwao zikawa haziishi , na vitu vyake alivyokuja navyo kwangu akawa anahamisha kidogo kidogo kila nnapokuwa sipo.

Nilipomuuliza akadai yeye kuna mtu amemuazima pesa na ili akasome ndio kaamua na yeye amuazime vitu vyake kisha akimaliza kusoma ataenda kuvigomboa, nikamuuliza mbona mimi hukunishirikisha ktk hilo japo vitu ni vyako, basi kuanzia hapo ni makeke tu na hivi niongeapo yuko kwa dada yake yapata wiki na zaidi hakuna ugomvi zaidi ya hilo suala, jana ananiambia uko kimya hali ya kuwa unajua nahitaji kwenda kusoma huku sina hela nikueleweje, NIMEMWAMBIA KAMA UNAJUA MIMI NI MUMEO NAWAJIBIKA KWA HILO NI VIPI UKAE KWA DADA YAKO ...?

NIMEKATA MAWASILIANO NA YEYE KAKAA KIMYA ..........

kaka unaumiza kichwa bure,mwanamke akishaanza ayo makeke hakuitaji tena ila anashindwa tu kukuambia mimi na wewe basi,usimsemeshe muangalie tu mpaka uone mwisho wake,ila uelewe tu uyo akufai
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom