Mke wangu hajui kupika wali

Mke wangu hajui kupika wali

Kwani we mikono huna?? Eboh!!kabla ya kumuoa ulikuwa hujui hilo? Mlikutana siku ya ndoa kanisani?? Huna mdomo wa kumwambia hadi uje umtangazie hapa?? Huyo ni mkeo au hawara??? Umemchoka?;???? Wanaume wengine bwana..!!!!
 
Umeoa mwanamke aliyekulia uzunguni ulitegemea nini........ Sisi waswahili wote tunajua kupika
 
Wali ni chakula ninachokipenda kuliko vyakula vyote duniani, kwa bahati mbaya naelekea kukichukia kwa sababu ya huyu mke.

Mwanzoni nilipomuoa alimleta housegirl kwa maana yeye anaenda kazini, huyo hg alikuwa ni mpishi mzuri na tuliishi naye karibu mwaka mzima,

Mimi sikuwa najua chakula wali siku zote ulikuwa unapikwa na hg ila nimejua hilo baada ya huyo hgal kuondoka na kuja mwingine ambaye ametoka kileji mambo ya mapochopocho ya town hayajui sawasawa.

Hii imelazimu muda mwingi wife ndio apike, sasa nilichogundua wife naye kupika ni ziro hasa ubweche,

Leo atapika bokoboko, kesho atapika mbichi, akipika bekitatu naye ni yaleyale, yapata miezi mitatu sasa sijala wali wa maana, sasa mnanishaurije nduguzanguni, nimtafute yule bekitatu aliyeondoka nimuweke ndani ili wife akae bench au mnaonaje? Nakonda mwenzenu
mnunulie rice cooker then uwe unamkadililia akipika roho una mkadilia na kipomo cha maji anachotakiwa kutumia hutakula mabokoboko Tena ....naimani mboga atakuwa anajua kupika vizuri tu
 
Dah,wali ulivyomtamu vile mkeo hawez kupika? kwel unakosa utamu mwingi sana
 
Hii nayo unataka ushauri.... Pika mwenyew au nenda kwa mama ntilie
 
Wali ni chakula ninachokipenda kuliko vyakula vyote duniani, kwa bahati mbaya naelekea kukichukia kwa sababu ya huyu mke.

Mwanzoni nilipomuoa alimleta housegirl kwa maana yeye anaenda kazini, huyo hg alikuwa ni mpishi mzuri na tuliishi naye karibu mwaka mzima,

Mimi sikuwa najua chakula wali siku zote ulikuwa unapikwa na hg ila nimejua hilo baada ya huyo hgal kuondoka na kuja mwingine ambaye ametoka kileji mambo ya mapochopocho ya town hayajui sawasawa.

Hii imelazimu muda mwingi wife ndio apike, sasa nilichogundua wife naye kupika ni ziro hasa ubweche,

Leo atapika bokoboko, kesho atapika mbichi, akipika bekitatu naye ni yaleyale, yapata miezi mitatu sasa sijala wali wa maana, sasa mnanishaurije nduguzanguni, nimtafute yule bekitatu aliyeondoka nimuweke ndani ili wife akae bench au mnaonaje? Nakonda mwenzenu
Mfundishe kupika
 
Beki tatu umuweke ndani kisa wife hajui kupika wali au kisa yeye ndo anaweza kupika wali ahaha we ni mnyakyusa au ni mtu wa pwani mpenda wali. usijaribu kufanya hivyo kwanza wewe mwenyewe ulitakiwa ujue kuupika huo wali halafu, wife anapotaka kupika uwe naye karibu ili umuelekeze unapoona amekosea au hajafanya vizuri sasa huenda na ww hauko vizuri, muite mama mzazi si anajua kupika wali mualike aje nyumbani atamsaidia mkeo pale ambapo atakuwa amekosea, au mlipie wife wako mafunzo ya mapishi ikiwemo na wali.
 
Nilijua kupika kwa mbinde sana kwanza mtihani mkubwa ni wali na ugali, nlichoka kula hotelini ila ilinilazimu kulazimisha kujua kupika, dada zangu walikuwa karibu sana na mm kunielekeza, sasa mara nyingi kama mnapikia kwenye mkaa ndio labda unampa changamoto kupika, ila mimi napikia jiko la gesi au jiko la mchina ndio naweza kwenye mkaa siwezi ku control huo moto. wanaume tujifunze kupika ili tuwasaidie wake zetu pale ambapo tunaona wameshindwa tuelekezane sio kutaka watu wa nje watusaidie watatusema nje huko kuwa hatuwezi, ujue mkeo hata siku moja asingeweza kupika wali ambao atakula huyo housegirl maana anajua atamsema huko nje kuwua hajui kupika.
 
Back
Top Bottom