Wali ni chakula ninachokipenda kuliko vyakula vyote duniani, kwa bahati mbaya naelekea kukichukia kwa sababu ya huyu mke.
Mwanzoni nilipomuoa alimleta housegirl kwa maana yeye anaenda kazini, huyo hg alikuwa ni mpishi mzuri na tuliishi naye karibu mwaka mzima,
Mimi sikuwa najua chakula wali siku zote ulikuwa unapikwa na hg ila nimejua hilo baada ya huyo hgal kuondoka na kuja mwingine ambaye ametoka kileji mambo ya mapochopocho ya town hayajui sawasawa.
Hii imelazimu muda mwingi wife ndio apike, sasa nilichogundua wife naye kupika ni ziro hasa ubweche,
Leo atapika bokoboko, kesho atapika mbichi, akipika bekitatu naye ni yaleyale, yapata miezi mitatu sasa sijala wali wa maana, sasa mnanishaurije nduguzanguni, nimtafute yule bekitatu aliyeondoka nimuweke ndani ili wife akae bench au mnaonaje? Nakonda mwenzenu