You are a man japokuwa sijui wewe ni ke au me aisee. Big up. ID zetu feki zisiondoe ubinadamu wetu. Nimejifunza katika maisha kutoropoka kuhusu mambo ya siri ya watu wangu wa karibu si baba si mama si kaka wala dada si mpenzi, maana baadae aibu inakurudia wewe.
Sikiliza mkuu mapenzi ni mfumo. Na hizi ni tabia za mifumo:
1. Ukitoa taarifa nyeti za mfumo wowote duniani, mfumo huo uko hatarini kuharibika. Ndio maana watu wa maana huwa hawaropoki madhaifu au mazuri ya wake zao au waume zao, maana wanajua wakiropoka watu fulani wakajua tayari hiyo ni nafasi ya mfumo wao kuharibiwa na michepuko.
2. Mfumo wowote hua unalenga kuwa na mlingano. Ndio maana unapokuwa wewe dhaifu mkeo au mpenzio anasimama badala yako na wewe pia hivyo hivyo mnatakiwa mbalance aisee.
3. Hizo zinakutosha kwa leo....