Mke wangu anataka kurudi kwao

Mke wangu anataka kurudi kwao

Joined
Apr 23, 2016
Posts
67
Reaction score
195
Wadau shalom

Bwana asifiwe

Mwaka 2014 mke wangu aliingiwa na tamaa yeye na wenzie wakajitenga na kanisa wakaenda kufungua huduma yao mahala pengine, hawakua na eneo hivyo wakawa wanatumia darasa la Shule ya msingi hadi sasa wako humo, aliendelea kuishi na mm kwa miezi kama 2 hivi baadae akabeba kila chake akaondoka

Baada ya mwaka Bwana akawa amenifunulia nichukue mdogo wake ambae yeye hakuhama kanisa kumfuata dada yake, basi tangu mwaka Jana mwezi may tunaishi pamoja na huyu mdogo wake Kutokana na MUNGU kutufunulia hivyo katika maono, kukawa na kama mgogoro hivi maana ukoo wao wote waliamia kule kwa mke wangu wa awali pamoja na wakwe zangu wanaabudu huko sasa hivi,

Hivi karibuni mke wangu mpya anadai amechoka na ugomvi na amechukiwa na wazazi wake kwa sababu amebaki kwangu sasa ameona hawezi kuendelea hivi, hivyo yeye ameona arudi ahamie kwa dada yake Ingawa ana mimba yangu kubwa tu, anasema ameona akapatane na dada yake akaenda kuomba msamaha , hawawezi kuishi kwa uhasama, hivyo akawa ameondoka mwanzo wa hii wiki,
Nikawa nimeomba kikao nao wote kujua hatma ya watoto wangu wawili na huyo ambae hajazaliwa, wamenijibu hovyo sana kwamba Sina changu, ila huyu mjamzito inaonekana yy anasukumwa tu bado ananipenda

Hata Kuna wakati nilisingiziwa kutembea na mke wa muumini wangu kumbe ni yule aliekua mke wangu aliehama kanisa ndie pamoja na wenzie wachache ndio walitengeneza Mpango ule ili niondolewe kama mchungaji mkuu iliposhindikana ndipo wakaenda kuanzisha huduma yao, lakini MUNGU akanipigania bado huduma yangu ndio kubwa wao bado wanasali kwenye darasa, sasa wameamua wamrubuni huyu binti (mke wangu wa sasa) na wamemtoa wanae huko wanadai watamtenga hivyo akaogopa, ila kwa kweli mm nampenda sana, tangu ameondoka jumatatu naumwa homa kali sana, sijatoka hata ndani, sikua najua nampenda huyu binti kiasi hiki alivyoondoka juzi

Sasa watu wa MUNGU sijui mnanishauri nifanyeje, niweze kupata haki yangu bila kudhuru image ya kanisa letu, na huyu binti nifanyeje aweze kurudi maana hata kula imekua shida kwangu,
Sasa hivi wamenibadilishia kibao wanadai nimemsaliti ndoa kwa kuchukua mdogo wa mke wangu wakati yeye ndie alikimbia nyumba
 
Pole sana mkuu, mkeo wa mwanzo mlifunga naye ndoa?? Baada ya kuondoka kwako ulimpa talaka? Je umezaa na mkeo wa mwanzo?
 
Wewe unaejiita mchungaji ulishawahi hata siku moja ukakaa ukaisoma Bible ukaelewa vizuri kilichoandikwa kuhusu ndoa na mafundisho yake au unaisoma kwa kutusua tusua baadhi ya vipengele ili ukawatoze waamini sadaka...yaani unamchukua mdogo wa mkeo unazini nae na kumzalisha unataka kumzalisha ila huoni kosa lako unakimbilia kuomba msaada humu?!katubu hiyo dhambi kwa Mungu wako muombe msamaha mkeo mkae myamalize ishi vile ndoa inataka acha ujanja ujanja na acha ujinga.(najua ukiisoma post yangu utajisemea nina pepo,ndo zenu hizo)
 
Sasa si urudi kwa mungu aliyekufunulia akupe ufumbuzi? Sisi hili jambo liko juu ya uwezo wetu kama wanadam...
Umenena vyema mkuu.Kwa sababu inaonekana Mchungaji huwa anapata maono kabla ya kufanya maamuzi kwa sababu hata mke wake alivyokimbia hakuja kutuomba ushauri bali alipata tu maono kutoka huko kwa Lusifa kuwa amchukue huyo mdogo wa mke wake. Kwa hili bora atulie tu ili maono yaje tena huenda yakamshauri kitu kizuri zaidi.
 
Wadau shalom

Bwana asifiwe

Mwaka 2014 mke wangu aliingiwa na tamaa yeye na wenzie wakajitenga na kanisa wakaenda kufungua huduma yao mahala pengine, hawakua na eneo hivyo wakawa wanatumia darasa la Shule ya msingi hadi sasa wako humo, aliendelea kuishi na mm kwa miezi kama 2 hivi baadae akabeba kila chake akaondoka

Baada ya mwaka Bwana akawa amenifunulia nichukue mdogo wake ambae yeye hakuhama kanisa kumfuata dada yake, basi tangu mwaka Jana mwezi may tunaishi pamoja na huyu mdogo wake Kutokana na MUNGU kutufunulia hivyo katika maono, kukawa na kama mgogoro hivi maana ukoo wao wote waliamia kule kwa mke wangu wa awali pamoja na wakwe zangu wanaabudu huko sasa hivi,

Hivi karibuni mke wangu mpya anadai amechoka na ugomvi na amechukiwa na wazazi wake kwa sababu amebaki kwangu sasa ameona hawezi kuendelea hivi, hivyo yeye ameona arudi ahamie kwa dada yake Ingawa ana mimba yangu kubwa tu, anasema ameona akapatane na dada yake akaenda kuomba msamaha , hawawezi kuishi kwa uhasama, hivyo akawa ameondoka mwanzo wa hii wiki,
Nikawa nimeomba kikao nao wote kujua hatma ya watoto wangu wawili na huyo ambae hajazaliwa, wamenijibu hovyo sana kwamba Sina changu, ila huyu mjamzito inaonekana yy anasukumwa tu bado ananipenda

Hata Kuna wakati nilisingiziwa kutembea na mke wa muumini wangu kumbe ni yule aliekua mke wangu aliehama kanisa ndie pamoja na wenzie wachache ndio walitengeneza Mpango ule ili niondolewe kama mchungaji mkuu iliposhindikana ndipo wakaenda kuanzisha huduma yao, lakini MUNGU akanipigania bado huduma yangu ndio kubwa wao bado wanasali kwenye darasa, sasa wameamua wamrubuni huyu binti (mke wangu wa sasa) na wamemtoa wanae huko wanadai watamtenga hivyo akaogopa, ila kwa kweli mm nampenda sana, tangu ameondoka jumatatu naumwa homa kali sana, sijatoka hata ndani, sikua najua nampenda huyu binti kiasi hiki alivyoondoka juzi

Sasa watu wa MUNGU sijui mnanishauri nifanyeje, niweze kupata haki yangu bila kudhuru image ya kanisa letu, na huyu binti nifanyeje aweze kurudi maana hata kula imekua shida kwangu,
Sasa hivi wamenibadilishia kibao wanadai nimemsaliti ndoa kwa kuchukua mdogo wa mke wangu wakati yeye ndie alikimbia nyumba
yaninimechekakweli dah ...wauminisijui wachungaji wa sa hivi kweli usanii.....
 
Back
Top Bottom