Usiache kunijuza maendeleo
<br /> <br / mtandike kama humjui then mtimulie mbali, mke gani anamegwa hovyohovyo? Hy hana tofauti na jibwa koko.IGWE jua kwamba huyu sio demu wangu, ni MKE wa ndoa na hapo ndipo nashindwa nifanye nini na kuamua kuwaomba ushauri
Achana na Facebook.
Facebook imekuwa chanzo cha mitafaruku mingi sana kwenye mahusiano. Mimi kama mimi sipo huko Facebook. Nipo ila nipo ki JF zaidi. Natumia jina la Nyani Ngabu na hata hivyo sijaingia huko tokea sijui lini..hata sikumbuki.
Watu huko huuza sura tu. Kila leo wanabandika mapicha yao halafu wanasubiri kumwagiwa misifa...ooh sijui you are beautiful...sijui I miss you...mara you look gorgeous...sasa kaka hebu fikiria kidogo. Yaani kama una mwenzako yuko huko halafu minjemba inamwagia misifa hivyo utapata amani kweli moyoni na akilini mwako? Vivyo hivyo kwako. Kama wachuchu wanakumwagia misifa kem kem mkeo au mpenzio unadhani atakuwa na amani kweli? Mimi sidhani hata kidogo.
Uamuzi wa mwisho ni wako. Ukiamua kubaki..poa tu...ukiamua kuachana nayo...na yenyewe haina ubaya. Mwisho wa siku pima uone jambo lipi ni la muhimu zaidi na fanya uamuzi kulingana na majibu utakayopata.
<br /> <br / mtandike kama humjui then mtimulie mbali, mke gani anamegwa hovyohovyo? Hy hana tofauti na jibwa koko.
huwezi kuishi bila FB? wengine tulishasahau kitu inaitwa FB!!
NN twapaswa kutatua tatizo badala ya kulikimbia...... Atakimbia social networks ngapi? Maendeleo yatakua yanasonga sisi tunarudi hatua tatu nyuma na kujipongeza kama alivyosema Prof J.....
Kimsingi hapo jamaa yeye ndo anajua root of the prob. Naamini hajasema yote...... Ameonyesha kidogo tu kwamba there's a marital infidelity...... Kutoka kwa wote na hususani kwa mwenza wake.... Na it appears hawajakaa na kuongea.... Anasubiri wamarekani watoe tena mafungu ya matangazo ya kuhamasasisha wanandoa au waliok ktk uhusiano kukaa na ku-discuss kuhusu mahusiano yao??????????
Kwangu Facebook haina umuhimu wowote na siifagilii. Ninaweza kuishi bila nayo.
kumbuka alianzia katika simu, je ningeacha kutumia simu ili yaishe? akahamia kuwa nina wapenzi kazini, je ningeacha kazi pia ili aniamini?
Mie Mlutheri, Mke mmoja maisha yote na hapo ndipo pananikosesha amani kila ninapofikiria kumuacha
NN kumbuka huko awali aliwahi kunituhumu kwa kutumia simu, je ningeacha kutumia simu? n baadae akadai kazini nina wapenzi, je ningeacha kazi pia? leo faceboo na kesho itakuwa kingine, kila kitu niwe nakiacha??
Kwani ulikuwa unaificha ficha na kumkataza kuishika simu yako?
Hii story ya upande mmoja.why mkeo akufuatilie.inawezekana na ww hujatulia
Sijamkataza, lakini ilikuwa akiishika asione msg toka kwa msichana yoyote hata ikiwa ni salamu tu patachimbika. baada ya simu kahamia kazini eti kaambiwa nano nina wanawake kibao
Lakini kwa nini kama umeoa uachie/ uruhusu wasichana wawe wanakutumia salamu kwenye simu yako? Wewe huoni kama ulimpa sababu ya kukushuku?
Jamani waungwana naomba msaada wenu huyu mke wangu mie simuelewi kabisa.
mwanzoni mwa mahusiano yetu alikuwa na tabia sana ya kuchunguza simu yangu na hakuwahi kugundua message yoyote mbaya ingawa hata msg isiyo ya kimapenzi ikiingia kwenye simu yangu so long as inatoka kwa mwanamke basi siku hiyo ni vurugu kupita kiasi akidai huyo mwanamke atakuwa bibi yangu ama mpenzi wangu tu. siku mie niliposhika simu yake siku moja, nikagundua msg nyingi za kimapenzi toka kwa wanaume wawili tofauti, anaomba radhi nikamsamehe.
Baada ya muda alikuwa akinisumbua kwa kudai kuwa mimi nina uhusiano na wanawake chungu tele kuanzia wale ninaofanya nao kazi hadi mtaani. Baada ya kuchunguza nikagundua kumbe yeye ndio ana mahusiano ya kimapenzi na rafiki yangu. mini ni mvumilivu nilimsamehe ingawa ni baada ua kukana sana na mwisho wa siku akakubali. hayo yakaisha mwaka jana.
Sasa hivi amekuja na mpya. Anasema kila mwanamke ambaye ni rafiki yangu facebook kwamba ni bibi yangu na anakomaa kwelikweli. mie nashindwa hata nimwambie nini ili aamini kuwa mawazo yake sio kweli maana kuna wasichana zaidi ya 1000 kwenye orodha ya marafiki zangu fb na wavulana kama 1000 wengine. kila comment yangu kwa mwanamke yoyote inakuwa ugomvi hauna mfano, kisa eti na comment kwa bibi yangu. kwakweli sina amani kabisa na hali hii inanikosesha raha.
Naomba waungwana mnisaidie nifanye nini maana nahisi kama anaanza tena kuficha uovu wake kwa kunipakazia mie, nahisi tu hilo sijafanya uchunguzi tena.
NN unataka kusema kwakuwa nimeoa basi sitakiwi kusalimiwa na wasichana wa aina yoyote? mfano wale tuliosoma nao, wale tunaotoka nao kijiji kimoja ama mkoa mmoja? wale niliowahi kukutana nao kwenye mikutano ya kikazi il mradi tu eti mke wangu asione nawasiliana na msichana yoyote???? Tena sio msg ya mapenzi ama dalili ya kuwepo mapenzi, salamu tu???