Ng'wanamangilingili
JF-Expert Member
- Aug 22, 2015
- 5,705
- 4,739
Arusha. Mke wa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, Jesca Thomas (28) ameieleza Mahakama namna walivyokamatwa na mume wake na askari waliokuwa na silaha jijini Dar es Salaam.
Jesca ambaye ni shahidi wa pili wa utetezi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Sabaya na wenzake sita ameieleza Mahakama kuwa alikamatwa na mume wake Mei 27 mwaka jana jijini Dar es Salaam ambapo alidai kabla ya kukamatwa walipekuliwa na askari hao waliokuwa wamevalia kiraia huku wakiwa na silaha.
Leo Januari 17, 2022 akiongozwa na Wakili Mosses Mahuna anayemtetea Sabaya, Jesca alijitambulisha mahakamani hapo kuwa ni mke wa mshitakiwa huyo na walifunga ndoa mwaka 2018
"Tukiwa chumbani walikuja watu usiku, walikuwa wanagonga kwa nguvu sana na hawakusubiri kufunguliwa walitumia njia zao wakaingia ndani ilikuwa ni saa 10 jioni. Walivyoingia Lengai akauliza ni nini na ni nani nyie, wakajibu wakasema ni askari wakatuamuru tukae sehemu moja,"
"Wengine wakawa wanapekua kabati mabegi wakatoa na godoro wakapekua kila mahali, vurugu kila kitu kikavurumushwa kule ndani,walivyomaliza wakasema tunaondona na nyie tunaenda Takukuru,na hawakutufahamisha chochote kabla ya kutupekua," amedai
Shahidi huyo amedai mahakamani hapo kuwa walikamatwa wao wawili na baada ya kutoka makao makuu ya Takukuru, Upanga walisafirishwa Juni 3 usiku na kufikishwa Arusha ambapo pamoja na vitu vingine walikabidhi gari aina ya Land Cruiser V8, lenye namba za usajili T 222 BDY ambayo walikutwa nayo, pesa pamoja na simu.
Amedai gari hilo Sabaya alinunua Oktoba 2020 kutoka kampuni ya Oil Com na ambaye alisimamia mauziano hayo alimtaja kwa jina la Said.
Kuhusu namba ya simu 0758 707171 inayodaiwa kuwa ya Sabaya, Jesca ameieleza mahakama kuwa namba hiyo imesajiliwa kwa jina la mume wake na wamekuwa wakiitumia wote ambapo yeye anaitumia kwa ajili ya kufanya biashara.
Akihojiwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Ofmed Mtenga shahidi huyo alidai kuwa wana magari mawili ambayo yote ni Land Cruiser VX V8 yote yanashikiliwa Takukuru
Chanzo: Mwananchi
----
My Take: Bwana ndogo anahangaika kweli kweli na hizi kesi zake mara baada ya mahakama kuthibisha ana kesi ya kujibu,nakumbuka wakati anaomba apunguziwe adhabu katika hukumu alidai hajaoa na anatarajiwa kufunga ndoa ana mchumba. Kumbe alikua na jiko tayari.’@“&€.
Ukipitia mahojiano ya mawakili na shahidi ambaye ndiye ‘mke wake’ yanatia sintofahamu lukuki utafikiri si mumewe ama kaokotwa tu kuja kuunga unga mahakamani.
Viongozi na wateuliwa tukumbuke madaraka yanapita na utu unabaki inategemea ntu na ntu yaani askari wale wale uliokua unawapa command kuvamia, kukamata na kutesa watu, kukupigia salute then hao hao wanakuja kukupiga tanganyika jeki! Yananikumbusha ya Masha enzi zile alivyosukumizwa kwenye karandika nyuma kwa tanganyika jeki wakati ndio alikuaga waziri wa mambo ya ndani.
Jesca ambaye ni shahidi wa pili wa utetezi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Sabaya na wenzake sita ameieleza Mahakama kuwa alikamatwa na mume wake Mei 27 mwaka jana jijini Dar es Salaam ambapo alidai kabla ya kukamatwa walipekuliwa na askari hao waliokuwa wamevalia kiraia huku wakiwa na silaha.
Leo Januari 17, 2022 akiongozwa na Wakili Mosses Mahuna anayemtetea Sabaya, Jesca alijitambulisha mahakamani hapo kuwa ni mke wa mshitakiwa huyo na walifunga ndoa mwaka 2018
"Tukiwa chumbani walikuja watu usiku, walikuwa wanagonga kwa nguvu sana na hawakusubiri kufunguliwa walitumia njia zao wakaingia ndani ilikuwa ni saa 10 jioni. Walivyoingia Lengai akauliza ni nini na ni nani nyie, wakajibu wakasema ni askari wakatuamuru tukae sehemu moja,"
"Wengine wakawa wanapekua kabati mabegi wakatoa na godoro wakapekua kila mahali, vurugu kila kitu kikavurumushwa kule ndani,walivyomaliza wakasema tunaondona na nyie tunaenda Takukuru,na hawakutufahamisha chochote kabla ya kutupekua," amedai
Shahidi huyo amedai mahakamani hapo kuwa walikamatwa wao wawili na baada ya kutoka makao makuu ya Takukuru, Upanga walisafirishwa Juni 3 usiku na kufikishwa Arusha ambapo pamoja na vitu vingine walikabidhi gari aina ya Land Cruiser V8, lenye namba za usajili T 222 BDY ambayo walikutwa nayo, pesa pamoja na simu.
Amedai gari hilo Sabaya alinunua Oktoba 2020 kutoka kampuni ya Oil Com na ambaye alisimamia mauziano hayo alimtaja kwa jina la Said.
Kuhusu namba ya simu 0758 707171 inayodaiwa kuwa ya Sabaya, Jesca ameieleza mahakama kuwa namba hiyo imesajiliwa kwa jina la mume wake na wamekuwa wakiitumia wote ambapo yeye anaitumia kwa ajili ya kufanya biashara.
Akihojiwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Ofmed Mtenga shahidi huyo alidai kuwa wana magari mawili ambayo yote ni Land Cruiser VX V8 yote yanashikiliwa Takukuru
Chanzo: Mwananchi
----
My Take: Bwana ndogo anahangaika kweli kweli na hizi kesi zake mara baada ya mahakama kuthibisha ana kesi ya kujibu,nakumbuka wakati anaomba apunguziwe adhabu katika hukumu alidai hajaoa na anatarajiwa kufunga ndoa ana mchumba. Kumbe alikua na jiko tayari.’@“&€.
Ukipitia mahojiano ya mawakili na shahidi ambaye ndiye ‘mke wake’ yanatia sintofahamu lukuki utafikiri si mumewe ama kaokotwa tu kuja kuunga unga mahakamani.
Viongozi na wateuliwa tukumbuke madaraka yanapita na utu unabaki inategemea ntu na ntu yaani askari wale wale uliokua unawapa command kuvamia, kukamata na kutesa watu, kukupigia salute then hao hao wanakuja kukupiga tanganyika jeki! Yananikumbusha ya Masha enzi zile alivyosukumizwa kwenye karandika nyuma kwa tanganyika jeki wakati ndio alikuaga waziri wa mambo ya ndani.