Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,005
- 9,872
Mkuu wa Wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe amesema, Lazaro Nyalandu amezuiwa Namanga kwasababu hakuwa na nyaraka muhimu na atafikishwa Mahakamani endapo atashindwa kuwasilisha nyaraka hizo.
Mke wa Lazaro Nyalandu, Faraja Kotta Nyalandu amesema wao wanaishi Arusha na mumewe hahitaji nyaraka ili kufanya shughuli zake akiwa upande wa Tanzania na wala hakuwa na mpango wa kuvuka mpaka wa nchi.
Pia amesema tukio hilo halikutokea Novemba 9, kama ilivyoripotiwa bali lilitokea Novemba 6.
Lazaro Nyalandu alikuwa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia CHADEMA. Iliripotiwa kuwa anashikiliwa na Maafisa Uhamiaji wa Tanzania kwa tuhuma za kutaka kuondoka nchini bila nyaraka muhimu.
Mke wa Lazaro Nyalandu, Faraja Kotta Nyalandu amesema wao wanaishi Arusha na mumewe hahitaji nyaraka ili kufanya shughuli zake akiwa upande wa Tanzania na wala hakuwa na mpango wa kuvuka mpaka wa nchi.
Pia amesema tukio hilo halikutokea Novemba 9, kama ilivyoripotiwa bali lilitokea Novemba 6.
Lazaro Nyalandu alikuwa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia CHADEMA. Iliripotiwa kuwa anashikiliwa na Maafisa Uhamiaji wa Tanzania kwa tuhuma za kutaka kuondoka nchini bila nyaraka muhimu.