Lucky One
JF-Expert Member
- Nov 27, 2013
- 663
- 431
Habarini za asubuhi wanajamvi,
Natumaini mmeamka vyema katika siku hii.
Kama kichwa cha habari kilivyo ni kwamba nimekuwa nipo katika mtanziko kuelewa kuwa mke mwema mtu humsubiria tu bila kuhangaika au inambidi mtu atafute mwenyewe.
1. Mke mwema huja kwa kumsubiria tu bila kuhangaika
Katika dhana hii kwa wakristo, watu husema inambidi mtu atulie tu maana Mungu kwa wakati wake atampatia mke mwema. Hoja kubwa hapa ni kwamba Adamu binadamu wa kwanza alilala tu kisha Mungu akampatia mwanamke na alipomuona akasema huyu ni nyama ya nyama yangu na mifupa ya mifupa yangu. Hivyo katika muktadha huu watu husema mtu hatakiwi kuhangaika kutafuta mke bali Mungu kwa wakati wake atampatia mtu mke mwema.
2.Mke mwema huja kwa bidii ya kutafuta
Hapa watu husema mke mwema hupatikana kwa bidii ya mtu mwenyewe kutafuta. Hivyo mtu anatakiwa ajue jinsi ya kumshawishi mtu awe mke wake katika hili watu hupinga kwamba kuna mke ambaye mtu humsubiria bali mtu mwenyewe anatakiwa afanye jitihada.Kulingana na maelezo haya nilikuwa naomba kusikia kutoka kwa wanandoa au watu ambao washapata wenzi na wanamatarajio ya ndoa,je mlifanya jitihada za kutafuta au mlisubiria tu?
Karibuni kwa michango.
Natumaini mmeamka vyema katika siku hii.
Kama kichwa cha habari kilivyo ni kwamba nimekuwa nipo katika mtanziko kuelewa kuwa mke mwema mtu humsubiria tu bila kuhangaika au inambidi mtu atafute mwenyewe.
1. Mke mwema huja kwa kumsubiria tu bila kuhangaika
Katika dhana hii kwa wakristo, watu husema inambidi mtu atulie tu maana Mungu kwa wakati wake atampatia mke mwema. Hoja kubwa hapa ni kwamba Adamu binadamu wa kwanza alilala tu kisha Mungu akampatia mwanamke na alipomuona akasema huyu ni nyama ya nyama yangu na mifupa ya mifupa yangu. Hivyo katika muktadha huu watu husema mtu hatakiwi kuhangaika kutafuta mke bali Mungu kwa wakati wake atampatia mtu mke mwema.
2.Mke mwema huja kwa bidii ya kutafuta
Hapa watu husema mke mwema hupatikana kwa bidii ya mtu mwenyewe kutafuta. Hivyo mtu anatakiwa ajue jinsi ya kumshawishi mtu awe mke wake katika hili watu hupinga kwamba kuna mke ambaye mtu humsubiria bali mtu mwenyewe anatakiwa afanye jitihada.Kulingana na maelezo haya nilikuwa naomba kusikia kutoka kwa wanandoa au watu ambao washapata wenzi na wanamatarajio ya ndoa,je mlifanya jitihada za kutafuta au mlisubiria tu?
Karibuni kwa michango.