Mke Mtarajiwa Anatafutwa

Masulupwete

JF-Expert Member
Feb 15, 2012
2,366
2,397
Masharti haya hapa

»Awe tayari kufunga ndoa nami mapema iwezekanavyo ikibidi wiki ya pili au ya tatu baada ya kukutana. Sitaki maswali kwa hili nina sababu zangu.

»Awe mstaarabu, wale wa macho juu juu kaeni mbali sana.

»Dini yoyote, ila nakula "ile kitu" so akubali japo kuniandalia tu.

»Awe mrefu, nipo siriazi kwenye hili maana mwenyewe mfupi, sitaki kuongeza mbegu fupi kwenye ukoo wetu. So wafupi kaeni mbali sana na nyuzi hii (ikiwezekana pointi hii iwe ya mwisho kwenu kusoma).

»Elimu sio ishu sana, ila ajue kusoma na kuandika.

»Awe hajazaa. Hapa nitakagua sana nisije kuchomekewa. Kifupi sitaki "mchicha mwiba" nasikia wasumbufu sana. Umri huu siko tayari kuambiwa "we masu mbona uko slow hivo mbona mwenzio makambo hakuwaga hivo".

»Umri awe 18-37. Wangu ni 40. Hapa viserengeti na vikongwe sana msijisumbue.

»Mambo ya kupimana afya sitaki, najiamini niko vizuri ila ahakikishe ana afya njema.

»Awe kaishi mjini ikiwezekana maisha yake yote. Nimepewa siri hawa wanajua sana bajeti sio kama wenzao wale wa kule mbalamaziwa, nsendakanoge, ikwiriri, litumbakuhamba n.k.

DM ikowazi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom