ndege JOHN
JF-Expert Member
- Aug 5, 2015
- 23,667
- 57,077
Watu wakubwa wananishauri nikitaka mke wa kuoa nitulie kwamba nikimuomba Mungu atamleta na kunionyesha kuwa huyu ndiye.sasa Mimi sijawahi kujua Kama namna Mungu anavyoongea na wanaume na kuwaonyesha wanawake wazuri,wake wazuri.nachojua unatakiwa tu wewe ndio uchague mzuri na umuombe muoane.ukisema usubiri Mungu akuonyeshe Ni kujidanganya.utavuna unachopanda.ni heri uchague mke ambaye wewe unaona Ni mrembo Sana hata Kama umesikia Ana tabia mbaya.kuliko uoe mwanamke ambaye sio mrembo hata akikukosea unaona vigumu kumsamehe.kwa sababu kwanza tabia me naamini zinaweza kubadilika muda wowote.kuna sababu internal na zike external.hakafu unakuta Kuna wadada wengine wanafahamika kwa vitabia vingi vibaya wanasemwa vibaya japo Ni vitabia ambavyo havina madhara Sana kwa upande wa mahusiano yenu. lakini Kuna ambao unawaona Ni wapole wa usoni ukadhani Wana tabia nzuri kumbe wana Mambo Yao siri makubwa na mabaya yasiyofahamika japo kwa nje Wana nidhamu.sasa kwa bahati mbaya Mungu hajatengeneza system ya kujua tabia zote za mtu au mawazo awazayo mtu.kwa hiyo Mungu anatoaje maono.maana Kuna jamaa yangu ananiambia kwamba mke analetwa na Mungu na huna haja ya kuforce au kumtongoza inakuja tu automatic anakuwa mke mwema
