Mke hataki nimpe mimba nyingine!

Mke hataki nimpe mimba nyingine!

Mtego wa Noti

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2010
Posts
2,633
Reaction score
1,657
Mimi namshangaa huyu mke wangu! nimezaa naye mtoto mmoja ila alijifungua kwa njia ya upasuaji miaka miwili iliyopita. kwa sasa mtoto keshakuwa mkubwa maana ana umri wa miaka miwili na mimi nilitaka nimpe mimba nyingine ili azae halafu ndio tupange mipango mingine ya maisha.

Cha kushangaza sasa ni kuwa kila ikifika muda wa yeye kupata mimba hukwepa sana ikiwemo kutaka tutumie zana ili asipate mimba.

Nishamwambia tupate mtoto mwingine ili tupumzike kabisa ili mwili wake upate nguvu aruie hali yake ya usichana lakini hataki kunielewa ati anataka tuzae mtoto mwingne baada ya miaka mitano! huku si kutaka kunifanya nikatafute nyumba ndogo ya kuzaa nayo ili niweze kujiongezea familia?

Au mwanamke anapojifungua kwa oparesheni inatakiwa akae miaka mingapi ndio apate ujauzito mwingine!
Kwa kweli nashindwa kumuelewa huyu mwanamke!
 
miaka miwili? mbona bado bado. ingekuwa alizaa njia ya kawaida sawa..
 
ulimuuliza sababu kwanini ataka hivyo akasema je ? Au wewe unataka kulazimisha hata huongei naye unadhani hizi ni zama za mwanaume kuamua tu?
 
ulimuuliza sababu kwanini ataka hivyo akasema je ? Au wewe unataka kulazimisha hata huongei naye unadhani hizi ni zama za mwanaume kuamua tu?
mimi simlazimishi ila ninachomwambia ni ukweli mtupu na yeye anadai bado sana kupata mimba, ifanyeje? kwani huo muda wa miaka miwili hawezi kupata ujauzito mwingine?
 
Hukutushirikisha wakati unampa mimba ya kwanza so endelea exparte hivohivo!pia kabla hujatafta nyumba ndogo fikiria ungekuwa ndo wewe umefanyiwa upasua afu jamaa anakupa mimba baada ya miaka miwili tu???hapo huja tuambia ameacha kunyonyesha lini??au ndo broila???vuta subira kaka mpe miaka mingine miwili so far anakupa unyumba haina taabu
 
Hukutushirikisha wakati unampa mimba ya kwanza so endelea exparte hivohivo!pia kabla hujatafta nyumba ndogo fikiria ungekuwa ndo wewe umefanyiwa upasua afu jamaa anakupa mimba baada ya miaka miwili tu???hapo huja tuambia ameacha kunyonyesha lini??au ndo broila???vuta subira kaka mpe miaka mingine miwili so far anakupa unyumba haina taabu
mh! mgumu kumesa lakini!
 
haina haja ya nyumba ndogo...we msikilize mwenzio usiwe na haraka mweleweshe taratibu tu ipo siku atakubali.........na ujitahidi kufahamu kwanini hataki.
 
Hataki kuzeeka na bandika bandua za mimba na hiyo nyumba ndogo itafute tu maana utakua unaikomoa familia yako sio sisi
 
Hili si jambo la wewe kutaka na lazima liwe - Ni swala la nyie wawili kujadiliana/kupeana hoja hadi mwafaka upatikane. Usiwe dikteta wakati anayekula kisu ni mwenzio.
 
mkuu kumbuka kuwa hiyo mimba nyingine itakuwa tena kwa operesheni. Just imagine muda mfupi aliokula kisu then mapema tena hivi akachanwe tena. Vile vile kama usemavyo operation huwa inaanza kupona kwa nje, then ndan taratibu taratibu. Mvutie subira walau mtoto afikishe 4yrs tafadhali.
 
Inatakiwa kwa kuanzia miaka mitatu baada ya operation sababu kubwa ni kwamba mshono kwenye kizazi unaweza kufumuka ikiwa atabeba haraka haraka pia kurudisha afya ya mama umewahi kusikia child spacing? Wewe mtoto anatakiwa anyonye miaka 2 1/2 sasa we ametimza
 
2PAC Keep ya Head Up
I wonder why we take from our women
Why we rape our women, do we hate our women?
I think it's time to kill for our women
Time to heal our women, be real to our women
And if we don't, we'll have a race of babies
That will hate the ladies, that make the babies
And since a man can't make oneHe has no right to tell a woman when and where to create one



 
thread kama hii ni ubabe mtupu, ni kwa nn wewe huwezi ukamsikiliza mwenzio kama vip beba mimba wewe. mwenzio kafanyiwa upasuaji katolewa mtoto afu unataka kumzalisha kabla hata ya miaka mitatu? unamtishia nyao kwenda nyumba ndogo? nenda mbona unachelewa.
 
hivi unampenda kweli mkeo au? Sbb nahs kama umemfanya kiwanda cha kutaka kuzalisha watoto bila kufikiria na yeye sbb zake. Inatakiwa wakati wa kujifungua kwake na wewe uwepo uone shuluba yake ndo utaheshim maamuzi yake
 
Mtego wa Noti.. Pole kwa yanayokusibu.. Kutafuta nyumba ndogo ni kutafuta tu excuse.

Kaaa na mkeo mjadiliane ujue kwanini hayuko tayari kwa sasa. Kubeba ujauzito ni suala linalotaka utayari sana kimwili na hata kiakili.

Wakati mwingine.. Ujauzito unakuja na majeraha mengi ya kimwili na nafsi ambayo hayafutiki kirahisi.. ..(Kwa huduma za uzazi zitolewazo tz ... mimba imekuwa kama njia ya kifo lolz.. Hivyo husababisha wasiwasi mwingi).

Majeraha mengine huwa mnayasababisha ninyi kinababa.. Hili linamfanya mama afikirie mara mbilimbili. Inabidi umpe matumaini pamoja na kuonyesha utayari wako katika kumsuport kwa kipindi chote.


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mimi namshangaa huyu mke wangu! nimezaa naye mtoto mmoja ila alijifungua kwa njia ya upasuaji miaka miwili iliyopita. kwa sasa mtoto keshakuwa mkubwa maana ana umri wa miaka miwili na mimi nilitaka nimpe mimba nyingine ili azae halafu ndio tupange mipango mingine ya maisha.
Cha kushangaza sasa ni kuwa kila ikifika muda wa yeye kupata mimba hukwepa sana ikiwemo kutaka tutumie zana ili asipate mimba. Nishamwambia tupate mtoto mwingine ili tupumzike kabisa ili mwili wake upate nguvu aruie hali yake ya usichana lakini hataki kunielewa ati anataka tuzae mtoto mwingne baada ya miaka mitano! huku si kutaka kunifanya nikatafute nyumba ndogo ya kuzaa nayo ili niweze kujiongezea familia?
Au mwanamke anapojifungua kwa oparesheni inatakiwa akae miaka mingapi ndio apate ujauzito mwingine!
Kwa kweli nashindwa kumuelewa huyu mwanamke!
Punguza Jazba, kaa naye chini na muulize yeye angependa kubeba mimba mtoto wenu akiwa na umri gani then hapo anaweza kukueleza na kukupa sababu za maamuzi yake. Huwezi kujua labda kuna tatizo la kiafya linalomfanya aone uzito kubeba mimba ...
Kwa kifupi, ni suala la kukaa na kujadiliana!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom