Mimi namshangaa huyu mke wangu! nimezaa naye mtoto mmoja ila alijifungua kwa njia ya upasuaji miaka miwili iliyopita. kwa sasa mtoto keshakuwa mkubwa maana ana umri wa miaka miwili na mimi nilitaka nimpe mimba nyingine ili azae halafu ndio tupange mipango mingine ya maisha.
Cha kushangaza sasa ni kuwa kila ikifika muda wa yeye kupata mimba hukwepa sana ikiwemo kutaka tutumie zana ili asipate mimba.
Nishamwambia tupate mtoto mwingine ili tupumzike kabisa ili mwili wake upate nguvu aruie hali yake ya usichana lakini hataki kunielewa ati anataka tuzae mtoto mwingne baada ya miaka mitano! huku si kutaka kunifanya nikatafute nyumba ndogo ya kuzaa nayo ili niweze kujiongezea familia?
Au mwanamke anapojifungua kwa oparesheni inatakiwa akae miaka mingapi ndio apate ujauzito mwingine!
Kwa kweli nashindwa kumuelewa huyu mwanamke!
Your such a selfish man. Unajifikiria wewe tu. Unafikiri kuzaa mchezo! Give her a break. Unafikiri miezi tisa mchezo! Kkichefuchefu, kuvimba miguu, mipresha hiyo hata mtu hujasahau unataka kumpa mimba halafu eti unasema nataka azae ili tupumzike kabisa? Wewe unabeba mimba wewe? Usijehesabie tupumzike sema mke wangu apumzike. Ukome kabisa kumshangaa mkeo give her time akiwa tayari pangeni kupata mtoto lakini biashara ya kusema naenda nyumba ndogo fika salama. Hivi tu ana mtoto unajidai ntatafuta nyumba ndogo je ingekuwa bado hajajaliwa ingekuwaje! U umenikera sana uache ubinafsi