Mke amfanyia ‘kitu mbaya’ staa wa soka

Mke amfanyia ‘kitu mbaya’ staa wa soka​



ByMtanzania Digital
November 1, 2021



PRETORIA, Afrika Kusini
MPACHIKAJI mabao wa zamani wa Orlando Pirates, Tendai Ndoro, amejikuta akipoteza mali zote alizochuma baada ya kukorofishana na mkewe aitwaye Thando Maseko.
Katika kilele cha penzi lao, Ndoro aliyewahi pia kung’ara akiwa na timu ya taifa ya Zimbabwe, aliandikisha jina la bibiye huyo kwenye mali zote, yakiwamo magari na nyumba.
Sasa, kilichotokea ni kwamba wawili hao wametibuana na alichokifanya bi. Thando ni kumfukuza mshikaji kwenye mjengo waliokuwa wakiishi, ikizingatiwa kuwa ndiye jina lake linalotumika kwenye umiliki.
Taarifa za Ndoro ‘kufulia’ zilianza kusambaa nchini Afrika Kusini hivi karibuni baada ya mwanasoka huyo kuonekana akiwa amepungua uzito, ambapo ilielezwa kuwa huenda anasumbuliwa na tatizo la akili.

Wananawake wengine mtihani mno mno.
 
haya matukio wa TZ wengi yashawakuta nchini Msumbiji, kuna masela kama wawili nipo nao mitaani dah wanasikitisha kwa kweli.


Madada wa Mozambique wakikuona ushatengeneza michongo na ramani imetulia wanakutengenezea misala mamwera wanakulamba. Na mapolisi wa Mozambique hawana simile na wageni, wale ni mambwa sijawahi kuona. Nchi ile haina sheria kabisa nyau wale.
 
Ni mjinga alistahili hilo pigo.

Unamwamini vipi mtu mmekutana ukubwani tu sio ndgu, ni wapenzi tu na wala hujui ka anakudanganya au ni mkweli.

Kwenye pesa simwamini yeyote najiamini mimi tuu. Kila siku mnaambiwa msimwamini mwanamke ila bado majuha hayaishi.
 
Anatia huruma jamaa alifanya kwa mapenz kumbe mwenzie alikuwa after money
 
Madada wa Mozambique wakikuona ushatengeneza michongo na ramani imetulia wanakutengenezea misala mamwera wanakulamba. Na mapolisi wa Mozambique hawana simile na wageni, wale ni mambwa sijawahi kuona. Nchi ile haina sheria kabisa nyau wale.

dah kuna jamaa tupo nae mitaani kama amepanguka kabisa, alifanyiwa kitu mbaya na mtoto wa kimozambique
 
Duuh yani Mali yangu niandike Jina la Mwanamke!!! Never labda kama ninazo za ziada.
 
Mi nadhani akitulia na akapata wakili mzuri hatapoteza haki, hata kama Mali Zina jina la mke itaonekana vilipatikana wakati wa ndoa, so watagawana pasu. Bora wagawane kuliko abaki mtupu
 
Mi nadhani akitulia na akapata wakili mzuri hatapoteza haki, hata kama Mali Zina jina la mke itaonekana vilipatikana wakati wa ndoa, so watagawana pasu. Bora wagawane kuliko abaki mtupu
Kweli kabisa,Sema itategemea sheria ktk nchi yao inasemaje kuhusu Ishu za kugawana Mali.
 
Hivi kumbe bado kuna wanaume maboya mpaka leo wanaandika vitu walivyonunua majina ya mke. Binafsi hata nikimnunulia pedi sitoandika jina la mke
 

Mke amfanyia ‘kitu mbaya’ staa wa soka​



ByMtanzania Digital
November 1, 2021



PRETORIA, Afrika Kusini
MPACHIKAJI mabao wa zamani wa Orlando Pirates, Tendai Ndoro, amejikuta akipoteza mali zote alizochuma baada ya kukorofishana na mkewe aitwaye Thando Maseko.

Katika kilele cha penzi lao, Ndoro aliyewahi pia kung’ara akiwa na timu ya taifa ya Zimbabwe, aliandikisha jina la bibiye huyo kwenye mali zote, yakiwamo magari na nyumba.

Sasa, kilichotokea ni kwamba wawili hao wametibuana na alichokifanya bi. Thando ni kumfukuza mshikaji kwenye mjengo waliokuwa wakiishi, ikizingatiwa kuwa ndiye jina lake linalotumika kwenye umiliki.

Taarifa za Ndoro ‘kufulia’ zilianza kusambaa nchini Afrika Kusini hivi karibuni baada ya mwanasoka huyo kuonekana akiwa amepungua uzito, ambapo ilielezwa kuwa huenda anasumbuliwa na tatizo la akili.
ni nyumba moja tu nimemhurumia huyu mama watoto wangu kwa kuandika majina yetu wawili, la kwangu na la kwake kama wamiliki kwenye hati. nayo ni matrimonial house (nyumba ya kuishi) vingine vyote vina majina yangu peke yake. vijana sitaki kuwashauri vibaya lakini jifunzeni kwenye makosa wanaume wenzetu wamefanya.
 
Back
Top Bottom