Mke afya OK, mume low sperm count - ushauri please

Washauri wengi hapa, ukiondoa wale walioshauri kuhusu vyakula, wamekushauri kuchukua hatua ya mbele sana kuliko ile unayopaswa kuchukua sasa ambayo ni rahisi na ipo ndani ya uwezo wako. Kama una low sperm count unachotakiwa kufanya ni kutokufanya tendo la ndoa mara kwa mara, ili sperm zijae ziwe nyingi ndo ufanye tendo la ndoa na ndo uweze kumrutubisha huyo mkeo. Kula vyakula vya mboga za majani, wanga (wali, ugali, mikate), matunda kwa wingi, EPUKA vyakula vya mafuta mengi (fat) pia fanya mazoezi mara kwa mara na kunywa maji ya kutosha kilasiku (angalau lita moja ya maji kwa siku - siyo chini ya hapo). Aliyekushauri kunywa maziwa lita moja/zaidi kakudanganya. Maziwa kikombe yanatosha. Yakizidi yatakujazia mafuta mwilini na kukuweka hatarini kiafya. Pia EPUKA vinywaji vya kulewesha vya aina yeyote ile. EPUKA pia vitu kama soda na kahawa. Ukiweza hata chai. Maana hivi vina kemikali inaitwa "caffeine" ambayo inapunguza nguvu ya mbegu zako. Kunywa maji tu Kaka. Kaa bila kufanya tendo la ndoa kwa muda wa kama mwezi mmmoja (wakati unaendelea kutekeleza ushauri huu) ndo ufanye. Atapata ujauzito bilashaka. Hata usihofu, low sperm count siyo tatizo kubwa hata kidogo. Ukiwa na low sperm count bado unaweza kumpa mwanamke ujauzito kwa njia ya asili (yaani tendo la ndoa).
Umesema vema sana ndugu yangu. Ushauri wako huu naufanyia kazi na nitarejea hapa.
 
naomba ushauri kama kuna mwenye experience au amewahi kusikia options ambazo ni productive. Mimi na mke wangu tuna miaka 4 sasa ya ndoa ya kikristo bila mtoto. Tumefanya vipimo vyote vya afya ya uzazi imeonekana mimi nina low sperm count na mke wangu hana tatizo lolote. Tendo la ndoa tunafanya kama kawaida bila shida yoyote na ndoa haina migogoro yoyote pamoja na hali hiyo lakini tunapenda sana kupata mtoto. Ushauri tafadhali kama kuna njia yoyote ya asili (natural) isiyoenda kinyume na imani ya kikristo.

pamoja na new tech.. Pia badili life style mkuu kuanzia diet, mazoezi, stress, na hakikisha unatafuta fertility specialists, hapo dar kuna dr. Anaitwa kapona yupo muhimbili au tumaini atakusaidia
 
Ingekuwa mwanamke ndio mwenye tatizo wala tusingekuona hapa. Sasa tuseme huko hospitali umeambiwa huo ugonjwa hauna dawa au ni nini? Kama hakuna dawa mwenzio atakuvumilia tu hivohivo, ni shida na raha. Na hizi mambo za hospitali umejitafutia shida bure, sa hizi ungekuwa na watoto zamani! Akili kumkichwa. Nakupa mbinu hii kaka niskize uzuri. Nenda chukua dawa yoyote mradi haina madhara umeze. Halafu baada ya mwezi mwambie mkeo ushapona. Utaona anapata ujauzito na maisha yataendelea vizuri. Upole muhimu.

you look like the feminist one maono yako tu yanaonesha hivyo..
 
dotnet
ushauri tafadhali kama kuna njia yoyote ya asili (natural) isiyoenda kinyume na imani ya Kikristo

Mkuu, dotnet pole kwa usumbufu. Sikujua kwamba codes nyingine zimebeba adverts za watu. Tumia maneno ya Billings Ovulation Method kwenye google na u"search".
 
[Umesema vema sana ndugu yangu. Ushauri wako huu naufanyia kazi na nitarejea hapa.]

Kila la heri Mkuu. Ila usiache kutumia nyama kabisa. Mara moja kwa wiki siyo mbaya. Nyama ina madini ya "Zinc" ambayo nayo ni muhimu kwa afya yako ya "uzazi".
 
pole sana kaka! but u were born to be a father,Mungu wetu ni mwaminifu muombe nae atakupa kama alivotuahidi!kaka pia nakushauri uende katika hospital moja ya natural therapy ipo opposite na hinduMandal posta wanatibu mambo ya uzazi na hawana gharana kubwa za matibabu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom