Mkasa Wa Kweli : Yamenikuta Salma Miee

Mkasa Wa Kweli : Yamenikuta Salma Miee

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,672
022f70d9d9ab6395b66afaab26d08b0a.jpg

MWANZO

Naitwa Ibrahim Amour. Ni mwenyeji wa Morogoro. Nilisoma morogoro hadi kidato cha sita. Nikafanikiwa kuingia chuo kikuu cha Mlimani jijini Dar es Salaam.
Nilipohitimu elimu ya chuo kikuu na kupata shahada yangu, nilifanikiwa kupata ajira mamlaka ya mapato TRA, nilifanya kazi kwa miezi michache tu nikahamishiwa Tanga.
Baada ya kuishi katika nyumba ya wageni kwa siku chache nilifanikiwa kupata nyumba ya kupangisha maeneo ya Usagara.
Wakati huo nilikuwa sijaoa bado na nilikuwa na mdogo wangu aliyemaliza kidato cha nne aliyekuwa amekaa nyumbani huko kwetu Morogoro. Nikamuita ili nikae naye pale nyumbani kwa sababu nilikuwa peke yangu.
Zacharia akaja Tanga baada ya kumtumia nauli. Nilikuwa pia na mpango wa kumtafutia kazi sehemu yeyote ambayo ningefanikiwa.
Kwa vile bado nilikuwa mgeni katika jiji hilo nikaona nimsubirishe kwanza ili niweze kuzoeana na wenyeji ambapo ingekuwa rahisi kumuombea kazi sehemu yoyote.
Nikiondoka asubuhi kwenda kazini ninamuacha Zacharia nyumbani. Kwa kawaida nikiondoka asubuhi hurudi jioni.
Mara kwa mara Zacharia alikuwa akiniuliza kuhusu ule mpango wa kumtafutia kazi. Na mimi nilimjibu asubiri kwanza.
Baada ya miaka miwili nikafanikiwa kununua gari. Sasa nikawa naenda kazini na kurudi na gari langu. Miezi michache baadaye nikanunua kiwanja jirani tu na pale nilipokuwa naishi.
Wakati naanza kujenga msingi tu, nikapata matatizo kazini. Mimi na maafisa wenzangu watatu tulikamatwa na polisi tukidaiwa kujihusisha na wizi wa mapato ya serikali.
Tulisimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi. Wakati uchunguzi unaendelea tulikuwa nje kwa dhamana. Baada ya uchunguzi huo kukamilika tulifikishwa mahakani.
Ilikuwa kesi iliyotuendesha sana. Iliunguruma kwa karibu miezi minane. Katika kipindi hicho nilikonda kwa hofu na wasiwasi wa kufungwa. Kwa bahati njema shahidi muhimu wa kesi ile ambaye angetoa ushahidi ambao ungeniweka mahali pabaya, alifariki dunia kwa maradhi ya sukari.
Hukumu ilipokuja kutolewa mwenzangu mmoja akaenda jela miaka saba. Mwingine alionekana hakuwa na hatia. Mimi nikaachiwa kutokana na kutokuwa na ushahidi wa kutosha.
Mwenzangu aliyeonekana hakuwa na hatia alirudishwa kazini. Mimi nikafukuzwa kazi kabisa.
Pia nilishukuru. Niliona bora kufukuzwa kazi kuliko kufungwa na ukitoka huko huna kazi.
Hata hivyo mpango wangu wa kuendeleza ujenzi wa nyumba yangu ambao nilikuwa nimeshauanza ukaishia hapo hapo.
Nilikuwa na akiba yangu benki nikaamua kuanzisha mradi wa kuchukua tenda za usambazaji vitu mbalimbali katika mashirika, taasisi na idara za serikali.
Nikafungua ofisi yangu jirani na maktaba. Baada ya kujitangaza katika maofisi mbalimbali nilifanikiwa kupata tenda ndogo ndogo lakini nikitegemea kuwa baadaye ningeweza kupata tenda kubwa kubwa.
Nilikuwa nikisaidiana na Zacharia na nilikuwa nimeajiri msichana mmoja aliyekuwa akibaki ofisini kwa ajili ya kazi ndogo ndogo kama vile kufungua ofisi asubuhi na kuifunga jioni, kupokea simu na kuhifadhi kumbukumbu zetu za kiofisi.
Siku moja nikashuhudia ajali karibu na ofisi yangu.
Msichana mmoja ambaye alikuwa akiendesha baskeli aligongwa na gari ndogo ambayo haikusimama.
Wakati tukio hilo linatokea mimi nilikuwa nikiondoka na gari langu ofisini kwangu. Nikalisimamisha gari karibu na mahali alipoanguka yule msichana na kuzirai.
Kitu kilichonishitua ni kwamba alikuwa akitokwa na damu nyingi iliyokuwa ikisambaa barabarani.
Baskeli yake ilikuwa imeanguka kando yake ikiwa imekunjwa kama iliyokanyagwa na treni.
Gari lililomgonga lilikimbia mara tu baada ya ajali kutokea.
Kutokana na kuona ile damu iliyokuwa ikitoka kwa wingi, nilizima gari nikashuka na kumfuata yule msichana. Sikuwaza hili wala lile, nilimzoa pale chini bila kujali damu iliyokuwa ikimtiririka ambayo ilikuwa ikiingia kwenye nguo zangu.
Nilimpakia kwenye siti ya nyuma ya gari langu, nikajipakia na kumuwahisha hospitali ya Bombo ambapo alipokelewa na kushughulikiwa.
Sikujua kama angepona kutokana na ile damu iliyokuwa ikimtoka kwa wingi, nikapwatwa na wasiwasi.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 02

ILIPOISHIA
Wakati nimekaa nje ya chumba cha daktari nikiwaza, daktari alitoka na kuuliza.
“Aliyemleta huyu majeruhi aliyegongwa na gari ni nani?”
Hapo hapo nilishituka nikajua kuwa msichana ameshakufa.
Nilikuwa nimekaa na watu wengine wanne waliokuwa na shida zao. Nikainuka na kumjibu yule daktari.
“Ni mimi”
“Majeruhi amepoteza damu nyingi na anahitaji kuwekewa damu ili kuokoa maisha yake. Na hapa tumeishiwa na damu” akaniambia.
“Sasa tutafanyaje daktari?”
“La kufanya ni kupatikana damu kutoka kwa mtu yeyote, kwani ndugu zake wako wapi?”
“Siwatambui. Kama yangu itafaa niko tayari kumsaidia”
“Haya twende tukakupime kama unaweza kumtolea”
SASA ENDELEA
Daktari huyo alinipeleka katika chumba cha maabara. Nilitolewa damu yangu kwa ajili ya kuchukuliwa kipimo.
Niliambiwa kwanza ingechunguzwa ili kuonekana kama ilikuwa salama na kama nina damu ya kutosha kumpatia mtu mwingine.
Nilisubirishwa kwa karibu saa nzima kabla ya kuambiwa kuwa damu yangu ilikuwa salama na nilikuwa na uwezo wa kumtolea yule msichana.
Nilifurahi sana nilipoambiwa hivyo kwani muda wote nilikuwa nikimsikitikia msichana huyo.
Kikubwa kilichokuwa kikinisikitisha ni kwamba sikutaka afe. Baada ya damu yangu kutolewa nilipewa kikombe cha chai ya maziwa ili kiniweke sawa.
Wakati nakunywa chai, damu niliyotoa ilipelekwa katika chumba alichokuwa
yule msichana. Baadaye kidogo polisi wa usalama barabarani wakafika.
Nilikuwa nimeshamaliza kunywa chai na polisi hao walikuwa wameshapewa maelezo na wafanyakazi wa hospitali.
Wakanitaka na mimi niwape maelezo, nikawaeleza jinsi ajali ilivyotokea na jinsi nilivyomchukua huyo msichana na kumleta hapo hospitali.
“Tumeambiwa kuwa alikuwa anahitaji kuwekewa damu na uliamua kumsaidia?” Polisi mmoja akaniuliza.
“Ndiyo nimemtolea damu”
“Sijui kama unamfahamu huyu msichana?”
Nikatikisa kichwa.
“Kwa kweli simfahamu”
“Je ile gari iliyomgonga uliiona?”
“Ndiyo niliiona”
“Unaweza kututajia aina yake na namba yake ya usajili”
“Ni Toyota ya rangi nyeupe. Namba yake ya usajili sikuiona yote. Niliona namba za mwanzo tu”
“Tutajie hizo hizo”
Nikawatajia.
“Umetusaidia. Kuna mtu aliona namba zinazofuatia. Mtu mwingine alikariri tarakiu zote. Sasa tutakuwa tumepata namba kamili. Ninaamini tutalikamata hili gari muda usio mrefu”
“Mkimpata huyo dereva ni vyema anyang’anywe leseni kabisa. Ni dereva katili sana”
“Tukimpata tutamfikisha mahakamani. Mahakama ndio yenye uamuzi”
“Sawa”’
Baada ya kuzungumza na polisi hao daktari alinifuata na kuniambia kuwa ninaweza kuondoka kwani majeruhi niliyempeleka anaendelea kuwekewa damu.
“Ameshazinduka?” nikamuuliza.
“Hajazinduka bado lakini tunatarajia kuwa atazinduka muda si mrefu. Tunaendelea kumfanyia uchunguzi kuona kama ameumia kwa ndani”
“Sawa. Nitakuja kumuangalia kesho asubbuhi”
“Vizuri”
Wakati natoka hapo hospitali jua lilikuwa limeshakuchwa. Nilimpigia simu Zacharia nikamuuliza.
“Uko wapi?”
“Niko ofisini?”
“Hamjafunga ofisi bado?”
“Ndio tunataka kufunga”
“Basi fungeni, mimi sitafika tena huko. Tutakutana nyumbani”
“Sawa kaka”
Nikajipakia kwenye gari na kurudi nyumbani.
Asubuhi ya siku ya pili yake nilipotoka nyumbani nilikwenda hospitali ya Bombo kumjulia hali yule msichana.
Nilifurahi kumkuta akizungumza na muuguzi aliyekuwa akimhudumia.
“Oh kaka umefika tena?” yule muuguzi aliniuliza akikumbuka kwamba ndiye mimi niliyemleta hospitali yule msichana jana yake.
“Ehe nimefika kumjulia hali mgonjwa wangu” nikamjibu huku nikitabasamu.
“Mgonjwa wako anaendelea vizuri, Jana tumemuwekea damu na jana hiyo hiyo alizinduka”
Wakati nikizungumza na yule muuguzi yule msichana alikuwa akinitazama kwa macho ya shauku na udadisi.
“Salma huyu ndiye yule kaka aliyekuleta hospitali” Muuguzi huyo akamwambia.
Msichana huyo akashituka.
“Ndiye huyu kaka? Nimefurahi kumuona”
Msichana akanitazama kwa macho ya bashasha na kuniammbia.
“Asante kaka, nnakushukuru sana kwa msaada wako. Mungu atakulipa”
“Ni watu wachache sana duniani wenye moyo kama wake, kuacha shughuli yake na kukushughulikia wewe mtu ambaye hakufahamu na zaidi ya hapo akutolee damu iliyoweza kukusaidia hadi leo unajisikia vyema” Yule muuguzi akamwambia.
“Ni moyo wa kibinaadamu kweli kweli. Kwa kweli namshukuru sana. Mimi sina cha kumlipa ila Mungu ndiye atakayemlipa”
“Asante mdogo wangu kwa shukurani zako. Nimekuja kukujulia hali nijue unaendeleaje kwa sababu jana niliondoka ukiwa bado hujitambui”
“Kwa kweli kaka naendelea vizuri, nashukuru Mungu”
“Mimi naitwa Ibrahim Amour, ni mkazi wa Usagara hapa Tanga, sijui wewe mwenzangu unaitwa nani?”
“Naitwa Salma Aboud”
“Unaishi wapi?”
“Ninaishi Chumbageni”
“Unaishi na wazazi?”
“Ninaishi na mama yangu, Baba yangu alishafariki”
“Kwa hiyo mama ako anayo taarifa kuwa umepata ajali?’
“Mama hayuko, amekwenda kijijini tangu juzi”
“Basi atakuwa hana habari”
“Atakuwa hajui”
“Alikwambia angerudi lini?”
“Atakuwa huko kwa wiki nzima”
“Si kitu, nitakuachia namba yangu ya simu, ukiwa na tatizo unaweza kunipigia”
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 03


ILIPOISHIA
Nilimuandikia namba yangu ya simu na kumuachia. Kwa vile yeye hakuwa na simu, sikuwa na haja ya kuomba namba yake.
Baada ya hapo nilitoa shilingi elfu hamsini nikampa.
“Hizi zitakusaidia kwa matumizi madogo madogo ukiwa hapa hospitalini” nikamwambia.
Msichana alipokea pesa hizo na kunishukuru.
“Asante kaka”
Yule muufuzi aliondoka na kutuacha.
“Hivi kaka ile baskeli niliyokuwa naendesha uliiona?”
“Baskeli yako itakuwa imechukuliwa na polisi. Ukitoka hapa unaweza kuifuata kituo cha polisi cha Mabawa”
“Asante kaka”
Baada ya hapo niliagana na yule msichana. Nilimuahidi kumtembelea tena siku itakayofuata.
Wakati natoka nje ya hospitali niliona polisi wa usalama barabarani wakisimamisha gari lao. Nikajua walikuwa wamemtembelea yule msichana.
Nikajipakia kwenye gari langu na kuondoka.
SASA ENDELEA
Zilipita siku tatu, sikufika kule hospitali kutokana na kubanwa na majukumu yangu. Siku ya nne yake nikafika kumjulia hali yule msichana.
Lakini nilikuta kitanda kikiwa na mgonjwa mwingine. Kulikuwa na muuguzi aliyekuwa akimpa dawa mgonjwa huyo.
Nikawasalimia wote wawili kisha nikamuuliza yule muuguzi kuhusu yule majeruhi wa ajali ya gari.
“Unamuulizia Salma?” Muuguzi huyo akaniuliza lakini kabla sijamjibu akaniambia.
“Salma alishapewa ruhusa tangu jana”
“Kumbe…!”
Nikaduwaa kidogo kisha nikamuaga muuguzi huyo na kuondoka.
“Kama amepata nafuu ndivyo nilivyokuwa ninamuombea” nikajiambia huku nikijipakia kwenye gari langu.
Nililiwasha moto na kuondoka.
Ikapita wiki nzima. Nilikuwa ninaendesha gari langu nikitokea gereza la Maweni ambako nilikwenda kuchukua hundi ya malipo yangu, simu yangu iliyokuwa kwenye mfuko wa shati langu ilipoita.
Nilitumia mkono wangu wa kushoto kuitoa na kutazama namba iliyokuwa inanipigia. Sikuweza kuitambua. Ilikuwa namba ngeni.
Nikajiuliza haraka haraka ni nani? Sikupata jibu. Nikabonyeza kiwambo cha kupokelea na kuiweka simu karibu na sikio.
“Hello!”
“Hello! Bila shaka nazungumza na Ibrahim Amour?” Sauti laini ya kike ikaniuliza kwenye simu.
Nikajikuta nazungusha akili yangu kujiuliza alikuwa nani.
“Ndiye mimi, nani mwenzangu?” nikamjibu.
“Naitwa Salma Aboud!”
Kusema kweli moyo wangu ulishituka.
Hapo hapo nikamkumbuka msichana aliyekuwa amegongwa na gari wiki moja iliyopita.
“Wewe ndiye yule msichana uliyepata ajali?” nikamuuliza.
“Ndiye mimi. Nilishapewa ruhusa hospitali, samahani kwa kuchelewa kukujulisha. Najua huenda ilikusababishia usumbufu kidogo…”
“Ni kweli, nilifika hospitali nikaambiwa kuwa uliondoka jana yake. Vipi hali yako?”
“Kwa sasa sijambo kidogo”
“Unaendelea vizuri?”
“Nashukuru Mungu, ninaendelea vizuri”
“Nakumbuka uliniambia unaishi Chumbageni, ndipo ulipo hivi sasa?”
“Ndiyo niko nyumbani Chumbageni”
“Ile baskeli yako uliipata?”
“Sijakwenda kituo cha polisi kuifuatilia”
“Natumaini itakuwa bado iko. Siku ukipata nafasi unaweza kwenda kuichukua”
“Sawa kaka. Asante. Kwa mara nyingine nakushukuru sana kwa msaada wako. Ukipata nafasi unaweza kunitembelea nyumbani, mama yangu atafurahi sana atakapokuona. Nilimueleza jinsi ulivyonisaidia”
“Vizuri. Nitatafuta siku ya kuja kukuona”
“Sawa. Asante sana kaka”
“Asante”
Msichana akakata simu.
Nikairudisha simu mfukoni..
“Salma bado ananikumbuka” nikajiambia kimoyomoyo wakati nikikata kona kuelekea benki.
Siku zikaendelea kupita.
Kulikuwa na siku nilikuwa nikiendesha gari langu mitaa ya Chumbageni. Kulikuwa na jamaa niliyekuwa nimemfuata. Sasa wakati narudi ofisini kwangu nikamkumbuka Salma ambaye aliniambia alikuwa anaishi Chumbage. Nikaliegesha gari langu pembeni mwa barabara kisha nikatoa simu yangu na kumpigia.
“Hello Salama!” nikasema mara tu simu ilipopokelewa.
“Kaka Ibrahim. Nimefurahi kuwa leo umenipigia”
“Niko maeneo ya Chumbageni, nataka nikujulie hali?”
“Oh! Uko upande upi?”
‘Niko hapa karibu na shule ya chekechea”
Salma akanielekeza nyumba yao ilipo. Haikuwa mbali sana na pale. Nikafika.
Nilishuka kwenye gari. Nilimkuta amesimama mlangoni akinisubiri.
“Oh karibu” alliniambia huku akitabasamu.
Nilikwenda kwenye mlango, Salma akanikaribisha ndani.
Nilipita ndani. Upande wa kushoto wa nyumba hiyo kulikuwa na sebule pana iliyokuwa imepambwa vizuri.
“Karibu ukae” Salma akaniambia. Tabasamu lilikuwa likiendelea kuchanua usoni kwake.
Nikakaa kwenye kochi mojawapo.
“Ngoja nimuite mama, anataka kukuona”
Salma aliingia ndani. Nikabaki nikiyazungusha macho yangu kwenye sebule hiyo.
Punde tu Salama alirudi akiwa amefuatana na mwanamke mmoja. Kwa mimi mwenyewe nisingeweza kuamini kama yule alikuwa ni mama yake kwani alionekana bado msichana. Na walionekana kama mtu na mdogo wake.
“Mama yule kaka aliyenisaidia siku ile kunipeleka hospitali na kunitolea damu ndiye huyu hapa” Salama alimwambia mama yake.
“Baba unajisikiaje hali yako?” Mama huyo akaniuliza kwa furaha.
“Sijambo mama. Shikamoo”
“Marahaba. Habari za siku”
“Ni nzuri, sijui nyinyi hapa”
“Sisi hatujambo. Tunashukuru Mungu”
“Kaka Ibrahim, huyu ndiye mama yangu” salma akaniambia huku akiketi.
“Nimefurahi kumuona”
“Leo umeamua kututembelea…” mwanamke huyo aliendelea kuniambia. Alikuwa bado amesimama na hakuonesha dalili yoyote kuwa angeketi.
Baada ya kuulizana naye hali akatuambia.
“Haya endeleeni kuzungumza, mimi niko huko uani nina kazi kidogo”
“Asante, hata hivyo sitakaa sana. Nimekuja mara moja tu kumjulia hali mgonjwa wangu kisha nitaondoka”
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 04


ILIPOISHIA
Mama huyo alicheka niliposema ‘mgonjwa wangu’
“Haya nawaacha kidogo”
Akaondoka.
“Nikupatie kinywaji gani kaka?” SALMA akaniuliza.
“Hapana, sihitaji kinywaji chochote”
“Kwanini, tunayo juisi ya parachichi”
“Nitakuja kunywa siku nyingine, usijali”
Tukaendelea kuzungumza kwa karibu nusu saa. Wakati nataka kuondoka nilimuachia Salma shilingi elfu hamsini.
“Hizi zitakusaidia kununua vitu vidogo vidogo” nikamwambia.
“Asante kaka, nashukuru”
Salma alikwenda kumuita mama yake ili niagane naye. Mama huyo alipokuja akanishukuru kwa mara nyingine kwa msaada nilioutoa kwa mwanawe siku alipopata ajali.
SASA ENDELEA
Jina langu ni Salama Aboud, nilikuwa mtoto wa tatu wa mzee Aboud ambaye alifariki dunia wakati mimi nikiwa darasa la saba.
Katika kipindi chote hicho nilikuwa nikiishi na mama yangu ambaye alikuwa akinipenda na kunidekeza sana.
Kutokana na utoro wangu wa shule nilishindwa kuendelea na masomo ya sekondari. Niliacha masomo nikiwa kidato cha tatu. Vile mama yangu alikuwa anashindwa kunikemea na kwa vile hakukuwa na mtu mwingine wa kunisema kitu, basi nilifanya vile nilivyotaka mimi.
Kaka zangu walionitangulia mmoja alikuwa amefariki, wawili walikuwa wakikaa Dodoma kwa baba mdogo.
Siku ile niliyopata ajali walikuja Tanga kunijulia hali kisha waliondoka kurudi Dodoma.
Sikujua ni kitu gani kilichofanya nimzowee sana Ibrahim. Pengine ni kutoka na wema alionifanyia siku ile nilipopata ajali. Kwanza nilimchukulia kama msamaria mwema lakini mazoea yetu yalipozidi nilianza kumpenda na nikawa na hisia ya kuishi na mtu kama Ibrahim.
Nilivutiwa sna na staili yake ya maisha na tabia yake. Lakini Ibrahim hakuwa akionesha kutambua mawazo yangu. Jambo hilo lilikuwa likinikera sana. Kusema kweli nilikuwa ninatamani tuwe wapenzi.
Usishangae kwamba nilikuwa nikiwaringia sana wanaume. Walitokea wanaume wawili waliotaka kunioa nikawakataa bila sababu yoyote.
Mama yangu kwa kufuatisha mawazo yangu, naye aliwatolea nje.
Mara kwa mara mama alikuwa akiniuliza.
“Utaolewa lini mwanangu, wenzako wote wameolewa?”
“Hao walioolewa waache waolewe, mimi niache tu”
“Sasa utakaa hivi hivi mpaka lini?”
“Kwani kuna mume aliyekwambia ananitaka nikamkataa?”
“Si walikuja vijana wawili ukawakataa mwanangu”
“Bado unawakumbuka tu”
“Nawakumbuka kwa sababu sioni dalili ya kutokea mume mwingine, naona kama umejitia nuksi”
“Muda wangu wa kuolewa ukifika nitaolewa tu mama”
Haukupita muda mrefu ndipo alipojitokeza Ibrahim.
Ibrahim nilimuonesha dalili zote za mapenzi kwani haikuwa rahisi kwangu mimi mwanamke kumueleza wazi kuwa nimempenda.
Siku moja nikaukata mzizi wa fitina. Nilimtumia meseji nikamwambia.
“Natamani ningekuwa mke wako Ibrahim”
Akarudisha jibu na kuniuliza.
“Kwanini?”
Nikamtumia meseji nyingine ya kumwambia.
“Nimependa tabia zako”
Akanijibu tena kwa kuniambia.
“Kama ungependa tuoane subiri nijiandae”
Kwa sababu nilikuwa nampenda, jibu lake hilo likanifurahisha.
Siku ya pili yake tulikutana katika hoteli moja tukazunguza sana kuhusu mapenzi.
Akaniambia yeye ni muangalifu sana katika kutafuta mchumba lakini katika siku chache tulizokuwa pamoja amegundua kuwa ninafaa kuwa mchumba wake. Ibrahim hakujua alikuwa amenifurahishaje kutokana na kauli yake hiyo.
Dhamiri yetu ikatimia. Baada ya kuzungumzia uchumba kwa wiki kadhaa, hatimaye Ibrahim akaleta barua ya uchumba kwa mama yangu.
Mama yangu aliipokea kwa mikono miwili kwa sababu nilishamueleza jinsi nilivyokuwa ninampenda Ibrahim.
Mama alimfahamisha baba mdogo aliyekuwa Dodoma kuwa kumeletwa barua ya uchumba ya Salma.
Baba mdogo akanipigia simu kuniuliza kama nimempenda huyo mchumba.
“Nimempenda ndio maana nilimuelekeza aje kwetu” nikamjibu.
“Nimesikia kuwa ndiye yule aliyekusaidia ulipopata ajali?”
“Ndiye yeye”
“Imekuwa heri. Huyo ni mchumba mwema. Mimi pia nimemkubali”
Baada ya baba mdogo kuzungumza na mimi alimpigia mama akamwambia kuwa na yeye amekubaliana na huo uchumba.
Mbali ya kumjulisha baba mdogo, mama pia aliwajulisha wajomba, yaani ndugu zake. Wote wakaukubali uchumba huo na jibu likapelekwa kwa Ibrahim kuwa uchumba wake umekuwa makubuli, yaani umekubaliwa.
Sasa ikawa ni mipango ya harusi. Mipango ya harusi yetu ilichukua karibu miezi mitatu. Nataka niseme ukweli kuwa tangu nijuane na Ibrahim mpaka tunakuwa wachumba sikuwahi kutembea naye hata siku moja.
Mimi sikutaka jambo hilo kwa sababu baadhi ya wanaume ukishatemmbea nao hubadili mawazo na kutafuta wachumba wengine.
Ibrahim pia hakuonesha kuwa na uchu wa wasichana. Alipoona dhamiri yangu ilikuwa ni kuoana, hakuwahi hata siku moja kunishawishi tufanye kitu.
Kwa hilo peke yake nilimsifu na kuona alikuwa mwanaume madhubuti aliyeweza kuuzuia moyo wake. Ni wanaume wachache sana wenye tabia kama ya Ibrahim.
Ndoa yetu ilifungwa siku ya ijumaaa saa saba na nusu. Ilifungwa katika msikiti wa Chumbageni baada ya mshuko wa swala ya ijumaa.
Mimi nilikuwa niko nyumbani nikimsubiri mume atoke msikitini. Tangu asubuhi nilikuwa saluni nikipambwa na kuchorwa piko. Nilirudishshwa nyumbani saa sita.
Nilipelekwa saluni nikitokea kwa kungwi ambako nilikaa kwa wiki maja nikifundwa jinsi ya kuishi na mume.
Nakumbuka somo moja muhimu nililolipata kwa kungwi ni kuwa nisimnyime mume wangu anapotaka penzi hata kama niko jikoni napika.
“Acha kazi zako ukamridhishe mumeo” kungwi wangu aliniambia.
Ibrahim aliporudi nyumbani kutoka msikitini alifuatana na watu watatu mmojawapo akiwa sheikh aliyetuozesha.
Ibahim alinipa mkono mke wake. Na hii ni kawaida. Mume akishakuoa akiingia chumbani hukupa mkono.
Sheikh akatuombea dua na kututaka tuishi maisha marefu, tupate watoto wema, tuishi kwa upendo na kuaminiana. Lakini akaongeza sentesi moja mabayo sikuipenda. Alisema.
“Mvumiliane, msameheane, muaminiane lakini kama itatokea mnaachana muachane kwa wema”
Kichwa changu kilikuwa kimefunikwa kwa mtandio unaoonya. Sheikh aliposema hivyo, niliinua uso wangu niliokuwa nimeuinamisha chini. Nikamtupia jicho Ibrahim huku yale maneno, “Kama itatokea mnaachana muachane kwa wema…” yakipita akilini mwangu.
Wakati namtupia jicho Ibrahim nilikuwa kama namuuliza. “Hivi tutakuja kuachana mimi na wewe?”
Moyoni mwangu sikutarajia kwamba hilo lingeweza kutokea kwa vile sheikh alishatuambia tuvumiliane, tusameheane na tuaminiane.
Niliamini kwa falsafa ya kuvumiliana, kusameheana na kuaminiana, suala la kuachana lingekuwa mbali sana na ndoa yetu.
 
SEHEMU YA 05


ILIPOISHIA
Baada ya sheikh kutuombea dua hiyo, sherehe za ndoa yetu zikaendelea hadi usiku wa manane. Lakini mimi na Ibrahim tuliondoka mapema kwenda nyumbani kwake Usagara.
Usiku wa siku ile ndio kwa mara ya kwanza, mimi nilimjua Ibrahim na yeye alinijua mimi kwa maana kwamba ndio tulikutana kwenye sita kwa sita.
Baada ya kitendo hicho cha siku ya kwanza, ndio nilimpenda zaidi Ibrahim na naamini hata yeye alinipenda zaidi.
Ibrahim na mimi tukawa tumefungua ukurasa mpya wa maisha.
Maisha ya siku za mwanzo mwanzo yalikuwa ya upendo sana. Ibrahim akitoka katika shughuli zake hurudi nyumbani. Kadhalika na mimi sikuwa mtu wa kutoka toka wala wa kwenda kwa majirani.
Na hilo ni funzo nililolipata kwa kungwi wangu kuwa nikiwa kwa mume wangu niachane na safari zisizokuwa na msingi na pia niepukane na mashoga na majirani wasio wazuri.
SASA ENDELEA
Jirani yangu mmoja wa nyumba tuliyopakana nayo upande wa kushoto alihama nyumba, akaja mpangaji mwingine, mtu mmoja na mke wake.
Huyo mwanaume alikuwa mtu mzima kidogo, alifikia umri wa miaka hamsini wakati mke wake alikuwa bado msichana ila alikuwa amenizidi mimi kidogo kwa umri.
Baada ya kuishi na majirani hao kwa mwezi mmoja nikajikuta nimependa staili yao ya maisha. Kila mmoja wao alikuwa na gari. Mume mtu alikuwa na gari lake na mke naye alikuwa na gari lake.
Aliyekuwa akifanya kazi ni mume, mke alikuwa yuko nyumbani tu wakati wote. Lile gari alikuwa akilitumia kwenda sokoni au kwenda safari zake nyingine.
Mwanaume huyo anapoondoka nyumbani asubuhi hurudi jioni na anaporudi huwa hatoki tena. Vicheko vyao wakati wa usiku vilikuwa vikisikika hadi ndani kwetu.
Taratibu nilijikuta nikizooeana na mke wa huyo jamaa.
Kulikuwa na siku kulikuwa na tatizo la kukatika maji. Msichana huyo akaja nyumbani kwangu asubuhi na kubisha mlango.
Niliposikia mlango unabishwa nilikwenda kuufungua nikamkuta amesimama mbele ya mlango.
“Mmeamkaje jamani?” akanisalimia.
“Hatujambo, sijui wewe” nikamjibu.
“Samahani jirani yangu, nataka kukuuliza huku kwenu maji yanotoka?”
“Hayatoki” nikamjibu na kuongeza.
“Yalikatika tangu jana usiku”
“Basi mwenzako sina habari kuwa maji yamekatika, nafungua bomba nakuta tupu. Mume wangu anataka ajimwagie aende kazini. Hukuweka akiba kidogo ukanigaia”
“Nina tenki la juu, huwa naweka akiba ya maji. Maji yanapokatika sipati taabu”
“Mh mwenzangu umenizindua. Nitamwambia mume wangu naye anunue”
“Sasa lete ndoo uje umchotee”
“Asante jirani, ngoja nikachukue ndoo”
Msichana huyo aliondoka. Nilifunga mlango nikaenda kufungua mlango wa uani na kumsubiri.
Alipotokea nikamuita.
“Njoo kwenye mlango huu”
Msichana huyo akaingia katika mlango huo wa uani. Nilikwenda naye kwenye bomba nikamwambia aweke ndoo yake. Nikamfungulia maji.
Ndoo yake ilipojaa akaniambia.
“Unanipa ndoo hii moja au nije unipe ya pili, kwa maana hii ataoga mume wangu, bado mimi sasa…”
“Na ya kupikia je…?” nikamuuliza.
“Hapo sasa!”
Tukacheka.
“Nakwambia hawa watu wa idara ya maji nao watatupa shida!” akaniambia.
“Njoo uchote shoga yangu usijali, leo kwangu kesho kwako”
“Ngoja nipeleke hii kwanza…”
Msichana huyo alibeba ile ndoo akatoka. Niliingia ndani nikaendelea na shughuli zangu. Punde tu nikamsikia akiniita.
“Jirani nimerudi!”
“Chota tu, nina kazi kidogo” nikamwambia.
“Asante jirani”
Niliendelea na kazi zangu. Baadaye nikamsikia tena.
“Nachota hii ya tatu”
“Chota tu” nikamwambia.
Alipomaliza kuchota aliniambia.
“Haya jirani asante, nakwenza zangu”
“Haya jirani”
Kutoka siku ile ndipo nilipoanza urafiki na jirani yangu huyo. Alikuwa akija nyumbani kwangu kuzungumza na wakati mwingine mimi nilikuwa nakwenda nyumbani kwake. Nikalifahamu jina lake. Alikuwa anaitwa Rita..
Rita akawa rafiki yangu mkubwa, tukafikia hadi kuazimana nguo na vitu vingine na pia tulipeana siri zetu za ndani.
Kutokana na urafiki wetu huo niliweza kugundua kuwa maisha aliyokuwa akiishi Rita na mume wake hayakuwa kama maisha niliyokuwa ninaishi mimi na mume wangu.
Wenzetu walikuwa wanaishi maisha ya hali ya juu na ya kifahari. Rita alikuwa akiniambia kila kitu alichohitaji, mume wake alikuwa akimtimizia. Alihitaji gari akamnunulia. Na wakati ule tunaanza kufahamiana alikuwa akimjengea nyumba maeneo ya Kange.
“Mume wangu si mgumu, ananisililiza na kunijali” Rita aliniambia na kuongeza.
“Kila ninachohitaji ananipatia”
“Basi una raha shoga yangu. Umepata mume mzuri. Wangu mimi ukitaka kitu mpaka kwa mbinde”
“Lakini hata huyu wangu aliponioa alikuwa hivyohivyo, nilifanya kumtengeneza”
Nikashituka.
“Ulimtengenezaje shoga?”
“Nilimuendea kwa mganga nikamlisha madawa mpaka yakamkolea”
“Wacha shoga!. Kumbe kuna madawa yanayoweza kubadili tabia ya mwanaume?”
“Yapo. Si unamuona mume wangu alivyo. Sasa nakwambia hakuwa hivi! Kuninunulia nguo ilikuwa ni mpaka tugombane”
“Wangu mimi hatugombani, ni mgumu tu. Kila siku yeye hana pesa lakini biashara anafanya. Sijui pesa zake zinakwenda wapi!”
“Basi ana mwanamke nje, ndiye anayemla. Mwenzangu wala chuya, mchele waliwa na mwenzio!”
Rita aliponiambia hivyo alinicheka na mimi nikajidai kucheka lakini moyo wangu ulipata fadhaa sana nilipohisi kuwa inaweza kuwa ni kweli mume wangu akawa na msichana wa nje anayekula pesa zake.
Siku ile niliwaza sana yale maneno aliyoniambia shoga yangu.
Mume wangu aliporudi jioni nilijaribu kumwambia.
“Mume wangu huninunulii hata pikipiki na mimi”
“Unataka pikipiki ya nini mke wangu?”
“Pikipiki ya nini? Watu wananunuliwa magari, wewe unasema pikipiki ya nini?”
“Kama ni gari si hili tunalo”
“Hilo ni la kwako. Mimi nataka pikipiki”
“Tuombe Mungu, kazi zangu zikienda vizuri nitakununulia”
“Utaninunulia lini?”
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 06

ILIPOISHIA
“Wangu mimi hatugombani, ni mgumu tu. Kila siku yeye hana pesa lakini biashara anafanya. Sijui pesa zake zinakwenda wapi!”
“Basi ana mwanamke nje, ndiye anayemla. Mwenzangu wala chuya, mchele waliwa na mwenzio!”
Rita aliponiambia hivyo alinicheka na mimi nikajidai kucheka lakini moyo wangu ulipata fadhaa sana nilipohisi kuwa inaweza kuwa ni kweli mume wangu akawa na msichana wa nje anayekula pesa zake.
Siku ile niliwaza sana yale maneno aliyoniambia shoga yangu.
Mume wangu aliporudi jioni nilijaribu kumwambia.
“Mume wangu huninunulii hata pikipiki na mimi”
“Unataka pikipiki ya nini mke wangu?”
“Pikipiki ya nini? Watu wananunuliwa magari, wewe unasema pikipiki ya nini?”
“Kama ni gari si hili tunalo”
“Hilo ni la kwako. Mimi nataka pikipiki”
“Tuombe Mungu, kazi zangu zikienda vizuri nitakununulia”
“Utaninunulia lini?”
SASA ENDELEA
“Si nimekwambia ufanye subira. Mambo yakiwa mazuri utapata pikipiki, hata gari”
“Yako ni hayo tu kila siku. Wanaume wengine hawapendi hata kuwapendezesha wake zao!”
“Salma usiige mambo ya watu. Kwa vile umemuona jirani yako ana gari na wewe unataka ununuliwe gari. Wewe unajua mume wake anafanya kazi gani?”
“Wala sio hivyo. Mimi nina akili zangu na naangalia maisha yangu. Siigi mtu mimi. Kama ninataka pikipiki ninaitaka kwa shida yangu. Tatizo ni kuwa kila ninachokwambia mume wangu lazima ukipinge”
Ibrahim akajidai kucheka.
“Si kweli. Mbona vitu vingi nakununulia. Nguo nakununulia pamoja na kukutimizia mahitaji mengine. Sema wewe sasa unataka makubwa”
“Haya basi nayaishe. Naona labda kuna mwenzangu wa pembeni maana siku hizi umebadilika sana”
Siku ile nilijaribu tu kumpima mume wangu ili nione atanijibu nini. Lakini jibu lake lilikuwa ni la kukatisha tamaa. Sikamini kabisa kuwa kwa kipato cha mume wangu angeshindwa kuninunulia pikipiki.
Pia sikuamini kuwa mwaname huyo angeshindwa kunitimizia mahitaji yangu mengine ninayotaka kama anavyofanyiwa shoga yangu na mume wake.
Pegine ulikuwa ni ugumu au roho mbaya inayotokana na mila zilizopitwa na wakati zinazowadharaulisha wanawake kwa wanaume.
Baada ya siku ile sikumuuliza kitu tena Ibrahim lakini ndani ya moyo wangu nilishaamua kama tabia ya Ibrahim itaendelea kuwa ile nisingeweza kupata maendeleo kama wanawake wenzangu.
Nilikaa kama siku tatu hivi nikiwaza, siku ya nne yake nikaenda kwa yule rafiki yangu. Nilimkuta amekaa sebukeni akitizama filamu kwenye televisheni yake.
“Vipi shoga?” akaniuliza.
“Ah mambo ya mume wangu yananichokesha!” nikamwambia huku nikiketi kwenye kochi.
Shoga yangu Rita akanicheka.
“Yamekuchokesha vipi shoga?”
“Ugumu shoga! Mume wangu ni mgumu sana. Juzi nilijaribu tu kumuomba aninunulie pikipiki, eti anajidai kuniuliza pikipiki ya nini…gari si hili tunalo”
“Labda hana pesa”
“Sio kutokuwa na pesa, sema ni mgumu. Pesa anazo lakini ana dharau, hataki maendeleo yangu. Nimeshamuona yule si mume ni gume gume”
Shoga yangu akacheka tena lakini mimi sikucheka nilijifanya nimekasirika.
“Kweli nakwambia shoga…yule si mume ni gume gume”
“Siku ile nilikwambia mwendee kwa songoma ukaleta gozi gozi. Si unamuona huyu mume wangu nimemnyoosha, haoni wala hasikii, nikikohoa tu ananiuliza wataka nini mke wangu?”
“Na hilo la songoma ndilo lililonileta, nataka unipeleke na mimi nikamtengeneze, awe kama mume wako. Nikimuona amekaa sawa, namwambia anijengeee nyumba”
Mimi na shoga yangu tukacheka pamoja.
“Na huyo songoma mwenyewe akikufanyia dawa zake utakuja kuniambia. Lazima mumeo atakujengea nyumba” Rita akaniambia na kuzidi kunipa moyo.
“Sasa utanipeleka lini shoga?”
“Siku yoyote utakayotaka, mimi niko tayari”
“Nataka unipeleke kwa huyo huyo aliyekufanyia wewe”
“Na ndiko huko huko nitakakokupeleka”
“Na itachukua siku ngapi hadi matokeo yaonekane?”
“Si siku nyingi. utamuona akibadilika kidogo kidogo”
Nilinyamaza kidogo kufikiri kisha nikamuuliza.
“Tunaweza kwenda kesho?”
“Tunaweza lakini iwe asubuhi, mpaka saa sita twe tumerudi”
“Na mimi pia muda wangu mzuri ni wa asubuhi, yule bwana akienda kazini. Najua akiondoka harudi mpaka jioni”
“Harudi mchana kuja kula?”
“Zamani ndio alikuwa anarudi kula lakini siku hizi akiondoka ndio mpaka jioni. Sijui anakula kwa huyo mke mwenzangu!”
“Yote utayajua huko huko kwa huyo mganga”
“Kama ana mwanamke atanieleza?”
“Atakueleza yote”
“Nataka nijue, uwezekano huo wa kwa na mwanamke upo”
“Sasa basi wewe jiandae, nikikupigia simu kesho asubuhi unakuja, tunakwenda zetu”
“Ni mbali sana”
“Mganga mwenyewe yuko Kisosora”
“Si tutakwenda na gari yako”
“Tutakwenda na gari yangu, usijali. Hapo Kisosora hata lita moja ya petroli haimaliziki”
“Tutatia lita moja”
“Mbona mume wangu ananitilia ya kutosha. Ananiwekea mafuta ya wiki nzima”
“Acha mambo yaende vizuri, na mimi keshokutwa nitakuwa na gari langu. Mwanaume pesa anazo lakini ni mgumu sana. Hataki hata nijue katika akaunti yake ya benki ana shilingi ngapi”
“Tena nakwambia ukimuweka sawa, hata jina la akaunti yake ya benki anaweka la kwako?”
“Acha shoga! Kwani wewe mume wako ameweka jina lako kwenye akaunti yake?”
“Mimi amenifungulia akaunti yangu kabisa, ananiwekea pesa kila mwezi”
“Na mimi itakuwa hivyo hivyo. Nitamwambia anifungulie akanti benki”
Siku ile nilirudi nyumbani kwangu nikiwa na furaha na ndoto za kupata tajiri. Kama mume wangu atanijengea nyumba, ataninunulia gari, atanifungulia akaunti benki, nitajiona kama nimeshakuwa tajiri.
Mume wangu aliporudi nyumbani jioni nilimchangamkia sana kuliko kawaida yangu kwa vile nilishajua mahali ambapo nitakwenda kumnyoosha.
Kwa vile ingekuwa ni mara yangu ya kwanza kwenda kwa waganga, siku ile sikupata usingizi kwa mawazo.
Mawazo yangu yalikwenda mbali nikawa nawaza wakati mume wangu akiwa bwege langu akinitii kwa kila kitu.
Nilijiambia wakati huo maisha yangu yatakuwa mazuri sana. Fedha za mume wangu nitakuwa nakaa nazo mimi.
Asubuhi kulipokucha nilianza kufanya usafi wa nyumbani kwangu. Sikushughulika kubandika chai mapema kwa sababu mume wangu alikuwa akiondoka asubuhi bila kunywa chai. Ananywea huko huko, yeye na mdogo wake.
Muda wao wa kutoka ulipowadia Ibrahim alinifuata uani akaniaga.
“Nimekuachia pesa za sokoni kitandani” akaniambia.
“Hizo ni pesa au visenti. Pesa utakuja kuniachia nitakapokutengeneza” nikamjibu kimoyomoyo.
Alipoondoka na mdogo wake nikaenda bafuni kuoga. Nilipomaliza nilivaa. Nikaenda kuketi sebuleni kwangu kusubiri Rita anipigie simu.
Nilipoona kimya na muda unakwenda nikampigia mimi.
“Shoga habari ya asubuhi?” nikamuuliza alipokea simu.
“Nzuri shoga, mume wangu ndio ameondoka sasa hivi. Nilikuwa nataka kukupigia kukwambia jitayarishe”
“Nimeshajitayarisha shoga”
“Basi njoo, mimi najiandaa”
Nikarudi chumbani kwangu kuchukua baibui langu nikalivaa na kupachika mkoba wangu begani, nikatoka.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 07


Y ILIPOISHIA
Alipoondoka na mdogo wake nikaenda bafuni kuoga. Nilipomaliza nilivaa. Nikaenda kuketi sebuleni kwangu kusubiri Rita anipigie simu.
Nilipoona kimya na muda unakwenda nikampigia mimi.
“Shoga habari ya asubuhi?” nikamuuliza alipopokea sim.
“Nzuri shoga, mume wangu ndio ameondoka sasa hivi. Nilikuwa nataka kukupigia kukwambia jitayarishe”
“Nimeshajitayarisha shoga”
“Basi njoo, mimi najiandaa”
Nikarudi chumbani kwangu kuchukua baibui langu nikalivaa na kupachika mkoba wangu begani, nikatoka.
SASA ENDELEA
Nilifunga mlango wangu wa mbele kwa funguo nikaenda nyumbani kwa jirani yangu.
Aliniacha sebuleni kwa karibu nusu saa kisha naye akatoka na kuniambia.
“Twenzetu”
Tulikwenda nyuma ya nyumba yake akafungua geti na kulitoa gari.
“Wewe jipakie kabisa, mimi nafunga geti” akaniambia na kurudi kwenye geti.
Aliingia ndani akalifunga geti hilo kisha akazunguka kwa mlango wa mbele.
Alifunga mlango na kuja kwenye gari. Wakati huo nilikuwa nimeshajipakia nikiwa kando ya siti ya dereva.
Akafungua mlango na kujipakia.
“Sasa twenzetu” akaniambia huku akiliwasha gari.
Alilirudisha gari kinyume nyume hadi barabarani. Akaligeuza na tukaanza safari yetu.
“Kinachonikera kwa yule mganga ni foleni ya watu, yaani ukifika unakuta msururu wa watu wanaomsubiri” Shoga yangu aliniambia wakati gari likiwa katika mwendo.
“Yeye mwenyewe anakuwa wapi” nikamuuliza.
“Anakuwepo ila wale watu wanafika kabla mwenyewe hajaamka. Wanamsubiri hapo nje mpaka aamke, aoge, anywe chai, unakuta foleni inakuwa ndefu”
“Sasa tutafanyaje shoga, tutawahi kurudi mapema kweli?”
“Tujaribu kubahatisha, tunaweza tusikute foleni ndefu. Kuna siku niliwahi kuja sikukuta mtu yeyote lakini kuna siku nilikuta foleni iliyonikatisha tamaa”
“Ukafanyaje?”
“Ilinibidi nisubiri hivyi hivyo. Mpaka nashughulikiwa ilikuwa imeshafika saa sita’mchana. Lakini nashukuru mambo yangu yalikwenda vizuri”
“Kama tutakuta foleni ndefu utaniacha niendelee kusubiri, hata kama nitaondoka jioni si kitu”
Dakika chache baadaye tukawa tumefika katika eneo hilo la Kisosora. Nyumba ya mganga huyo ilikuwa kibanda kidogo kilichojengwa kwa miti na udongo. Mbele ya kibanda hicho kulikuwa na nyumba kubwa ya matofali iliyokuwa haijakalmilika.
Tuliacha gari mbele ya ile nyumba tukaingia uani. Tulikuta watu ambao hawakuzidi kumi waliokuwa wameketi kwenye baraza ya kibanda hicho.
“Leo hakuna watu wengi, ni wale wachache tu” Rita akaniambia.
“Mbona hawajapanga foleni’ nikamuuliza.
“kila mtu anajijua ni wa ngapi kuingia. Sisi ndio tutakuwa watu wa mwisho. Labda waje wengine nyuma yetu”
Na sisi tukaenda kwnye ile baraza. Tuliwasalimia watu tuliowakuta kisha tukakaa.
Wakati tunakaa, mtu mmoja akatoka ndani ya kile kibanda. Alikuwa ni mteja aliyekwishahudumiwa. Mtu mwingine akaingia.
Baada ya nusu saa mtu huyo naye akatoka akaingia mwingine. Yule aliyeingia hakukaa sana, akatoka na kuingia mwingine.
Kitu kilichonipa moyo ni kuwa foleni ilikuwa ikienda kwa haraka.
Ilikuwa inakaribia kuwa saa nne na nusu, mimi na Rita tulipoingia.
Mganga mwenyewe alikuwa mzee aliyekuwa amejifunga kaniki. Chumba chake hakikuwa na mwanaga wa kutosha kutokana na kuwa na dirisha dogo. Tulipoingia tu nilianza kusikia joto.
“Karibuni” Mganga huyo akatuambia.
Alikuwa amekaa kwenye jamvi lililoenea chumba kizima.
Tukakaa kwenye jamvi mbele yake.
“Shikamoo” Rita akamwamkia na mimi nikamwammkia.
“Marahaba hamjambo”
“Hatujambo. Naona kama umenisahau” Rita akamwambia.
Mganga akamtazama vizuri.
“Kama nakukumbuka”
“Mimi ni Rita. Niliwahi kuja ukanishughulikia matatizo ya mume wangu”
“Ahaa! Nimekukumbuka. Uliniambia unaishi Usagara”
“Haswaa! Ni kweli umenikumbuka”
“Muda mrefu umepita sijakuona ndio maana nimekusahahu kidogo. Habari za siku?’
“Nzuri. Nimekuletea huyu mteja, ni rafiki yangu”
“Ana matatizo gani”
“Atakueleza”
Nikataka kumpima yule mganga kujua uwezo wake.
“Shida yangu nataka unitazamie ramli?” nikamwambia.
“Hapa ramli ndio nyumbani kwake, nipe mkono wako” Mganga akaniambia huku akininyooshea mkono wake.
Nikanyoosha mkono wangu na kumpa. Akaushika na kutazama kiganja changu.
“Huu mstari wa maisha unaonesha kuwa una tatizo na mume wako. Maisha yako hayaendi vizuri’ Mgaga akaniambia kisha akanitazama na kuniuliza.
“Kweli au uongo?”
“Ni kweli” nikamjibu.
“Enhe. Matatizo ya mume wako hayatofautiani sana na matatizo aliyokuwa nayo mume wa mwenzako. Kweli au uongo?”
“Ni kweli”
“Enhe. Mwanamme pesa anapata lakini hazionekani. Ugomvi hawishi nyumbani. Kweli au uongo”
“Ni kweli”
“Yaani ni sawa na kusema kuwa mapenzi hayapo nyumbani. Si kama ilivyokuwa wakati mnaanza sasa maisha. Kweli, uongo”
“Ni kweli”
Sasa mama una wasiwasi, unahisi kama mko wengi. Kweli, uongo’
“Ni kweli”
“Alama za kiganja chako zinanionesha kuwa mumeo ana nyumba ndogo iliyoharibu akili yake”
Hapo hapo nikamtazama Rita kwa mshangao.
“Unasikia maneno hayo. Mimi nilikwambia utaambiwa kila kitu” Rita akaniambia.
“Yaani mume wangu ana mwanamke wa nje?” nikamuuliza mganga huyo kwa taharuki.
“Wewe unadhani ni kitu gani kimeharibu tabia yake?’
“Huyo msichana ndio amemuharibu?”
“Yaani ndio anampenda kuliko wewe”
Nikatingisha kichwa changu kumkubalia.
“Asante kwa kunifahamisha, sasa na mimi nataka kumkomoa. Nataka amuache huyo mwanamke anipende mimi peke yangu, anijali na kunisikiliza, Kila ninachomwambia atii”
“Hata kama utataka akununulie gari atakununulia”
“Nifanyie hiyo kazi, utahitaji shilingi ngapi?’
“Kwa vile umeletwa na mteja wangu wa siku nyingi, nitakufanyia shilingi laki moja”
Nikaguna na kumtazama Rita.
Sikuwa nimechukua shilingi laki moja. Nilikuwa na shilingi elfu hamsini tu kwenye pochi yangu.
“Unajua shoga nilifanya ujinga nilipoondoka nyumbani, nilichukua shilingi elfu hamsini tu”
“Sasa mimi nitakutolee elfu hamsini, tukifika nyumbani unirudishie”
“Sawa shoga, nitakurudishia”
Rita akafungua pochi yake na kutoa shilingi elfu hamsini na mimi nikatoa kiasi kama hicho kutoka kwenye pochi yangu. Tukampa yule mganga.
“Anaitwa nani mumeo?” Mganga akaniuliza baada ya kupokea zile pesa.
“Anaitwa Ibrahim Amour”
ITAENDELEA kesho
 
SEHEMU YA 08

ILIPOISHIA
Nikatingisha kichwa changu kumkubalia.
“Asante kwa kunifahamisha, sasa na mimi nataka kumkomoa. Nataka amuache huyo mwanamke anipende mimi peke yangu, anijali na kunisikiliza, Kila ninachomwambia atii”
“Hata kama utataka akununulie gari atakununulia”
“Nifanyie hiyo kazi, utahitaji shilingi ngapi?’
“Kwa vile umeletwa na mteja wangu wa siku nyingi, nitakufanyia shilingi laki moja”
Nikaguna na kumtazama Rita.
Sikuwa nimechukua shilingi laki moja. Nilikuwa na shilingi elfu hamsini tu kwenye pochi yangu.
“Unajua shoga nilifanya ujinga nilipoondoka nyumbani, nilichukua shilingi elfu hamsini tu”
“Sasa mimi nitakutolea elfu hamsini, tukifika nyumbani unirudishie”
“Sawa shoga, nitakurudishia”
Rita akafungua pochi yake na kutoa shilingi elfu hamsini na mimi nikatoa kiasi kama hicho kutoka kwenye pochi yangu. Tukampa yule mganga.
“Anaitwa nani mumeo?” Mganga akaniuliza baada ya kupokea zile pesa.
“Anaitwa Ibrahim Amour”
SASA ENDELEA
Mganga aliuachia mkono wangu akachukua karatasi na kuiandika jina la Ibrahim.
“Na wewe unaitwa nani”
“Mimi naitwa Salma Aboud”
Mganga akaandika jina langu kwenye ile karatasi.
Pembeni mwake palikuwa na tunguri kadhaa. Alichukua tunguri mojawapo akakitia kile kiratasi kwenye mdomo wa ile tunguri kisha akaanza kuitikisa huku akitabana maneno kwa kiluga.
Kila alipotabana alikuwa akilitaja jina la Ibrahim na jina langu.
Baadaye alikitoa kile kiratasi ambacho kilikuwa kimeloa kwa dawa iliyokuwemo ndani ya ile tunguri. Akachukua chetezo kilichokuwa na makaa ya moto akakitia kile kikaratasi, kikaanza kuungua na kutoa moshi.
Akachukua tunguri nyingine akaitabania maneno huku akilitaja jina langu na la Ibrahim kisha akachukua karatasi na kumiminia unga fulani kutoka katika ile tunguri, akakiweka kile kikaratasi mbele yangu.
Akachukua tunguri nyingine nayo akaitabania kisha akamimina unga kama ule wa kwanza kwenye kikaratasi kingine.
Baada ya hapo alikifunga kikaratasi cha kwanza, kikawa kama kipakiti. Halafu alikifunga kikaratasi cha pili.
“Sasa sikiliza” Mganga akanimabia.
“Ndiyo nakusikiliza”
Alichukua kile kipakiti cha kwanza akanipa.
“Hiki utamuwekea kwenye maji ya kuoga kwa siku tatu”
“Sijakuelewa, nitamuwekea kwenye maji ya kuoga kivipi?”
“Yaani katika yale maji anayooga kwenye ndoo, tia hii dawa kidogo bila mwenyewe kukuona”
“Sasa sisi hatuogi kwenye ndoo, tunaoga moja kwa moja kwenye bomba”
“Mnatumia bomba la mvua?”
“Ndiyo”
“Sasa itakuwaje, hii dawa ni lazima aioge”
“Hakuna njia nyingine?”
Mganga akatikisa kichwa.
“Ingekuwepo ningekwambia”
“Si kitu, nipe”
“Utafanyaje?” Rita akaniuliza.
“Nitafunga maji kwenye mita kisha nitamtilia maji kwenye ndoo nimwambie maji yamekatika. Atayaoga tu”
“Lakini umeambiwa ni kwa siku tatu”
“Kwa siku tatu itakuwa vigumu, atagundua kuwa maji yanatoka”
Nikamtazama mganga na kumuuliza.
“Kwa siku moja haitatosha”
“Kama ni kwa siku moja itie mara tatu. Yaani chota kidogo tia, halafu chota mara ya pili tia halafu chota mara ya tatu tia. Itakuwa imemalizika yote.
“Ngoja nikwambie nilivyokuelewa. Nikishatia maji kwenye ndoo nichote kidogo hii dawa niitie kwenye maji halafu nichote tena nitie, halafu nichote tena mara ya tatu nitie. Au nimekosea”
“Ni sawa”
“Kwa hiyo nitaimaliza dawa yote?”
“Ndiyo utaimaliza yote”
“Haitaonekana kwenye maji?”
“Hapana, inayayuka na ni nyeupe tu. Hawezi kuiona”
“Sawa”
Mganga akachukua ile pakiti nyingine akanipa.
“Na hii utamuwekea kwenye chakula. Unatia kidogo kwenye mchuzi au wali au hata kwenye chai”
“Nitie wakati napika au wakati tunakula?”
“Wakati wowote, bora uitie tu”
“Sasa tatizo ni kwamba tunakula pamoja”
“Haina madhara hata kama wewe utakula hicho chakula au mtu mwingine atakula”
“Sawa. Nimtilie mara ngapi?”
“Mtilie mara moja kwa siku tatu”
“Wakati gani?”
“Wakati wowote asubuhi au jioni, unaweza kumtilia”
“Sawa”
“Baada ya siku tatu utaona matokeo yake, utakuja kuniambia”
“Atanipenda sana?”
“Na atakupa kila kitu unachokitaka”
“Nitakushukuru sana babu kwa maana yule mwanaume ananitesa sana”
“Mateso yote yatakwisha, utakuwa unamtesa wewe”
“Kila itakavyotokea nitakuja kukuambia”
“Sawa, sasa kazi yenu imekwisha mnaweza kwenda”
Tulipoondoka kwa yule mganga moyo wangu ulikuwa umepata matumaini sana na kufarijika hasa nilivyojua kwamba ninakwenda kumkomesha mume wangu.
“Sasa kazi kwako” Rita akaniambia wakati gari ikiwa kwenye mwendo.
“Nakwenda kumuwekea leo leo, singoji kesho”
“Ndiyo ianze leo”
“Nikifika nayafunga maji, atakapotaka kuoga namtilia maji kwenye ndoo”
Dakika chache baadaye tukafika nyumbani. Rita alilisimamisha gari mbele ya geti. Akashuka na kuniambia
nimsubiri.
Alikwenda kufungua mlango akaingia ndani kisha akaja kufungua geti.
Geti lilipokuwa wazi aliingia kwenye gari akaiingiza gari ndani. Tukashuka sote. Alikwenda kufunga geti. Alipomaliza tukaingia ndani ya nyumba yake.
“Shoga asante, acha niende nikatayarishe mambo” nikamuaga shoga yangu kabla ya kutoka kwenda kwangu.
Nilifungua mlango wa nyumba yanngu nikaingia ndani. Wakati nikiwa jikoni nikitafuta mahali pa kuficha vile vipakiti, nikasikia mlango ukigongwa. Nikaviacha vile vipakiti kwenye mkoba wangu, nikaenda kufungua mlango.
Nikashituka kuona alikuwa mgeni. Alikuwa mdogo wake Ibrahim aliyekuwa akikaa Dar. Alikuwa anaitwa Mashaka lakini mwenyewe alijiita meshack.
Alikuwa ni mdogo wake Ibrahim shangazi kwa mjomba.
“Oh shemeji, karibu sana” nikamkaribisha huku nikipokea begi alilokuwa amelipachika kwenye bega lake.
“Asante, habari ya hapa?”
“Nzuri, za safari”
Baada ya kulipokea begi niliingia nalo ndani.
“Nashukuru ni nzuri, sijui nyinyi hapa”
Meshack aliingia akafunga mlango.
Nikamkaribisha sebuleni lakini begi lake nilikwenda kuliweka kwenye chumba cha wageni.
Nilipotoka Meshack aliniuliza.
“Kaka yuko wapi?”
“Yuko kazini kwake, hapa anarudi jioni sana, si ana taarifa kuwa unakuja?”
“Anayo taarifa na leo asubuhi wakati najiandaa kuja huku nilimpigia simu kumjulisha kuwa ninakuja”
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 09

ILIPOISHIA
Geti lilipokuwa wazi aliingia kwenye gari akaiingiza gari ndani. Tukashuka sote. Alikwenda kufunga geti. Alipomaliza tukaingia ndani ya nyumba yake.
“Shoga asante, acha niende nikatayarishe mambo” nikamuaga shoga yangu kabla ya kutoka kwenda kwangu.
Nilifungua mlango wa nyumba nikaingia ndani. Wakati nikiwa jikoni nikitafuta mahali pa kuficha vile vipakiti, nikasikia mlango ukigongwa. Nikaviacha vile vipakiti kwenye mkoba wangu, nikaenda kufungua mlango.
Nikashituka kuona alikuwa mgeni. Alikuwa mdogo wake Ibrahim aliyekuwa akikaa Dar. Alikuwa anaitwa Mashaka lakini mwenyewe alijiita meshack.
Alikuwa ni mdogo wake Ibrahi shangazi kwa mjomba.
“Oh shemeji, karibu sana” nikamkaribisha huku nikipokea begi alilokuwa amelipachika kwenye bega lake.
“Asante, habari ya hapa?”
“Nzuri, za safari”
Baada ya kulipokea begi niliingia nalo ndani.
“Nashukuru ni nzuri, sijui nyinyi hapa”
Meshack aliingia akafunga mlango.
Nikamkaribisha sebuleni lakini begi lake nilikwenda kuliweka kwenye chumba cha wageni.
Nilipotoka Meshack aliniuliza.
“Kaka yuko wapi?”
“Yuko kazini kwake, hapa anarudi jioni sana, si ana taarifa kuwa unakuja?”
“Anayo taarifa na leo asubuhi wakati najiandaa kuja huku nilimpigia simu kumjulisha kuwa ninakuja”
SASA ENDELEA
“Ngoja nimpigie nimjulishe kuwa umeshafika”
Nikachukua simu yangu na kumpigia.
“Heloo!” Sauti ya Ibrahim ikasikika kwanye simu.
“Shemeji ameshafika” nikamwambia.
“Shemeji yupi?” akaniuliza.
“Shemeji Mashaka kutoka Dar”
“Oh alinipigia simu asubuhi kunijulisha kuwa anakuja lakini nilisahau kukuambia. Amefika sasa hivi”
“Ndiyo namkaribisha hapa”
“Mwambie ninakuja, tunafunga ofisi”
“Sawa”
Nikakata simu kisha nikamwambia shemeji.
“Anakuja”
Kutokana na ule muda aliofika shemeji nilikisia kuwa hakuwa amekula chakula cha mchana, nikaona angalau nikamtayarishie chai ya maziwa imchangamshe hadi usiku.
“Shemeji naenda jikoni” nikamuaga na kuondoka kwenda jikoni kumtayarishia chai.
Chai ilikuwamo kwenye chupa. Nilichukua slesi tatu za mikate, nilimpakia siagi na kumuandalia kwenye sahani pamoja na kikombe cha chai nikampelekea.
“Karibu shemeji” nikamwambia wakati nikimuwekea sahani.
“Asante shemeji”
Nikakaa kando yake kumzungumzisha huku akiendelea kunywa chai.
Alipomaliza kunywa chai alinishukuru. Nikaenda kuiondoa ile sahani na kuirudisha jikoni. Nikarudi tena pale sebuleni. Tuliendelea kuzungumza hadi mume wangu alipotokea. Niliwaacha wakisalimiana nikaingia chumbani.
Nilijilaza kitandani na kuanza kuwaza jinsi ya kuifanya ile dawa yangu wakati kulikuwa na mgeni ambaye angekula kile chakula. Isitoshe nisingeweza kufunga bomba na kusingizia maji yamekatika wakati kulikuwa na mgeni huyo.
Nilijimbia kama itagundulika kuwa maji yanatoka ispikuwa niliyafunga na kusingizia kuwa maji yamekatika, ningeeleweka vibaya mbele ya mgeni. Ningeonekana kama nimemfungia yeye na kwamba sikuvutiwa na ujio wake.
Nikaona nimpigie simu shoga yangu Rita.
“Tumepata mgeni” nikamwambia Rita alipopokea simu yangu.
“Ni nani?” Rita akaniuliza.
“Ni shemeji yangu, ndugu yake mume wangu. Sasa sijui itakuwaje?”
“Kwani yeye atakuzuia nini?”
“Si ile dawa nilitakiwa niitie kwenye chakula”
“Kama nakumbuka vizuri yule mzee alikwambia hata wewe mwenyewe unaweza kula hicho chakula, kwani si kuna huyo mdogo wake mwingine mnayeishi naye. Si pia atakula hicho chakula?”
“Sasa kama hilo si tatizo, kuna tatizo jingine. Nikiyafunga yale maji, si nitaonekana nimemfungia mgeni? Si unakumbuka tulikubaliana nisingizie kuwa maji yamekatika ili huyu bwana aoge kwenye ndoo?”
“Kwani huyo mgeni atakaa kwa siku ngapi?”
“Sijajua bado”
“Unaweza kusubiri hadi atakapoondoka”
“Naona nachelewa”
“Sasa utafanya nini?”
“Sina la kufanya, itabidi nisubiri hadi atakapoondoka lakini ndio hivyo moyo waumia”
“Subira huvuta heri msichana, acha pupa” Rita akaniambia kwa mzaha. Tukacheka.
“Najua kuwa subira huvuta heri lakini ngoja ngoja nayo huumiza matumbo”
Wakati nasema hivyo mume wangu akafungua mlango ghafla na kuingia ndani. Nikazuga hapo hapo.
“Basi shoga tutaongea baadaye, ngoja nimuhudumie mume wangu ndio amerudi sasa hivi kutoka kazini”
Sikungoja jibu lake nikakata simu.
“Unazungumza na nani?” Ibrahim aliposikia namsema akaniuliza.
“Nazungumza na jirani yangu Rita” nikamwambia huku nikinyanyuka kitandani.
“Umempa chakula mgeni?”
“Nilimpatia chai tu na slesi tatu, hakukuwa na chakula”
“Jioni utapika nini?”
“Mh! Sijajua bado. Ulitaka njipike nini?”
“Labda ukaange chipsi, viazi si vipo?”
“Viazi vipo”
“Kaanga chipsi na mayai”
Baada ya kuzungumza hivyo na Ibrahim nilitoka mle chumbanni nikaingia jikoni na kuanza kumenya viazi. Mpaka inafika saa mbili usiku, chipsi kwa mayai ya kukaanga zikawa tayari. Ndani ya friji kulikuwa na jagi la juisi ya matunda. Nikaenda nalo mezani.
Baada ya kuyayarisha mlo huo nikaenda sebuleni kumuita mume wangu na shemeji zangu.
Tulikula pamoja. Baada ya kula wenzangu waliondoka na kuruidi sebuleni, wakaniacha nikiondoa vyombo.
Muda wa kulala ulipowadia nilimuuliza Ibrahim kama mdogo wake aliyekuja kutoka Dar alikuwa amepata likizo kazini kwake.
“Sijamuuliza kama alipata likizo” Ibrahim akanijibu.
Nikataka nimuulize ataondoka lini lakini niliona swali hilo halikuwa la msingi kumuuliza mume wangu hasa kwa kuzingatia kuwa yule alikuwa ndugu yake.
Asubuhi ya siku iliyofuata nilifurahi Ibrahim alipoondoka na mgeni wake. Walikwenda kunywa chai huko huko.
Walipoondoka tu nikaenda kwa Rita.
Baada ya kusalimiana naye aliniuliza “Vipi?”
“Mpango wangu umekwama” nikamwambia huku nikiketi kwenye kochi.
“Kwa sababu ya huyo mgeni?”
“Na sijui ataondoka lini!”
Rita alipoona nimechukia akanicheka na mimi nikajidai kucheka.
“Huyo mgeni siku zote haji, anangoja nina mipango yangu ndio anakuja. Si balaa hili!”
“Pengine hatakaa sana, ni wasiwasi wako tu”
“Kama hatakaa sana ndivyo ninavyotaka”
Mgeni huyo alikaa kwetu kwa siku nne. Usiku wa siku hiyo ya nne akaniambia kuwa kesho yake ataondoka kurudi Dar kwani alikuja kutujulia hali tu. Nilifurahi sana aliponiambia hivyo.
Asubuhi ya siku iliyofuata Mashaka akaondoka kurudi Dar. Nikaona sasa nitumie ile nafasi kufanya ile dawa yangu. Ilipofika jioni nilijaza maji kwenye ndoo zote na kwenye mabeseni kisha nikaenda kufunga mita ya maji.
Mume wangu alipokuja nikatangulia kumwambia kuwa maji yalikuwa yamekatika.
“Yamekatika saa ngapi?” akaniuliza.
“Hivi jioni”
“Sasa tutaoga nini?”
“Niliwahi kuchota. Nimejaza ndoo zote”
“Oh! Umefanya vizuri sana”
Ilipofika usiku yeye alikuwa wa kwanza kwenda kuoga. Aliponiambia nimtayarishie maji, nikaenda kukichukua kipakiti kimoja kati ya vile viwili nilivyopewa na mganga, nikachota ile dawa na kuitia mara tatu kwenye ndoo kama alivyoniagiza yule mganga.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 10


Baada ya kusalimiana naye aliniuliza “Vipi?”
“Mpango wangu umekwama” nikamwambia huku nikiketi kwenye kochi.
“Kwa sababu ya huyo mgeni?”
“Na sijui ataondoka lini!”
Rita alipoona nimechukia akanicheka na mimi nikajidai kucheka.
“Huyo mgeni siku zote haji, anangoja nina mipango yangu ndio anakuja. Si balaa hili!”
“Pengine hatakaa sana, ni wasiwasi wako tu”
“Kama hatakaa sana ndivyo ninavyotaka”
Mgeni huyo alikaa kwetu kwa siku nne. Usiku wa siku hiyo ya nne akaniambia kuwa kesho yake ataondoka kurudi Dar kwani alikuja kutujulia hali tu. Nilifurahi sana aliponiambia hivyo.
Asubuhi ya siku iliyofuata Mashaka akaondoka kurudi Dar. Nikaona sasa nitumie ile nafasi kufanya ile dawa yangu. Ilipofika jioni nilijaza maji kwenye ndoo zote na kwenye mabeseni kisha nikaenda kufunga mita ya maji.
Mume wangu alipokuja nikatangulia kumwambia kuwa maji yalikuwa yamekatika.
“Yamekatika saa ngapi?” akaniuliza.
“Hivi jioni”
“Sasa tutaoga nini?”
“Niliwahi kuchota. Nimejaza ndoo zote”
“Oh! Umefanya vizuri sana”
Ilipofika usiku yeye alikuwa wa kwanza kwenda kuoga. Aliponiambia nimtayarishie maji, nikaenda kukichukua kipakiti kimoja kati ya vile viwili nilivyopewa na mganga, nikachota ile dawa na kuitia mara tatu kwenye ndoo kama alivyoniagiza yule mganga.
SASA ENDELEA
Nilipoona bado ilikuwa ikielea juu ya maji, nilitia mkono wangu nikatibuatibu yale maji, ile dawa ikapotea.
Wakati mume wangu anaoga nilikuwa nikitayarisha chakula mezani, ile dawa nyingine nikaitia kwenye wali upande ule ambao nitamtilia yeye kwenye sahani.
Baada ya kuoga mume wangu alikuja mezani. Mara tu alipoketi kwenye kiti nilimsikia akisema.
“Mbona kichwa kinaniuma halafu macho yanniwasha?”
Akawa anayafikicha fikicha macho yake.
“Hicho kichwa kimekuanza saa ngapi?” nikamuuliza.
“Kimenianza wakati huu huu”
“Basi kula chakula halafu ule dawa”
Hapo hapo nikamuona akitikisa kichwa na kutazama kila upande kwa haraka haraka kabla ya kuniambia.
“Haa! Mke wangu macho yangu yamefunga kiza, sioni kitu!”
“Huoni kitu kwa sababu gani?” nikamuuliza.
“Sijui” akaniambia huku akijitahidi kuyafumba macho yake na kuyafumbua.
“Au ni kwa sababu ya hicho kichwa ulichosema kinakuuma?”
“Kichwa hakiwezi kusababisha macho yasione kabisa. Mimi sioni kabisa”
Wakati akisema Ibrahim alikuwa akiyaangaza macho yake kila upande kutafuta mwanga.
“Mke wangu nimepofuka macho!” akaniambia kwa sauti iliyotia huruma.
Nikaguna. Maelezo hayo yalikuwa yamenishangaza.
“Hebu nitazame nione macho yako” nikamwambia.
Mume wangu akageuza uso wake upande wangu. Macho yake yalikuwa ni mazima lakini yalionesha wazi kuwa hayakuwa yakiona kitu.
“Huoni kabisa?” nikamuuliza.
“Sioni”
“Mbona macho yako ni mazima na yako kama kawaida?”
“Sasa sijui kilichonitokea. Hii hali nimeiona baada ya kumaliza kuoga”
Isijekuwa ni ile dawa niliyomtilia kwenye maji aliyooga ndiyo iliyompofua macho mume wangu? Nikajiuliza kimoyomoyo.
Wakati nikijiuliza hivyo Ibrahim alikuwa akijitahidi kuyafikicha macho yake huku akijaribu kutazama bila mafanikio.
“Sijui ni kitu gani kimenitokea jamani?”
akajisemea peke yake.
“Hebu nisubiri hapo hapo” nikamwambia na kuinuka.
Niliingia chumbani nikiwa nimekishika kile kipakiti cha dawa niliyomtilia kwenye chakula. Nikakitazama vizuri. Hapo hapo niligundua kuwa nilikuwa nimechanganya zile dawa. Ile dawa niliyoambiwa nimtilie kwenye chakula ndiyo niliyomtilia kwenye maji ya kuoga na ile niliyoambiwa nimtilie kwenye maji ya kuoga nilimtilia kwenye chakula.
Sasa nikajiuliza ile dawa ndiyo iliyompofua macho Ibrahim kwa sababau niliitumia kinyume na nilivyoagizwa?
Nikamsikia Ibrahim akiniita.
Nikatoka mle chumbani na kumfuata pale kwenye meza.
Ibrahim alinigundua kuwa nimefika kwa kunipapasa.
“Bado huoni kabisa” nikamuuliza.
“Sioni, naona kiza kitupu. Yuko wapi Zacharia?”
“Nafikiri yuko nje”
“Hebu muite”
Nikatoka nje na kumuita Zacharia mdogo wake. Zacharia alinifuata mezani akijua nimemuitia chakula.
“Huyu hapa” nikamwambia ibrahim.
“Zacharia!” Ibrahim akamuita.
Zacharia mwenyewe alishituka kuitwa na kaka yake kwa sauti kubwa akiwa yuko karibu naye kabisa.
“Ndiyo kaka”
“Nilikuwa nimekwenda kuoga, sasa natoka bafuni nije hapa nikaona kichwa kinaniuma. Mpaka nafika hapa macho yangu yakazima kabisa. Hivi tunavyozungumza sioni kabisa”
“Alah! Huoni kabisa” Zacharia akamuuliza kwa mshangao.
“Sioni. Tangu muda huo nilikuwa namueleza shemeji yako kuwa sioni”
“Ina maana ni macho yenyewe tu hayaoni au kuna sababu?”
“Sijui”
Zacharia akaguna.
“Isije kuwa nina presha, kwa maana kichwa kilianza kuniuma?’
“Labda ni presha” nikaitilia nguvu hoja ya presha.
“Basi twende tukapime. Kama ni presha upate tiba yake”
“Subiri nikavae twende” Ibrahim alisema huku akijitahidi kuinuka kwenye kiti.
Nilimshika mkono nikamuongoza kuelekea chumbani. Tulipokuwa chumbani nilimvua saruni aliyokuwa amejifunga nikampa suruali na shati. Alipovaa nilimwambia achukue pesa za hospitali.
Akafungua kabati na kupapasa kabla ya kuukamata mkoba wake ambao huweka pesa.
“Hebu nitolee shilingi laki moja” akaniambia huku akinipa ule mkoba.
Niliuchukua nikaufungua. Ndani ya mkoba huo mlikuwa na vitita vya noti ambavyo hesabu yake alikuwa akiijua mwenyewe. Pesa hizo ndizo alizokuwa akizizungusha kwenye baishara yake.
Nilihesabu shilingi laki moja nikampa. Hakugundua kuwa ninampa pesa hizo mpaka nilipozigusisha kwenye mkono wake. Akazipokea na kuzitia mfukoni.
Niliurudisha ule mkoba kwenye kabati kisha nikatoka naye.
“Zacharia uko wapi?” akauliza mara tu tulipotoka chumbani.
“Niko hapa” Zacharia aliyekuwa amekaa kwenye meza alimjibu.
“Njoo unishike mkono twende, nafikiri hii itakuwa ni presha” Ibrahim akamwambia kisha akakumbuka kitu.
“Hebu tutolee ufunguo wa gari, nimeusahau” akaniambia.
Nikarudi chumabni na kuchukua funguo ya gari nikampa Zacharia.
“Gari utaendesha wewe” nikamwambia.
“Itabidi”
Zacharia akamshika kaka yake mkono wakatoka.
Nilipobaki peke yangu mle ndani nilikwenda ikata ile sehemu ya chakula niliyoitia ile dawa kwa ajili ya Ibrahim, nikaenda kuimwaga kwenye pipa.
Nilihofia kwamba huenda Ibrahim akirudi kutoka hospitali atataka kula. Nilikuwa sitaki ale ile dawa ambayo ilikuwa ni ya kuoga.
Yasije yakatokea mengine, nikajiambia.
Nikataka nimpigie simu Rita nimwambie, lakini niliogopa kutoa ile siri kwamba mume wangu amepofuka macho kwa sababu ya ushirikina wangu.
Lakini nilipanga kwamba kila itakavyokuwa kesho yake niende kwa yule mganga nimueleze hali iliyotokea, pengine angeweza kuwa na ufumbuzi.
Kwa upande mwingine nilijipa moyo kwamba huenda dawa ile aliyooga siyo iliyomfanya mume wangu asione bali ni presha kama mwenyewe alivyokuwa anahisi.
Niliomba Mungu iwe ni presha kweli. Kama itakuwa si presha itakuwa ni ile dawa, nilijiambia.
Ilipita karibu saa nzima, nikampigia simu Zacharia. Zacharia alipopokea simu nikamuuliza.
“Enhe mmefika hospitali?”
ITAENDELEA
 
Back
Top Bottom