Wakipekee
JF-Expert Member
- Aug 21, 2019
- 5,355
- 9,222
Episode 01
Ulikua usiku mzuri ambapo kulikua na mawingu angani yaliyochangia kuleta ubaridi. Nilivaa sweta swetu zito lililonikinga na baridi ile, tayari ilikua saa tatu na dakika kumi siku ya tarehe 24/12 tulipoingia kanisani kukesha kabla ya kuipokea siku ya Xmas. Watu walikua bize kusherehekea mkesha wa sikukuu hiyo kubwa ya mwisho mwaka. Kwa wakiristo ilikua siku muhimu sana. Wengi walikua makanisa wakifanya ibada na kuimba nyimbo mbalimbali za kusifu na kuabudu.
Binafsi sikuwahi kusali kwa walokole ila kutokana na ushawishi wa rafiki yangu aitwae Juvi ambaye tulikua tumepanga nyumba moja nilijikuta nami nimeenda kujionea mambo yanavokuaga.
Kiukweli nilipitia wakati mgumu sana maana sikua na utaalamu wowote wa kuomba na kunena Kwa lugha kama wenzangu walivofanya, walau wakati wa kupiga mapambio nilikua naungana na waumini wengine maana zile nyimbo nilikua na idea nazo, inshu ilikua kwenye kucheza lakini ilinibidi nikomae tu kibishi.
Muda ni kama ulikua umeganda nilitamani kurudi home lakini nilishindwa ikabidi tu nijikaze. "Ningejua nisingekuja" nilijalumu moyoni mwangu, nilikua nimechoka Sana na nilitamani kurudi home kulala, lakini nikasema kama nimevumilia hapo awali muda wa kama masaa mawili nashindwa vipi muda kidogo ulibakia kufika tamati ya mkesha. Mara nikiwa katikati ya lindi la mawazo sauti za shangwe zikasika "amezaliwaaaa.... kazaliwaaaa..." Watu walishangilia kwa nguvu sana. Tayari ilikua imeshafika saa sita kamili usiku, kumaanisha kua tayari siku ilishabadirika kua tarehe 25/12 siku aliyozaliwa Yesu ambapo sikukuu ya Xmas hufanyika.
Walau sasa niliweza kutabasamu maana nilikua na uhakika wa kurudi ghetto kulala, kiukweli nilikua nimechoka sana. Nilimfuata Juvi ambaye ndiye tuliyekua tumekuja nae kwenye ule mkesha. Tulianza safari ya kurudi nyumbani. Njiani tulikutana na watu wengi tu maana wengine pia walikua wakirudi kutoka kwenye makanisa wanayosali. Tukiwa tunakaribia nyumbani tulikutana na mabinti wawili nao walikua wakirejea nyumbani. Tulisalimiana na kupiga stori mbili tatu ili kufupisha safari Katika maaongeza nilitokea kumkosha binti mmoja Kati ya wale wawili kibaharia nikafanikiwa kupewa namba yake ya simu.
Niliporudi ghetto nilimpigia simu na tulipiga sana stori kama vile tunafahamiana Kwa siku nyingi nikafanikiwa kumshawishi kesho aje gheto Nile tunda kimasikhara akakubali basi nikazima simu na kulala.
Ulikua usiku mzuri ambapo kulikua na mawingu angani yaliyochangia kuleta ubaridi. Nilivaa sweta swetu zito lililonikinga na baridi ile, tayari ilikua saa tatu na dakika kumi siku ya tarehe 24/12 tulipoingia kanisani kukesha kabla ya kuipokea siku ya Xmas. Watu walikua bize kusherehekea mkesha wa sikukuu hiyo kubwa ya mwisho mwaka. Kwa wakiristo ilikua siku muhimu sana. Wengi walikua makanisa wakifanya ibada na kuimba nyimbo mbalimbali za kusifu na kuabudu.
Binafsi sikuwahi kusali kwa walokole ila kutokana na ushawishi wa rafiki yangu aitwae Juvi ambaye tulikua tumepanga nyumba moja nilijikuta nami nimeenda kujionea mambo yanavokuaga.
Kiukweli nilipitia wakati mgumu sana maana sikua na utaalamu wowote wa kuomba na kunena Kwa lugha kama wenzangu walivofanya, walau wakati wa kupiga mapambio nilikua naungana na waumini wengine maana zile nyimbo nilikua na idea nazo, inshu ilikua kwenye kucheza lakini ilinibidi nikomae tu kibishi.
Muda ni kama ulikua umeganda nilitamani kurudi home lakini nilishindwa ikabidi tu nijikaze. "Ningejua nisingekuja" nilijalumu moyoni mwangu, nilikua nimechoka Sana na nilitamani kurudi home kulala, lakini nikasema kama nimevumilia hapo awali muda wa kama masaa mawili nashindwa vipi muda kidogo ulibakia kufika tamati ya mkesha. Mara nikiwa katikati ya lindi la mawazo sauti za shangwe zikasika "amezaliwaaaa.... kazaliwaaaa..." Watu walishangilia kwa nguvu sana. Tayari ilikua imeshafika saa sita kamili usiku, kumaanisha kua tayari siku ilishabadirika kua tarehe 25/12 siku aliyozaliwa Yesu ambapo sikukuu ya Xmas hufanyika.
Walau sasa niliweza kutabasamu maana nilikua na uhakika wa kurudi ghetto kulala, kiukweli nilikua nimechoka sana. Nilimfuata Juvi ambaye ndiye tuliyekua tumekuja nae kwenye ule mkesha. Tulianza safari ya kurudi nyumbani. Njiani tulikutana na watu wengi tu maana wengine pia walikua wakirudi kutoka kwenye makanisa wanayosali. Tukiwa tunakaribia nyumbani tulikutana na mabinti wawili nao walikua wakirejea nyumbani. Tulisalimiana na kupiga stori mbili tatu ili kufupisha safari Katika maaongeza nilitokea kumkosha binti mmoja Kati ya wale wawili kibaharia nikafanikiwa kupewa namba yake ya simu.
Niliporudi ghetto nilimpigia simu na tulipiga sana stori kama vile tunafahamiana Kwa siku nyingi nikafanikiwa kumshawishi kesho aje gheto Nile tunda kimasikhara akakubali basi nikazima simu na kulala.