mheshimiwa Mkapa amewachana live wapinzani na hasa ambao wanajiita wanataka kuiokomboa nchi akina CHadema
mosi akiwaambia kuwa CCM na serikali yake ndio ilioikomboa nchi tokea 1961
CCM na chama chake ndio kilichoshirikiana na nchi za jirani kuweza kujikomboa kutoka kwa wakoloni na mabeberu
amezungmzia suali zima la kubinafsisha na kuonesha jinsi gani walivyotekeleza sera hio kwa ufanisi, na kuwaita wapinzani wavivu wa kufikiri
Waliokomboa Tanzania ni watanzania wenyewe bila kujali vyama kwani kipindi hicho kilikuwepo chama kimoja. Hivyo alitakiwa aongee baada ya kuingia kwa vyama vingi. Sio kudanganya watanzania, anazungumzia kuwasaidia Africa kusini sawa lakini kutokana na ufisadi wao ndio maana afrika kusini wako juu sisi tuko nyuma. Asitufanye watanzania wa leo kama wa mwaka 47 tumebadilika na tunataka maendeleo. Iweje yeye rais mwenye mke mmoja na mtoto mmoja na anasaidiwa na kodi yetu kulipiwa kila kkitu katika maisha yake yote. Awe na tamaa ya kujilimikisha mali kupita kiasi ya nn kama sio wizi na tamaa