Mkapa: Kuna mtu kanizomea?

Natumai hao ndugu na majamaa ndo wapo humu ndani kumpigia chapuo ni kama wanalipa fadhila kwa neema waliyoipata kutoka kwake!!..nahisi kabisaa naniii ....atakuwa mmoja wapo
 
Mkuu umejibiwa mr clean kafanye mengi lakini kaboronga mengi.makaburu wa Africa kusini walimuuliza steve Biko kwamba je hakuna jema lolote ambalo weupe wameifanyia Africa kusini? Akajibu yapo lakini not worth commenting. umejibiwa pia baya moja ufunika mema yote. Research inaonyesha kwamba kukua kwa uchumi huo unaosema ukuendana na kupungua kwa umaskini wala utapiamulo Tanzania. kumbe basi pesa za kigeni zilitokana na tanzania kuuza resources zake kwa pei ya kutupa na siyo uzalishaji mali.Ukiangalia bei halisi ya resources za tanzania alizouza ulinganishe na hayo unayoona amefanya utakuta loss kubwa. Hao waliotangulia na waliofuata wangeuza au wakiuza resources za Tanzania kwa speed na bei ya mkapa taifa lingecolapse.Hataivyo mwanao akiwa wa kwanza darasani baada ya kupata alama 40% utajua darasa hili ni la wachovu huwezi ukamsifia ilihali unajua kafeli.
 
Kila awamu ilikuwa na mazuri yake na mabaya ukianzia kwa Mwl Nyerere hadi kwa Kikwete. Hayo madudu yaliyofanywa kwenye miaka ya mwisho ya Ben na wasaidizi wake yasiwe nongwa. Kina Mkono, Bhoke na wengine walifaidika na utawala wa awamu ya kwanza.
Linga nisha yaliyofanyika katika awamu ya nne kwa miaka hii mitatu na halafu jaribu kufikiria hali itakuwaje mpaka tunapofika 2015.
 
Mh. inawezekana huoni wanaokuzomea physically, lakini nakuhakikishia watu wanasononeka mioyoni mwao kwa mambo ambayo ulitenda aidha bahati mbaya au kwa makusudi au kwa kuingizwa mjini na waliokuwa wakikuzunguka including mkeo. Mh. ulipoingia madarakani kwa ujasiri mkubwa ulitangaza mali ulizokuwa nazo lakini ulipoondoka ulishikwa na kigugumizi cha kutaja mali zako kwani ulijua ulichokikifanya watanzania hawatakipenda. Hivyo japo unatuona kimya lakini moyoni watanzania tunakuzomea.
 
mikataba ya kihuni karibu yote ilisainiwa kipindi chake..........
 
Unakubali tulinganishe madudu yao?? Kuzomewa alikokutaja kunahusiana na nini?
 
Hivi anafikiri hizo hela zote alizochukua atazikwa nazo???????????? Shame on him!! He is dispeakable. Yaani hata sina cha kuongezea yote mmeyamaliza hapa. One day HE WILL PAY FOR ALL EVIL THINGS HE HAS DONE!
 
Mapokezi aliyoyapata hayamaanishi kama wanampenda au wanamuheshimu sana.....
Kumzomea sio ishara kwamba hakuboronga ..moyoni mwake anajua madudu aliyoyafanya iko siku asiyoitarajia atafedheheka na kukumbuka kwa nini hakuzomewa
 

Mwanangu lugha hiyo imenikuna, manake hapo hujauita mguu ukucha, ila umeonyesha jinsi mguu huo ulivyokuchosha na usivyostahili kuwa mguu. Kula tano!
 
Mkapa anajifanya kasahau kwamba akienda vijijini, amri na hofu wanayopewa wanakijiji, inatosha kuwafanya kutii mamlaka pindi inapolazimisha jambo fulani. Na hilo ndilo lililo tokea wilayani Kilolo. Hebu, ajipitishe Manzese tu, hata bila mwaliko apate habari yake. Bahati mbaya zaidi, Mkapa ni mwizi tunayejua. So unlucky!! Hata asipojionyesha, bado tunajua ni mwizi, hata akijionesha tunajua ni mwizi. Kwetu sisi, kulia na kucheka kwake, yote ni makelele tu.

Watu bado tuna usongo naye, yeye anatuletea hizo?

Hata kama akijifananisha kiutendaji na wezi wengine, naye kujiona ni afadhali kidogo (though i doubt this) hiyo hai uhalalishi wizi wake. Akitaka ajibu hoja ya mambo aliyoorodhesha BUBU pale juu. Aache ghilba.
 
Sina commemnts.Ninachokijua watanzania tu waoga hatuna ubavu wa kumzomea kiongozi mkubwa kama yeye ila dhambi anazo tena za kutisha.
 
Tatizo ni kwamba yeye as Mkapa ni mwizi , vile vile Jakaya Kikwete ni mwizi sasa wanapokutana wezi wawili wanashindana nani kaiba zaidi ndio sababu ana hii jeuri, kwa sababu anafahamu Jakaya Kikwete hawezi kufanya lolote. Waacheni wasubiri siku ya siku itakapowadia watasimuliana vizuri Segerea .
 
Watanzania naona bado tunatafuta mchawi/wachawi wa matatizo yetu. Ningeshauri sote tutafute vioo vya kujiangalia ikiwezekana hata vile vya mwili mzima. Jibu liko huko kwenye vioo.

Kama hakuzomewa inamaanisha ya kwamba waliompokea hawajaona au hawajui ubaya wa alichofanya. Sasa mtu atazomea kitu kizuri?? Haingii akilini
 
“Mmeona mapokezi yangu, kuna mtu yeyote amenizomea? Sijifichi na wala sikimbii kuzomewa, mimi niko ‘busy’ sana na shughuli za kimataifa baada ya kumaliza utumishi wangu serikalini,” amesema Mkapa.


CHANZO: Habari Leo

hapa kuna tatizo. kwa heshima aliyo nayo si mtu wa kuyatamka haya
 
The guy would do better maintaining his silence instead of mocking the Tanzanians he has wronged. He has neither political credibility nor charisma. As well, this isn't simply a matter of comparison between good and bad deeds of an individuea; or criminal doings of presidents past and present.

His was a regime that mainstreamed heinous economic crimes that threaten to destabilise the country's growth and socio-economic development (involving key institutions: the Central Bank, TISS and TPDF). And he had the audacity to claim, in the inetrantional press, of being duped by the Bretton Woods institutions in dishing out major national assets to foreign investors - without realising the expected (huge) returns!
 
Yeye alikuwa anahutubia madaktari na manesi , sasa ajitokeze kwenye mkutano wa hadhara kwani ndio ataona kama atazomewa ama laa.

Ila kama alikuwa anasubiria hilo na halikutokea juzi basi atakua anaishi kwa hofu kubwa sana ,maana kila anapoenda anakuwa na hofu ya kuzomewa .

Heri mfungwa wa gerezani kuliko kufungwa kifungo cha jamii...
 
Jamani jamani, Mkapa ni Msaliti wa taifa. Ni mtu ambaye baba wa taifa alizunguka nchi nzima kumnadi kwa ndiye mtu safi. Kweli jamaa alikuwa safi ukilinganisha na walijitokeza wakati huo(kama sio alikuwa bado kazubaa). Kiuwezo wa akilia na ufanyaji kazi jamaa ni safi kabisa. Tukamwamini baba wa taifa, tukamuunga mkono, tukijua Waarabu hawatapata nafasi ya kuchukua Loliondo nyingine. Uuuuuwiiiii! Usimuamshe aliyelala, jamaa kajanjaruka, kalaghaiwa na wazungu, eee bwana eeee....wacha aipige nchi mnada. Huku htaki kusikia la mtu. Wabunge wakakandamizwa, atakayeleta fyoko,harudi bungeni next time! Dhahabu yetu ikapigwa mnada, migodi mikubwa ikafunguliwa 1999, 2000, 2002, 2003 baada tu yule aliyemweka hapo alinde mali hizo kumrudia muumba wake! Kajiuzia mgodi mkubwa wa makaa ya mawe kwa shiling millioni 700 akatanguliza milioni 70, akaanza kuvuna! Milioni 700 kwani unanunua nyumba Temeke? Mgodi wenye thamani ya mabilioni! Kumbukeni kauli mbiu ya uchaguzi mwaka 1995 ilikuwa "hakuna biashara ikulu". Asiyejua kosa kubwa tulilofanya wakati wa Mkapa kama nchi ni uuzaji wa maeneo ya DHAHABU, ikishachimbwa hatakaa ijitengeze milele. Wamechukua bure! kama huamini fuatilia Ghana, SA, Mali na Zimbabwe, utagundua jamaa alituingiza mjini kama yeye si Mtanzania! Watu wanasema ni wa Msumbiji, yawezekana kabisa.

Jamaa ni msaliti kabisa, uwezo alikuwa nao lakini akautumia kuumiza nchi. Mazuri aliyofanya ilikuwa ni ghiliba kutuibia, naamini hivyo.
 
Wadanganyika Wenzangu,
Nawasalimu katika jina kuu kupita majina yote.
Zamani nilipokuwa kijana mdogomdogo nilikuwa simuamini Bwana Julius Kambarage Nyerere, nilimuona kama mtu fulani mjanjamjanja hivi, na nilivyokuwa nikisoma habari za Historia mbalimbali za viongozi wa Afrika, niliona wengi wanafananafanana hivi. Niliamini kwamba Nyerere lazima atakuwa amejilimbikizia mali kama vile Mobutu. Lakini Baada ya kifo chake na hata sasa nina hakika mwalimu was the real son of Tanzania and Afrika. Alikuwa masikini, kama alivyokuwa kawawa, Sokoine , Timothy Apiyo na wengine wachache waliomzunguka mwalimu.Na hilolinadhihirishwa na namna familia yake inavyoishi sasa, ni masikini tena kuliko wengi wetu humu ndani.Enzi ya Nyerere Viongozi walikuwa na adabu, siyo hawa wa sasa hivi kila mtu anajifanya yeye ndio yeye.
Sasa njoo kwa Mzee Ruksa, ruksa ni mtu mpole mnyenyekevu, na ndiyo maana utawala wake watu walifanya walivyotaka na yeye alikaa kimya.
Na huyu BIG Ben nasema hapana, ni worse, amefanya mambo mengi ya aibu kwa Rais. amekebehi watanzania na kujuona kuwa yeye ndio yeye , sisi ni mabwege tu atufikiri chochote, wavivu tu . Hakika JF Hakuna mvivu.
JK amekuwa mkimya sana, bado hajalipa matarajio ya wapiga kura wake, anapiga debe badala ya kupiga kazi, Aaache debe apige kazi kisha tumpime.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…