Mkapa anaongoza nchi kimyakimya?

Mkapa anaongoza nchi kimyakimya?

mnyinda

JF-Expert Member
Joined
Sep 25, 2012
Posts
277
Reaction score
64
Rais Jakaya Kikwete jana alikiri mbele ya mkutano mkuu wa CCM kuwa mambo yote yaliyofanyika ni ushauri wa Benjamini Mkapa. Kikwete aliyasema hayo wakati akiwashukuru wanachama walio mpigia kura alisema,

ninanukuu,
''mara nyingi mimi huwa nikisha jifungia ikulu huwa sielewi kinacho endelea na wakati mwingine hawa majamaa huninyang 'anya hata simu yangu ya mkononi ili watu wasinisumbue lakini mzee Mkapa akisikia au kuona jambo yeye kwakuwa hazuhiliwi pale ikulu hunifuata moja kwa moja na kunipa maelekezo ndugu wajumbe hata utaratibu tulioutumia kwenye mkutano huu ni mzee Mkapa kapangilia''.

Hivyo inaonesha jinsi gani Mkapa anavyomsaidia JK
 
Kuna mambo mengi hapo baadaye atayaropoka. Hili nililihisi pia, kuna maamuzi ameshayafanya ambayo nikiangalia uwezo wake siamini kama kweli ni yeye aliyeyafikiria, huenda ni Mkapa
 
Mkapa ni jembe. Nahisi kama hasingekuwepo hizi campaign za ndani kwa ndani za kumpinga mwenyekiti zingezaa matunda. JK mshukuru sana mzee Mkapa, amekukingia kifua sana tu japo umechelewa kutoa shukrani waziwazi.
 
Ni heri Mkapa arudi Ikulu Kimya kimya kama Dereva wa Train apitavyo na kusababisha watu kugonga Train.

Mwanzo alifikiri ni mambo kirahisi hivyo ila naona Mkapa ameshituka na kuona nchi hii inaenda kushoto na mapinduzi yakifanyika basi na yeye yupo kikaangoni.

Ndiyo maana safu ya uongozi wa CCM inabadilika. Nina imani kuwa hata WIZARA na hasa PM nao watabadilka na kuleta wachapakazi na si Wasanii au Mafisadi.

Simpendi Mkapa kwa Ufisadi wake ila walau KAZI linachapa. Anaiba shilingi 20 na kuleta BoT shilingi 100. Sasa unapokuwa na Rais ambaye haleti na haibi ila ANATUMIA sh.100 zote, basi ni heri Mwizi wa Sh.20 na analeta Sh.100.
 
Huu ndio uungwana. Mshukuru sana maana anastahili!
 
Dah!mkapa very strategic,kwahiyo alisoma mchezo akawa analia time tu,halafu muda wote wakati wa vikao alikuwa anatafuna kitu kama bubble gum.hata hivyo kutambua uwezo na mchango wa mwingine ktk kukufanikishia jambo ni busara,maana amesema ukweli na hilo litamfanya awe huru sana ktk nafsi yake.so mkapa kaamua kumbabua lowasa na mikakati yake yote.
 
For the sake of JF Status, nawaomba Mods wafanyie editing ya hii kitu. Maana inaumiza kichwa na macho.
 
tutamsema mzee mkapa kwa mabaya lakini ukweli unabaki pale pale kuwa ni kiongozi shupavu,mahili,jasiri,mwenye msimamo ma kwa uchache wa sifa hzo ndo maana anaheshmika na kuaminika nje ya nchi
 
Inasemekana hata kuwadhibiti siasa kali Mkapa ndio anawashauri nini cha kufanya...wao pekee wasingeweza. Chezea chinga weye...
 
hawezi kumshauri kusafiri,ila mi nafurah kama anamshauri maana huo ndo uanaume,kumwacha mwenzio anadhalilika si vizuri,big up uncle ben
 
mbona ajamshauri walioiba pesa za wananchi na kuzificha nje wakamatwe na kurejesha!!
 
mkapa anafanya kazi ya usalama wa taifa? maana JK anataka kudai kuwa usalama wa taifa hawamsaidii kama mkapa anavyosaidia, wao wamefanya kumnyang'anya simu (which also shows he is not serious-hawezi kucontrol matumizi ya simu yake mwenyewe kwa kuzingatia majukumu yake) mengineyo kama kumpa taarifa ya kinachoendelea hakuna..nlifikiri mkapa angehitajika kwa ajili ya uzoefu wake..mara1 moja mambo yakionekana yanaelekea pabaya...duh kama ndivyo kumbe tuko vibaya kuliko nlivyofikiri..
 
Kwa maneno hayo mkapa alimpa shart kwanza ukitaka nikusaidie mrudishe kwanza magula jk sawa mzee,kati ya watu ambao jk alikuwa anawchukia ni mn'gula
 
Rais jakaya kikwete jana alikiri mbele ya mkutano mkuu wa ccm kuwa mamboyote yaliyofanyika ni ushauri wa benjamini mkapa kikwete aliyasema hayo wakati akiwashukuru wanachama walio mpigia kura alisema,ninanukuu, maranyingi mimi huwa nikisha jifungia ikulu huwa sielewi kinacho endelea na wakati mwingine hawa majamaa huninyang 'anya hata sm yangu ya mkononi ili watu wasinisumbue lakini mzee mkapa akisikia au kuona jambo yeye kwakuwa hasuhiliwi pale ikulu hunifuata mojakwamoja nakunipa maelekezo ndugu wajumbe hata utaratibu tulioutumia kwenye mkutano huu nimzee mkapa kapangilia.hivyo inaonyesha jinzi gani mkapa anavyo msaidia jk

sidhani kama ni kweli kuwa mambo yote.
 
Kwahiyo atasafari za nje yeye ndiyo anamshauri aende pia?

Hata usishangae kama safari pia ni ushauri wa Mkapa, maana kama unakumbuka yeye ndio alianza kutanua kila mara unamsikia kasafiri kwenda nje!
 
Rais jakaya kikwete jana alikiri mbele ya mkutano mkuu wa ccm kuwa mamboyote yaliyofanyika ni ushauri wa benjamini mkapa kikwete aliyasema hayo wakati akiwashukuru wanachama walio mpigia kura alisema,ninanukuu, maranyingi mimi huwa nikisha jifungia ikulu huwa sielewi kinacho endelea na wakati mwingine hawa majamaa huninyang 'anya hata sm yangu ya mkononi ili watu wasinisumbue lakini mzee mkapa akisikia au kuona jambo yeye kwakuwa hasuhiliwi pale ikulu hunifuata mojakwamoja nakunipa maelekezo ndugu wajumbe hata utaratibu tulioutumia kwenye mkutano huu nimzee mkapa kapangilia.hivyo inaonyesha jinzi gani mkapa anavyo msaidia jk

Je haiwezi kuwa anaomba samahani kwa aliowapa ahadi za uwongo? Mi nafikiri anajitetea kwa marafiki ili wamwelewe kuwa si maamuzi yake na wasimshugulikie maana wanajua nguvu na madhaifu yake poor him he is going to fall a victim.....Huyo anayemsaidia anafanya ili kukimbiza bawa lake; yeye kwanini hakuchanganya na za kwake? By the way I am very happy my mission is complete only awaiting for the manifestation....See you soon comrades with my motor cades!
 
Back
Top Bottom