Mkapa ainanga serikali ya Kikwete

Mkapa ainanga serikali ya Kikwete

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,866
Reaction score
4,252
Akizungumza katika mkutano wa Mkapa HIV Foundation, kasema lazima taifa hili lijiheshimu na lirudishe heshima yake kwa kutumia sera yake ya kujitegemea.

Kasema kasoma makala fulani kupitia laptop yake kuwa Tanzania ni ya tatu duniani kwa kuomba ikitanguliwa na Afghanistan na Irak.


Maoni yangu:
Kiukweli hii ni aibu kwa serikali ya 'handsome' boy kuomba hivyo. Hivi Tanzania tangu vita ya nduli hadi leo ndo imetuathiri kiasi hiki? Akina irak tunawasamehe kwa madhila waliyopitia. Tanzania umepitia madhila gani? Hii ni aibu kwa JK.

Chanzo: ITV NEWS
 
Mmmmmmmmh!!!!!!!!! yaani kwa maneno mengine hata Somalia wanatuzidi????????? Jamani daaaah!!!!!!! I heti politics totally
 
This is too much. Wakati huyu handsome akiingia magogoni alizunguka dunia nzima kujitambulisha. Leo ndo tumejua ziara zote zile zilikuwa ni za kuombaomba. Halafu wanasema eti ziara za huyu handsome zina tija kwa nchi kumbe kutuchafulia heshima.
 
ni kweli. Hata somalia wametuacha. Tusi la Cameron liliwalenga watu kama jk
 
This is too much.Wakati huyu handsome akiingia magogoni alizunguka dunia nzima kujitambulisha.Leo ndo tumejua ziara zote zile zilikuwa ni za kuombaomba.Halafu wanasema eti ziara za huyu handsome zina tija kwa nchi kumbe kutuchafulia heshima.

Zina tija mkuu,hujaskia kwamba tunaenda kuwa twanga wa iran tukiwasaidia wamarekani?
 
Ni aibu taifa kuwa omba omba. Hatuna sab
abu ya kuwa omba omba wakati tuna rasilimali lukuki. Matatizo haya yote yanaletwa na uongozi mbovu wa kitaifa. Ni aibu kutetea uovu kwa kivuli cha udini. Kama tunalika taifa hili lazima tubadilike, tuache tabia ya kubebana na kuoneana aibu. Kikwete anahaki ya kubebeshwa lawama zote za matatizo haya.
 
This is too much.Wakati huyu handsome akiingia magogoni alizunguka dunia nzima kujitambulisha.Leo ndo tumejua ziara zote zile zilikuwa ni za kuombaomba.Halafu wanasema eti ziara za huyu handsome zina tija kwa nchi kumbe kutuchafulia heshima.

Za kujitambulisha zimeisha.Bado za kuaga.
 
Nadhani kuna watu wajinga tu kwa kuzaliwa: sasa mtu kusema kwa sisi ombaomba ukatoliki au dini yake inaingiaje hapo? Watu hawa ndio watachelewesha ukombozi. Na ukombozi ukija tutaanza kuwanyonga wao kwanza maana ni nuisance!
 
Mmmmmmmmh!!!!!!!!! yaani kwa maneno mengine hata Somalia wanatuzidi????????? Jamani daaaah!!!!!!! I heti politics totally
Jumlisha na Ethiopia, Matajiri wa Tz walienda Ikulu kwa baba riz, kuchangia Somalia njaa. Masikini hawakujua kumbe somalia ni matajiri na hawaombi km TZ, Wenye rasilimali kibao. Aaaaibu sana. Ndo maana wanatuletea masharti ya kicameroon.
 
Baada ya maovu yote aliyotufanyia hili taifa ikiwa ni pamoja na kutuwekea serikali ya sasa, bado ana ubavu wa kuongea! Only in Tanzania.

serikali ya sasa kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali iliwekwa hapo kwa nguvu ya vikundi. Na Mkapa hakuwa upande wa jk. Muulize lowassa ilikuwaje jk yuko madarakani.
 
Ikitokea tajiri kama Mengi awe anatembeza bakuri anaomba pesa mtamwelewa kweli? Ndo tz ilivyo ina mali lukuki
 
Atawale, atawala tu mwacheni JK atawale. Ni zamu yake naye kutawala kwa mtindo anaoona unafaa
 
This is too much. Wakati huyu handsome akiingia magogoni alizunguka dunia nzima kujitambulisha. Leo ndo tumejua ziara zote zile zilikuwa ni za kuombaomba. Halafu wanasema eti ziara za huyu handsome zina tija kwa nchi kumbe kutuchafulia heshima.

Subiri atakavyo anza kuzunguka akiaga nchi rafiki ili rais ajaye aendeleze mazuri.
 
  1. ..kama siyo kusafiri "mngekufa na njaa" by JK
  2. ..kama si safari za rais nje, hali ingekuwa mbaya by Membe
Ila kama kuna mfuatiliaji wa hotuba za JK, nakumbuka alipokuwa anazindua mradi wa barabara wa arusha na wakuu wa EAC, alisema kauli moja ambayo ndiyo kauli mbiu yake kuwa mtu anapoahidi ni vema kumfuatilia "..ni vizuri kukumbusha, yaani mzee unakumbuka ule mzingo uliotuahidi" by JK. Kwa maana hiyo jamaa ni mtalaamu wa kuomba na pia ni mfuatiliaji, alifaa sana kuwa mhasibu!
 
  1. ..kama siyo kusafiri "mngekufa na njaa" by JK
  2. ..kama si safari za rais nje, hali ingekuwa mbaya by Membe
Ila kama kuna mfuatiliaji wa hotuba za JK, nakumbuka alipokuwa anazindua mradi wa barabara wa arusha na wakuu wa EAC, alisema kauli moja ambayo ndiyo kauli mbiu yake kuwa mtu anapoahidi ni vema kumfuatilia "..ni vizuri kukumbusha, yaani mzee unakumbuka ule mzingo uliotuahidi" by JK. Kwa maana hiyo jamaa ni mtalaamu wa kuomba na pia ni mfuatiliaji, alifaa sana kuwa mhasibu!

tatizo jk anamfuatilia mtoa ahadi hadi faraghani, na ndio maana hizi ripoti za kuombaomba zinawekwa hadharani hivi ku discourage haka kamchezo.
 
Kwa hiyo ina maana nchi hii imeomba mpaka waingereza wanataka wa i CAMEROUN BONGO!
 
Back
Top Bottom