Wanajukwaa,salam,
Baada ya kumsikia waziri Mkuu wa zamani,ndugu Edward Lowassa na baada ya kusoma michango mbalimbali humu ukumbini kutoka kwa wanaomuunga mkono na wanaompinga kuhusu ''safari ya matumaini'' nahisi mkanganyiko,
1.Inasemwa kashfa ya Richmondi ilitungwa tu na akina Sitta na Dr Mwakyembe ili ku muangusha Kwenye uwaziri mkuu.Hivyo hapakuwa na kitu halisia kama Richmond scandel,ilibuniwa tu,
2.Lowassa kasema hakufanya kitu chochote kuhusu Richmond bila kumshirikisha mh.Rais.Hata alifikia hatua ya kutaka kuvunja mkataba ila hakukubaliwa.Hapa,je,huo mkataba aliotaka kuuvunja ni upi kama Richmondi ilikuwa ni kitu ya kubuni? Ina maana angevunja mkataba dhahania?
3. Ndg Lowassa anasema alikaa kimya kwa muda mrefu wa takribani miaka saba ili kuilinda Serikali (rais) na chama! Kwa hiyo hapa rais mtarajiwa anakiri kuwa mradi wa Richmond ulikuwa ni ufisadi mkubwa hata wa kuiangusha serikali! Na hivyo,je,tujue lipi,kwamba ni rais pekee ndio alikuwa mhusika wa Richmondi au Rais na Waziri mkuu wake(Lowassa) walihusika pamoja ila yeye alikaa kimya ili bosi mwingine apone(Hapa kama ndio hivyo maana yake uzalendo wake ni kwa mtu na siyo nchi?)
4.Ripoti ya kamati ya Dr.Mwakyembe ilionesha vimemo kutoka kwa PM kwenda kwa mawaziri na mpaka wabunge wa ccm wakashawishika kumhusisha Lowassa na Richmond.Ina maana hawa walikuwa hawaelewi mtego wa Sitta na Dr Mwakyembe,walikuwa wamehongwa au kipi kilitokea?
(Akina ole Sendeka,Kilango Malecela et a' nasikia wameshaungama)
Yote kwa yote,Richmondi ilikuwa kitu REAL au FAKE?
Kama ilikuwa real,Lowassa hakushiriki kabisa au alishiriki pamoja na mh.Rais ila baadae akatolewa sadaka kwa niaba ya mkuu?
Na kama alishiriki pamoja na mkuu wake kwa nafasi yake kunamfanya asiwe fisadi?
Karibuni Wajuaji,mtufumbue wengine macho.