Ukweli kuhusu Richmond utaendelea kubaki kuwa siri ya Baraza la Mawaziri la kipindi hicho cha Lowasa. Hakuna mkataba wowote unaoingiwa bila kujadiliwa kwenye Baraza la Mawaziri. Hivyo, sisi Raia wa kawaida (layman) tunaijadili RICHMOND kijuu juu tu, ukweli wanaujua mawaziri waliokuwepo.
Kuhusu kujiuzulu kwa Lowasa, aliwajibika ili kuinusuru serikali. Kumbuka kuwa kama richmond ilikuwa inaihusu serikali, ilikuwa mkuu wa serikali ndiye awajibike ambaye ni rais. Hivyo ili kuondoa ile total collapse of Government ambayo ingetokea kwa rais kujiuzulu, ikabidi Waziri mkuu awajibike kwa nafasi yake (Uwaziri mkuu), ili kuvunja baraza la mawaziri liundwe upya. Hivyo, issue si Lowasa kama mtu binafsi. Issue ni waziri mkuu ajiuzulu ili kumnusuru Rais asijiuzulu. Kwa maana nyingine ni kwamba, hata kama waziri mkuu wa wakati huo angekuwa Pinda, au Mwakyembe au Sumaye, lazima angewajibika ili kumlinda rais. Ndo maana jamaa alisema tatizo ni uwaziri mkuu.
Pia hata kama asingejiuzulu, bado asingeendelea kuwa waziri mkuu maana baraza la mawaziri lingevunjika kwa president kujiuzulu.
NOTE: Simtetei lowassa kwa nafsi yake, ila ninazungumza kile kilichotakiwa kutokea.
Mikakati yote na hatua zote za kuipata RICHMOND rais alikuwa na taarifa, na naamini alitoa go ahead, baada ya kujadiliwa kwenye Cabinet wakuu.
Tusiwe soft minded kihivyo[/QUOTE
. Msaidizi Mkuu wa Lowassa, Ole Kuyan, katika barua yake kwenda kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anasema,
Endelea kusaini mkataba kati ya Richmond na serikali, maana Waziri Mkuu, Edward Lowassa tayari ameridhika kwamba Richmond ipewe mkataba Kauli kwamba Waziri Mkuu Lowassa ameridhika inafunga mjadala na inadhirisha kwamba Lowassa alijua kila hatua katika kufanikisha mkataba huu. Aidha, kauli ya Kuyan, kwamba Waziri Mkuu ameridhika na hivyo mkataba kati ya serikali na Richmond usainiwe, inaonyesha wazi kuwa Lowassa ndiye aliyekuwa anasimamia jambo hili. Vilevile, ni Lowassa ambaye anatajwa kushinikiza upokonywaji Bodi ya Tenda ya Tanesco kazi ya kutafuta mzabuni, baada ya Bodi hiyo kukataa kuipa kazi ya kufua umeme wa dharula kampuni ya Richmond.
Ni Lowassa yuleyule anayetajwa kushinikiza kupunguzwa kwa vigezo ili kufanikisha azima ya kuipa kazi kampuni hiyo ya kitapeli. Lowassa na wenzake walijua, pasipo na shaka kuwa Richmond ni kampuni isiyokuwa na hadhi, sifa, wala uwezo wa kufanya kazi iliyotaka kupewa.
Hili linathibitishwa na barua ya aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha kwenda kwa Lowassa, ambayo watetezi na wafuasi wa Lowassa wanaitumia kutaka kumsafisha. Barua hiyo yenye Kumb. Na. CDB 286/397/01 ya 17 Juni, 2006 inasema,
Nakubaliana na mapendekezo ya Kamati ya Majadiliano ya Serikali (GNT) ya kuteua Richmond na naomba kuwasilisha kwako, kwa uamuzi na maelekezo. jamani hapa hakuna namna lowasa anaweza mwingiza kikwete kwenye uchafu wake.ila tunajua mfa maji haachi kutapa tapa.chamuhimu hapa ni kujua suala la richmond lilikwisha lowasa aliwajibika kwa makosa yake mwenyewe na si kwa kuiokoa serikali au kwa makosa ya waliyo chini yake.naneno yote niliyo andika hapa yametoka kwenye ripoti ya mwakyembe,ripoti iliandikwa kitaalam kwa miaka saba mnatafuta pakutokea hampaoni ,viva mwakyembe msomi bingwa wa sheria alieitendea haki taaluma yake