Mkakati wa CCM: Hawa ndio Watakaoongoza Kampeni ya NDIYO Katika Katiba Pendekezwa

Standalone

JF-Expert Member
Nov 15, 2014
676
576
Yaan Kila wanachofanya Lumumba tunakipata mapemaa….Angalieni attachment ya Mkakati wa kupitisha kura ya ndio. Fungua kiambatanisho hapa chini.
===========================


MAPENDEKEZO YA MUUNDO WA KAMATI ZA KAMPENI YA KURA YA MAONI YA
KATIBA INAYOPENDEKEZWA

Sheria ya Kura ya Maoni inaanzisha Kamati kwa ajili ya kuendesha kampeni ya kura ya maoni. Kifungu cha 12 cha sheria hiyo kinaanisha kamati hizo kama ifuatavyo:-

Kamati mbili katika ngazi ya kitaifa; na

Kamati mbili katika ngazi ya Jimbo

Kamati hizi zitaundwa na makundi ya watu, vyama vya siasa na taasisi au asasi zinazokusudia kuunga mkono au kupinga Katiba Inayopendekezwa. Swali litakaloulizwa ni lile lililochapishwa na Tume ya Uchaguzi kwenye Gazeti la Serikali na. 414A la tarehe 17 Oktoba, 201: "Je unaikubali Katiba Inayopendekezwa?, mpiga kura atatakiwa kutoa jibu la "ndiyo" au "hapana"

Kamati ya kura ya maoni katika ngazi ya taifa au jimbo inapaswa kuomba usajili kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ndani ya siku ishirini na moja kabla ya kipindi cha kampeni ya kura ya maoni kuanza. Kwa mantiki hiyo, kwa kuwa kipindi cha kampeni cha kura ya maoni kinaanza tarehe 30 Machi, 2015, Kamati husika zinatakiwa kuomba usajili Tume kabla ya tarehe 9 Machi, 2015.

Kwa kuwa Sheria ya Kura ya Maoni inatoa masharti kwa Kamati zinazokusudia kuomba usajili kuteua kiongozi na kuainisha majina ya wajumbe, ni vema tukaanza maandalizi kuhusu suala hili mapema.

Katika kuhakikisha kwamba wananchi wanaipigia kura ya NDIYO Katiba Inayopendekezwa, inashauriwa kwamba muundo wa Kamati ya kura ya maoni kwa ajili ya kuunga mkono swali lililochapishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi uwe kama ifuatavyo:-

Kamati ya kitaifa iwe na jumla ya wajumbe 300.

Katika kamati hii, kila mkoa utapangiwa wajumbe 12 ambao watakuwa na jukumu la jumla la kusimamia Kampeni ya NDIYO katika mkoa husika. Kamati hii itajumuisha wajumbe kutoka:

Makundi ya watu Vyama vya Siasa Asasi zisizo za kiserikali; na Wadau na wakereketwa wa Katiba Inayopendekezwa Namna ya kuwapata wajumbe 12 wa kila mkoa.

Wajumbe watatokana na viongozi wa Chama wa mkoa husika ambao ni:-

- Mwenyekiti wa CCM wa mkoa - Katibu wa CCM wa mkoa

- Katibu wa Siasa na Uenezi wa mkoa - Katibu wa Uchumi na Fedha wa mkoa - Mwenyekiti wa UWT wa mkoa

- Mwenyekiti wa Wazazi wa mkoa - Mwenyekiti wa UVCCM wa mkoa

Wajumbe wengine watano (5) watokane na orodha ya wajumbe 125 walioorodheshwa.

Sababu za mapendekezo haya;

(1) Kuwateua viongozi wa mkoa husika kuwa sehemu ya wajumbe wa kitaifa kutajenga ushirikishwaji wa kutosha kutoka katika mkoa huo ambao kimsingi watakuwa wanajua mbinu zaidi zitakaozwezesha kuongeza ufanisi katika zoezi hili.

(2) Wajumbe watano kutoka katika orodha iliyoambatishwa, washirikisha viongozi wa kitaifa na makundi ya watu wengine vikiwemo vyama vya siasa, Asasi zisizo za Serikali na wadau wengine wakereketwa wa Katiba Inayopendekezwa.

Kamati ya Jimbo imependekezwa iwe na wajumbe 50

Inapendekezwa wajumbe hawa wateuliwe chini ya usimamizi wa Kamati ya Siasa ya wilaya na ijumuishe:

- Viongozi wakuu wa chama wa wilaya

Wabunge wa Majimbo yaliyoko kwenye wilaya

Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya wilaya wenye uwezo wa kuitekeleza kazi hii walioko katika Jimbo husika hususan Madiwani, Wenyeviti wa kata, Makatibu kata, Makatibu wa Siasa na Uenezi, Uchumi na Fedha wa kata na viongozi wa Jumuiya.

Makada wengine wa chama, viongozi wa dini na Asasi nyingine wenye mtazamo wa kuunga mkono Katiba Inayopendekezwa.

MAPENDEKEZO YA MAJINA YA WAJUMBE WA KAMATI YA KITAIFA WANAOTOKANA NA VYAMA YA SIASA, ASASI ZISIZO ZA SERIKALI NA WADAU WENGINE

Orodha iliyoambatishwa iwe ni pamoja na wajumbe wa kitaifa waliopendekezwa kutoka katika mkoa husika, wajumbe wengine wasiotokana na mikoa ni hawa wafuatao:-

VYAMA VYA SIASA

1. Philip Mangula (Mwenyekiti)
2. Abdulrahman Kinana CCM na Jumuiya zake
Mizengo Pinda
Balozi Seif Iddi

Nape Nnauye
Mohamed Seif Khatib
Zakia Meghji
Mwigulu Nchemba

Abdallah Bulembo 10. Sophia Simba

Jerry Slaa
Adam Kimbisa

Khadija Aboud

Emmanuel Nchimbi
Samia Suluhu Hussein

Makame Mbarawa

Anna Tibaijuka

Shamsi Vuai Nahodha

Pindi Chana
Hussein Mwinyi
William Lukuvi

Maua Daftari

Steven Wasira
Jesta Mhagama
Asha Bakari

Amina Makilagi

Eva Kihwele

Salama Aboud
Sadifa Hamis Juma

Sixtus Mapunda
Anna Abdallah
Shaka Hami Shaka
Mfaume Ali Kizigo

Wilson Mukama
Martine Shigela
Anthony Mavunde

37. Hamad Rashid CUF/ADC
38. Khadija Abdalla Ahmed
39. John Cheyo UDP
40. Juma Khamis Faki
41. Rashid Yusuph Mchenga AFP
42. Mwanamrisho Ahmeed Demokrasia Makini
43. Tatu Mbarouk APPT Maendeleo
44. Peter Kuga Mziray
45. Mwanaid O. Tahir NRA

46. Juma Ali Khatib TADEA

47. Augustino Mrema TLP

Hussein Juma

Fahmi Dovutwa

ASASI ZISIZO ZA KISERIKALI

50. Magdalena Rwebangira Chama cha Wanasheria Wanawake
(TAWLA)

51. Siti Abbas Ali Chama cha Wanasheria wanawake
52. Salama Aboud Talib Zanzibar (ZAFELA)
53. Amon Mpanju Shirikisho la Vyama vya Watu wenye
54. Frederick Msigala Ulemavu (SHIVYAWATA);

55. Shaban Suleman Muyombo
56. Agatha Harun Senyagwa Shirikisho la Vyama vya Wakulima
57. Suzy Samson Laizer Tanzania (TASO)
58. Dkt. Maselle Z. Maziku
59. Hadija Kondo
60. Reuben Mtango
61. Veronica Sophu (M/Kiti) Mtandao wa Vikundi Vidogo vya
62. Catherine G. Sibuti Wakulima Tanzania (MVIWATA)

63. William Tate Olenasha
64. Makeresia Pawa Pastoralists Indigenous Non-
65. Mashavu Yahya Governmental Organization (PINGOs)
66. Said Abdalla Bakari

67. S.Mwakifwamba Shirikisho la Wasanii nchini
68. Jacob Stephen
69. Nasib Abdoul
70. Ali Kiba
71. Steve Nyerere
72. Mrisho Mpoto
73. Mohamed Lyasi
74. Mariam Hamdan
75. Hamis Mwinjuma (Mwana FA)

76. Mohamed Mavala

77. Valeri Msoka Mtandao wa Jinsia Tanzania
(TGNP)/TAMWA

78. Dkt. Ave-Maria Semakafu ULINGO

79. Idrissa Kitwana Mustapha Asasi za Kiraia za Zanzibar (Youth
80. Fatma Musa Juma (Sukwa) Centre, MYDO

81. Mary Paul Daffa Tanzania NGO's (TANGO)

82. Mzee Kingunge Ngombale Taasisi ya Tiba ya Jadi
Mwiru

83. Elizabeth Minde KIWAKUKI

84. Godfrey Simbeye Private Sector Foundation of
Tanzania

WADAU NA MASHABIKI WA KATIBA INAYOPENDEKEZWA

Dkt. Francis Michael

Evod Mmanda

Dkt. Benson Bana

Prof. B. Rutinwa

Mohamed Fakihi

Prof. Costa Mahalu

Asha Abdallah Juma

Doroth Malecela

Prof. Remmy J. Assey

Dr. Suzan Kolimba

Prof. Esther Daniel Mwaikambo

Prof. Romuald Haule

Makame Omar Makame

Dkt. Mwinyi Talib Haji

Layila Ali Salum

Hamis Dambaya

Ali Ahmed Uki

Asha Makungu Othman

Hawa Mchafu

Waziri Rajabu

Biubwa Yahya Othman

Fatma Hamid Salim

Askofu Mkuu (Mstaafu) Donald Leo Mtetemela

Mch. Ernest Kadiva

Askofu Amosi Muhagachi

Sheikh Thabit Nouman Jongo

Sheikh Hamid Masoud Jongo

Juma Bakar Alawi

Dkt. Jasmine Tiisekwa

Magdalena Songora

Honorata Chitanda

Teddy Malulu

Shamsa Mwangunga

Asha Mtwangi

Paul Kimiti

Jesca Msambatavangu

Yasmin Aloo

Shamim Khan

Agness Likokola

Margaret Sitta

Felista Bura

B. MAPENDEKEZO YA MAJINA YA WAJUMBE WA KAMATI YA JIMBO

Inapendekezwa kwamba kila Kamati ya jimbo iwe na wajumbe 50. Wajumbe hao wahusishe:-

VYAMA VYA SIASA

1. Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya
2. Mbunge wa Jimbo husika CCM na Jumuiya zake
3. MNEC
4. Wajumbe wengine wote wa Kamati * Inapendekezwa kuwa
ya Siasa ya Wilaya* wajumbe wote wa Kamati ya
5. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Siasa ya Wilaya majina yao
Wilaya/Manispaa/Mji/Jiji yaorodheshwa hapa.
anaetokana na CCM
6. Madiwani wote wa CCM katika Na pale ambapo Wilaya ina
jimbo husika** majimbo zaidi ya moja basi
wajumbe wagawanywe katika
kila jimbo.
** majina wa madiwani wote
wanaotokana na CCM katika
jimbo husika majina yao
yaorodheshwe hapa
7.
8. ADC
9. UDP

10. AFP
11. Demokrasia Makini
12. APPT Maendeleo
13. NRA

14. TADEA

15. TLP
 

Attachments

  • CCM.pdf
    458.3 KB · Views: 1,468
Huu ni wizi mkubwa...Wanahangaika na Kampeni ya nini wakati Ukawa walishajitoa?

Si waache tu siku ya kura wajipigie Ndiyo karatasi zote kutoka Tume yao ya uchaguzi??

UKAWA (umoja wa katiba ya wananchi) ,je watakao piga kura siyo wanainchi?
 
Nimeona Hadi Kuna watu wanachama wa vyama Viwili....ha ha ha ha ha kuelekea Uchaguzi mkuu tutajua nani Mpinzani wa kweli...
 
John Memose Cheyo, Agustino Lyatonga Mrema na Dovutwa hawa watu watakachoambulia uchaguzi mkuu October hawatakuja kukisahau.
 
Katiba lazima ipite...muhimu tujitahidi Rais ajae na wabunge wengi wawe wanatoa hoja ya kurekebisha vifungu...tulishashindwa toka kitambo...muhimu ni kujipanga na sio kutoa mapovu wala kebehi. Hawa wa ukawa mbona katika maridhiano yao walikuwa wanajifungia na Rais.
 
kuna tatizo gani hapa standalone? ...tumewaacha ukawa kwa kuwa ukawa wako kundi la kuikataa katiba na tuliowaorodhesha ni wale wote waliobaki bungeni mpaka mwisho hivyo wao wako kundi la ndiyo...lazima tufanye mkakati wa kuipitisha kwa kuwa imeghariimu fedha nyingi za walipa kodi na ninyi fanyeni mkakati wa kuikataa lakini usituzuie sisi kufanya yetu
Yaan Kila wanachofanya Lumumba tunakipata mapemaa….Angalieni attachment ya Mkakati wa kupitisha kura ya ndio. Fungua kiambatanisho hapa chini.
attachment.php

attachment.php

attachment.php


 
Wanahangaika nini wakati mwenyekiti wao JK alisema wacha wajitoe washinde kiulaini?
 
Haya sie wengine tunapelekwa na wenye nchi, maana nchi ni yawana siasa si wananch
 
Back
Top Bottom