Mkaa vs mafuta taa kipi nafuu?

Mkaa vs mafuta taa kipi nafuu?

Kiboko ya vyote ni gesi. Kwa sababu utaiwasha pale tu unapohitaji na kusitisha matumizi mara baada ya uhitaji wako. Mkaa unakupotezea energy nyingi ukishamaliza kupika. Mafuta ya taa naona kama ni bei ghali, sina hakika lakini.

Kuna mtungi mdogo wa gesi ambao umeunganishwa na jiko kabisa unafaa zaidi kwa mabachela.
Umesema kweli kabisa, mafuta na mkaa ni hatari sana.
 
Dah...Ngoja nikuchanganye kidogo...
Kati ya mkaa na mafuta ya taa/ndege kiasi kikubwa cha nishati kinabebwa ndani ya mafuta ya taa/ndege. Mkaa una mgandamizo msongamano wa kiasi cha 10MJ kwa kila uzito wa kilogram 1 na mafuta ya taa ni 46MJ kwa kila kilogram 1.
Bei ya mafuta huku kwetu ni karibu shilling 1900 kwa kilo 1....... na mkaa ni karibu shilingi 1500 kwa kilo 1...sasa kwa kuzingatia matumizi ya kawaida ya nyumbani...joto linalopotea wakati wa kutumia ni kati ya asilimia 30 hadi 80 kwa jiko la mkaa na kati ya 5 hadi 25 kwa jiko la mafuta.... Muda wa kufikia kwenye mchanganyo mkubwa (kukolea kwa moto) ..mkaa hutumia kati ya dakika 5 hadi 20 wakati mafuta ni kati ya nusu dakika hadi dakika 2.....mkaa hutoa joto kwa mtindo wa kielpsi wakati mafuta mtindo wake ni wa kitrapezia.......
Baada ya maelezo hayo naona kila kitu kiko wazi sasa .... Amua mwenyewe 😀😀😀😀😀😀
EBO!..
 
Hakuna jibu la moja kwa moja hapo.. fanya hivi
1. Piga hesabu ya mkaa unaoutumia kwa mwezi
2. Piga hesabu ya gharama ya mafuta utumiayo kwa mwezi
3. Linganisha gharama hizo mbili uone ipi ipo juu
4. Angalia gharama zinazosababidhwa na upatikanaji wa mkaa na mafuta... zilinganishe
5. Linganisha gharama uzipitiazo usafi, mabaki hadi unaupata moto
Apige na muda pia anatumia
 
nimewaelewa vyema wakuu nitajitahidi ninunue mtungi
 
Back
Top Bottom