Hii maada haijabeba uhalisia wa maeneo tofauti tofauti ya Tanzania.. inawezekana mtoa maada amefikiria miji mikuu pekee.. Mfano: Kwa mji wanakoishi wazazi wangu ambao ni makao makuu ya mkoa fulani, tunapata gunia la mkaa kwa sh 17,000/=. Burnout ya mkaa ni tofauti na gesi, Wakemia wanajua vema.. kupika majimbi, maharage, kande, kuchemsha maji ya kuoga familia etc.. kwa ile location mkaa >>>>>>>>gesiHabarini,
Jamani leo naomba tujadili hili jambo binafsi, naona gesi ni bora na bei rahisi kuliko mkaa lakini naona hadi leo kuna watu wanapendelea kutumia mkaa wakisema ni bei rahisi kuliko gesi sasa nashindwa kuelewa ni bei ndogo kweli au ni mazoea, naomba tujadiliane kati ya gesi na mkaa kipi bora na bei rahisi?
Ni ufahamu tu. Lakini gesi ni rahisi sana. Ila sema haipiki maharage
Hii nayo kali mkuu unakuaje mtamu zaidi?Ndugu wali wa kupikwa na gas hauna radha hila wa mkaa ni mtamu sana asikuambia mtu mkaa unapika fresh
Wali una banikwa juu chini ladha yake karibia na papuchiHii nayo kali mkuu unakuaje mtamu zaidi?
hehehehehehee mkuu unataka yawe na utamu wa maini au kitimoto?
Noma sanaWali una banikwa juu chini ladha yake karibia na papuchi
Haina = AinaKwa unafuu wa uchumi mkaa unatosha ukitumia jiko bunifu gunia la elfu 80 utadumu nalo miezi 6 kama una familia kama hauna ni mwaka 1 na unapika haina yoyote ya chakula bila kujari ugumu wa chakula hicho kuiva
Na hapo nimejitaidi sana labda ninge andika kwa kihayaHaina = Aina
Kujari = Kujali
Huwa dk ngapi mkuu?Ukitaka kupika maharage nunua pressure cooker....(sufuria sio ile ya umeme)...ukiweka kwenye gas...maharage yanaiva fasta tu...
Laki 2 hatari sanaKuna majiko bunifu yana save sana mkaa gunia la mkaa la elfu 80 unatumia miezi 6
Umesema kweli kabisaGesi ni bora na rahisi kwa watu wenye kipato cha kati lakini gesi ni bora ila siyo rahisi kwa watu wenye kipato cha chini, kwa mfano; kuna familia unakuta kwa siku wana uwezo wa kununua mkaa wa mia tano tu ambao hupika siku nzima kwa kujibana sana, hatahivyo hakuna gesi ya 500. Utambue kuwa watanzania wengi wana kipato cha chini na hawawezi kukusanya elfu 21 au 22 ya kununulia gesi ya mitungi midogo kila inapoisha ila wanauwezo wa kubahatisha 500 ya kununulia mkaa.
Hii dhana ya gesi kutokupika maharage sijui inatokea wapi!!!??? Mi naona ni woga wa watu kuhisi maharage yanachukua muda mrefu kuiva kwahiyo yatamaliza gesi na si kwamba gesi haiivishi maharage.Kama rahisi kwann isipike maharage?
Pole mkuu mkaa wa 2,000 ni debe 1 kwetuGesi ni nishati ya bei rahisi sana ukilinganisha na Mkaa.
Nitolee mfano wa familia yangu::
Kukiwa hakuna gesi, hutumia mkaa wa sh 2000/= kwa siku, ambao ni wastani wa sh 60000/= kwa mwezi.
Lakini ninunuapo gesi ya Oryx kilo 15 kwa takribani shilingi 48000/=, hukaa kwa muda wa miezi miwili mpaka mitatu. Ambayo kwa wastani ningetumia mkaa ingekua ni kati ya 120,000/= - 180,000/=.
Japo ugumu wa gesi ni kuchemshia vitu vigumi mfano maharag n.k ambavyo kwangu mimi hununua mkaa hata wa 2000/= na vitu husika vikaCheshwa vingi na kuhifadhi kwa friji.
Kiujumla gesi + friji ni gharama nafuu sana.
Naomba utupie picha ya hilo jiko bunifu na sehemu ambayo mtu anaweza kulipataKwa unafuu wa uchumi mkaa unatosha ukitumia jiko bunifu gunia la elfu 80 utadumu nalo miezi 6 kama una familia kama hauna ni mwaka 1 na unapika haina yoyote ya chakula bila kujari ugumu wa chakula hicho kuiva
Pole mkuu mkaa wa 2,000 ni debe 1 kwetu
sana kwa vipi? Haipiki maharage kwa vipi?Ni ufahamu tu. Lakini gesi ni rahisi sana. Ila sema haipiki maharage
Naomba utupie picha ya hilo jiko bunifu na sehemu ambayo mtu anaweza kulipata
Biriani la mbuzi ,kachumbari pembeni, juice asilia,ahhh hapo weekend yetu itakua imeenda vizuriUnataka nikupikie msosi gani babaakee