Kinumbo
JF-Expert Member
- Dec 8, 2019
- 2,742
- 4,931
Bila shaka kila mmoja anamfahamu kijana huyu kutokana na kipaji chake cha kuimba.
Hapa nitawafahamisha mganga wa Diamond Platnumz anaemfanya ang'are kila kukicha. Hivyo hivyo kila mmoja anatamani kujua Diamond Platnumz anatumia uchawi upi unaomfanya awe maarufu namna hiyo.
Bwana mdogo huyu amejizolea umaarufu chungu nzima kuanzia Tanzania na Afrika yote kiujumla.
Mganga halisi wa Diamond Platnumz ni juhudi, kujituma pamoja na uvumilivu, nyenzo hizo tatu ndio zimemfanya kijana huyo azidi kung'ara kila uchwao.
Bila kupepesa macho kijana huyo ndio msanii mwenye mafanikio makubwa nchi Tanzania na Afrika Mashariki katika upande wa muziki.
Ni aibu na kukosa maarifa kumfananisha na wasanii wengine ambao hajafikia hata robo ya mafanikio yake Diamond Platnumz amekuwa mbunifu, mvumilivu, juhudi pamoja na kujituma na ndio maana anazidi kuwa mcharo kila kukicha. Na huo ndio uchawi wa Diamond Platnumz.
Nimetizama ziara zake za hivi karibu alipo kuwa nje ya nchi kuanzia Sierra Leone na ile ya Guinea Bissau.
Kuanzia mapokezi mpaka kwenye shoo husika unagundua kabisa huyu jamaa sio wa kawaida.
Tizama yale mapokezi apata utadhani ni kama ameenda Tandale kumbe yupo Kaskazini na Magharibi mwa Afrika. Ukifika wakati wa shoo ndio balaa lenyewe sasa anawaimbisha vile anataka.
Kongole kwake, kama binadamu naye ana mapungufu yake.
Hapa nitawafahamisha mganga wa Diamond Platnumz anaemfanya ang'are kila kukicha. Hivyo hivyo kila mmoja anatamani kujua Diamond Platnumz anatumia uchawi upi unaomfanya awe maarufu namna hiyo.
Bwana mdogo huyu amejizolea umaarufu chungu nzima kuanzia Tanzania na Afrika yote kiujumla.
Mganga halisi wa Diamond Platnumz ni juhudi, kujituma pamoja na uvumilivu, nyenzo hizo tatu ndio zimemfanya kijana huyo azidi kung'ara kila uchwao.
Bila kupepesa macho kijana huyo ndio msanii mwenye mafanikio makubwa nchi Tanzania na Afrika Mashariki katika upande wa muziki.
Ni aibu na kukosa maarifa kumfananisha na wasanii wengine ambao hajafikia hata robo ya mafanikio yake Diamond Platnumz amekuwa mbunifu, mvumilivu, juhudi pamoja na kujituma na ndio maana anazidi kuwa mcharo kila kukicha. Na huo ndio uchawi wa Diamond Platnumz.
Nimetizama ziara zake za hivi karibu alipo kuwa nje ya nchi kuanzia Sierra Leone na ile ya Guinea Bissau.
Kuanzia mapokezi mpaka kwenye shoo husika unagundua kabisa huyu jamaa sio wa kawaida.
Tizama yale mapokezi apata utadhani ni kama ameenda Tandale kumbe yupo Kaskazini na Magharibi mwa Afrika. Ukifika wakati wa shoo ndio balaa lenyewe sasa anawaimbisha vile anataka.
Kongole kwake, kama binadamu naye ana mapungufu yake.