Mjue Mamba: Kiumbe mwenye uzito wa ajabu

Mjue Mamba: Kiumbe mwenye uzito wa ajabu

Fall Army Worm

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2015
Posts
19,371
Reaction score
14,515
Heshima zenu Wakuu, Karibuni ktk Makala hii fupi Kuhusu huyu Kiumbe.
Mamba ni miongoni Mwa Viumbe hatari Zaidi kwa maisha ya Binadamu, Mamba ameorodheshwa miongoni Mwa Viumbe 10 hatari kwa maisha ya Binadamu. Mamba hufanya mawindo yake kwa kuvizia akiwa ndani ya maji na mara chache Zaidi akiwa nchi kavu.

Kimaumbile, Mamba huwa anakuwa na nguvu Zaidi anapokuwa kwenye maji. Utafiti unaonyesha kuwa kuna aina 23 za Mamba wanaojulikana Kitaalamu na kugawanywa kwenye makundi kutegemeana na kufanana kwao kitabia na mazingira wanayopenda kuishi.

Jamii ya Mamba wanaojulikana kama "SALT WATER CROCODILE " au "Indo -pacific crocodile ",ndio wakubwa Zaidi Kuliko jamii zingine zote. Mamba wa aina hii hupatikana Kaskazini Mwa Australia, Kusini Mwa Bara la Asia na baadhi ya maeneo ya India. Tofauti na Mamba tuliozoea kuwaona kwenye mito na Maziwa, "Salt Crocodile "maisha yao ni kwenye maji ya chumvi.

Mamba mkubwa wa aina hii ya "Salt Water Crocodile " ana uzito wa kati ya kilo 1000-2000 yaani tani 1-2,Uzito ambao ni mkubwa kwa Viumbe wote wanaotambaa.

Kimsingi Mamba huweza kuishi kati y'a miaka 40 hadi 60.Mamba jike hupevuka anapofika miaka kati ya 12-14 ,wakati dume hufikia hatua hiyo anapokuwa na miaka 16.Mamba jike huweza kutaga mayai kati ya 40-90 mara Moja kutegemea na jamii zao, kwa maana ya makundi waliyogawanywa.

Mamba mrefu Zaidi anaweza kufikia futi 20,sawa na Sm 600 au mita sita (6) au Zaidi, wakati Mamba mdogo huwa na Urefu wa futi tano (5).

Kingine kinachofurahisha Zaidi kwa Mamba ni kwamba ana uwezo wa kuota meno katika muda wake wote wa maisha.

Source -Gazeti la Nipashe Jumapili, la tarehe 1-7 April 2012.Karibuni sana.
 
Kuna habari ilitangazwa na matukio RFA kuwa, mamba alicheza na MTU/binadamu lisaa limoja kabla waokoaji hawajaja kumuokoa...!!

Nadhani alikuwa mamba mtoto
 
Kuna habari ilitangazwa na matukio RFA kuwa, mamba alicheza na MTU/binadamu lisaa limoja kabla waokoaji hawajaja kumuokoa...!!

Nadhani alikuwa mamba mtoto
Huyo alikuwa mdogo, Km angelikuwa ni yule Babu kubwa aina ya Salt Crocodile, jamaa asingelifurukuta.
 
Kuna habari ilitangazwa na matukio RFA kuwa, mamba alicheza na MTU/binadamu lisaa limoja kabla waokoaji hawajaja kumuokoa...!!

Nadhani alikuwa mamba mtoto
Si mtoto,ni Mamba mkubwa tu.Ujanja wa mamba ni kwenye maji ya kina kifupi,ili mamba akudake vizuri ni lazima asimike miguu na mkia kwenye tope apate "balance" ya kukuvuta na kukujeruhi.

Kwenye kina kirefu,mamba anakuwa hana nguvu,hivyo mnaweza kuzungushana kama tu una pumzi na unaweza kuogelea.Watu wa ziwa Nyasa,maeneo ya Lituhi,Lihuri na Manda Area hadi Mbaba-Bay wanajua sana kucheza na akila za mamba kwenye kina kirefu,ukienda maeneo ya Ukara huko Ziwa Nyanza hiyo michezo ya kuwakwepa mamba wanaijua sana.

Miaka fulani wakati wa Mwalimu Nyerere,tulipelekwa kisiwa cha Ukara,kule walikuwa wanasemwa kama ni "Wachawi" sana,wanatumia mpaka uchawi wa kukutumia mamba kwenye makarai ya chuma tulikuwa tukiogea zamani.Unaweza ukawa unaoga ukaona mamba ameibuka toka kwenye karai.

Watumishi wakawa hawaendi wakifika Ukerewe wakiambiwa wanapangiwa Ukara,wanaacha kazi.Kule tulienda kufanya "tafiti" ya mazingira ya wenyeji na kwanini wengi wanaogopa kwenda.Ukifika kule utajua jinsi watu wanavyomuona mamba kama kenge tu
 
Si mtoto,ni Mamba mkubwa tu.Ujanja wa mamba ni kwenye maji ya kina kifupi,ili mamba akudake vizuri ni lazima asimike miguu na mkia kwenye tope apate "balance" ya kukuvuta na kukujeruhi.

Kwenye kina kirefu,mamba anakuwa hana nguvu,hivyo mnaweza kuzungushana kama tu una pumzi na unaweza kuogelea.Watu wa ziwa Nyasa,maeneo ya Lituhi,Lihuri na Manda Area hadi Mbaba-Bay wanajua sana kucheza na akila za mamba kwenye kina kirefu,ukienda maeneo ya Ukara huko Ziwa Nyanza hiyo michezo ya kuwakwepa mamba wanaijua sana.

Miaka fulani wakati wa Mwalimu Nyerere,tulipelekwa kisiwa cha Ukara,kule walikuwa wanasemwa kama ni "Wachawi" sana,wanatumia mpaka uchawi wa kukutumia mamba kwenye makarai ya chuma tulikuwa tukiogea zamani.Unaweza ukawa unaoga ukaona mamba ameibuka toka kwenye karai.

Watumishi wakawa hawaendi wakifika Ukerewe wakiambiwa wanapangiwa Ukara,wanaacha kazi.Kule tulienda kufanya "tafiti" ya mazingira ya wenyeji na kwanini wengi wanaogopa kwenda.Ukifika kule utajua jinsi watu wanavyomuona mamba kama kenge tu
Kweli!
 
Si mtoto,ni Mamba mkubwa tu.Ujanja wa mamba ni kwenye maji ya kina kifupi,ili mamba akudake vizuri ni lazima asimike miguu na mkia kwenye tope apate "balance" ya kukuvuta na kukujeruhi.

Kwenye kina kirefu,mamba anakuwa hana nguvu,hivyo mnaweza kuzungushana kama tu una pumzi na unaweza kuogelea.Watu wa ziwa Nyasa,maeneo ya Lituhi,Lihuri na Manda Area hadi Mbaba-Bay wanajua sana kucheza na akila za mamba kwenye kina kirefu,ukienda maeneo ya Ukara huko Ziwa Nyanza hiyo michezo ya kuwakwepa mamba wanaijua sana.

Miaka fulani wakati wa Mwalimu Nyerere,tulipelekwa kisiwa cha Ukara,kule walikuwa wanasemwa kama ni "Wachawi" sana,wanatumia mpaka uchawi wa kukutumia mamba kwenye makarai ya chuma tulikuwa tukiogea zamani.Unaweza ukawa unaoga ukaona mamba ameibuka toka kwenye karai.

Watumishi wakawa hawaendi wakifika Ukerewe wakiambiwa wanapangiwa Ukara,wanaacha kazi.Kule tulienda kufanya "tafiti" ya mazingira ya wenyeji na kwanini wengi wanaogopa kwenda.Ukifika kule utajua jinsi watu wanavyomuona mamba kama kenge tu
Asante mkuu..

Ila nimrfurahi kusikia mamba anaonekana kama kenge tu kwa wakara.
 
Kazi kwenu mnaopenda kuogelea kwenye fukwe za coco beach,mmeshasikia sasa kuna Salt water crocodile...
 
Si mtoto,ni Mamba mkubwa tu.Ujanja wa mamba ni kwenye maji ya kina kifupi,ili mamba akudake vizuri ni lazima asimike miguu na mkia kwenye tope apate "balance" ya kukuvuta na kukujeruhi.

Kwenye kina kirefu,mamba anakuwa hana nguvu,hivyo mnaweza kuzungushana kama tu una pumzi na unaweza kuogelea.Watu wa ziwa Nyasa,maeneo ya Lituhi,Lihuri na Manda Area hadi Mbaba-Bay wanajua sana kucheza na akila za mamba kwenye kina kirefu,ukienda maeneo ya Ukara huko Ziwa Nyanza hiyo michezo ya kuwakwepa mamba wanaijua sana.

Miaka fulani wakati wa Mwalimu Nyerere,tulipelekwa kisiwa cha Ukara,kule walikuwa wanasemwa kama ni "Wachawi" sana,wanatumia mpaka uchawi wa kukutumia mamba kwenye makarai ya chuma tulikuwa tukiogea zamani.Unaweza ukawa unaoga ukaona mamba ameibuka toka kwenye karai.

Watumishi wakawa hawaendi wakifika Ukerewe wakiambiwa wanapangiwa Ukara,wanaacha kazi.Kule tulienda kufanya "tafiti" ya mazingira ya wenyeji na kwanini wengi wanaogopa kwenda.Ukifika kule utajua jinsi watu wanavyomuona mamba kama kenge tu
Shikamoo mzee barafu
 
Heshima zenu Wakuu, Karibuni ktk Makala hii fupi Kuhusu huyu Kiumbe.
Mamba ni miongoni Mwa Viumbe hatari Zaidi kwa maisha ya Binadamu, Mamba ameorodheshwa miongoni Mwa Viumbe 10 hatari kwa maisha ya Binadamu. Mamba hufanya mawindo yake kwa kuvizia akiwa ndani ya maji na mara chache Zaidi akiwa nchi kavu.

Kimaumbile, Mamba huwa anakuwa na nguvu Zaidi anapokuwa kwenye maji. Utafiti unaonyesha kuwa kuna aina 23 za Mamba wanaojulikana Kitaalamu na kugawanywa kwenye makundi kutegemeana na kufanana kwao kitabia na mazingira wanayopenda kuishi.

Jamii ya Mamba wanaojulikana kama "SALT WATER CROCODILE " au "Indo -pacific crocodile ",ndio wakubwa Zaidi Kuliko jamii zingine zote. Mamba wa aina hii hupatikana Kaskazini Mwa Australia, Kusini Mwa Bara la Asia na baadhi ya maeneo ya India. Tofauti na Mamba tuliozoea kuwaona kwenye mito na Maziwa, "Salt Crocodile "maisha yao ni kwenye maji ya chumvi.

Mamba mkubwa wa aina hii ya "Salt Water Crocodile " ana uzito wa kati ya kilo 1000-2000 yaani tani 1-2,Uzito ambao ni mkubwa kwa Viumbe wote wanaotambaa.

Kimsingi Mamba huweza kuishi kati y'a miaka 40 hadi 60.Mamba jike hupevuka anapofika miaka kati ya 12-14 ,wakati dume hufikia hatua hiyo anapokuwa na miaka 16.Mamba jike huweza kutaga mayai kati ya 40-90 mara Moja kutegemea na jamii zao, kwa maana ya makundi waliyogawanywa.

Mamba mrefu Zaidi anaweza kufikia futi 20,sawa na Sm 600 au mita sita (6) au Zaidi, wakati Mamba mdogo huwa na Urefu wa futi tano (5).

Kingine kinachofurahisha Zaidi kwa Mamba ni kwamba ana uwezo wa kuota meno katika muda wake wote wa maisha.

Source -Gazeti la Nipashe Jumapili, la tarehe 1-7 April 2012.Karibuni sana.
Mamba na ubabe wake wote hana ujanja kwa chui hata kama yupo kwenye maji chui anammalizia hukohuko!
 
Back
Top Bottom