Wazungu walifika nchini Marekani wakawakuta wale wanaoitwa Wamarekani wa Asili, wakavamia na kuwaua kwa mamilioni. Wamebaki wachache sasa. Moja hilo, nchi hii si yao, ukifuata historia hiyo. Kwa hivyo kama kuna mtu ana haki ya kufukuza kule ni Mmarekani wa Asili. Mzungu katokea Yuropa.
Pili, si wazungu wote wabaguzi. Labda hujui kwamba miaka ya 50 na 60 kulikuwa na harakati kubwa huko kukomesha sheria za kibaguzi. Ingawa watu weusi ndiyo walioongoza harakati hizo, waliungwa mkono na watu weupe. Hata JFK alipeleka majeshi ya serikali ya shirikisho kwenda kukomesha ubaguzi wa rangi jimboni Alabama na kuwasimamia watoto weusi kuingia katika shule zilizokuwa za wazungu tu.
Tatu, tumesema siku zote kwamba wengi wanaomuunga mkono Trump wana misingi ya kibaguzi. Na wala hawawezi kusikia hoja hata kama hoja nzuri zinatolewa. Kama uliangalia mdahalo wa jana utakuwa uliona dhahiri jinsi Trump anavyopwaya na kupwayuka hovyo.
Nne, katika mdahalo utakuwa jingine ambalo tumelisema siku zote kwamba Trump ni mnafiki namba moja. Anachopigania sasa hivi si nchi yake. Anataka tu kuingia ikulu. Kwa mfano anadai Wachina na Wamexico wanachukua viwanda vya Marekani. Ukweli ni kwamba yeye mwenyewe ni mmojawapo wa matajiri ambao wamehamishia utengenezaji wa bidhaa nje. Angalia unafiki huo hapa:
Umeona lakini kwamba anasema kitu halafu mara moja anakataa hakusema hivyo. Kama hujaona bado angalia juu ya comment yake juu ya madai ya Hillary kwamba Trump halipi kodi.
Yote haya tunayoyasema si kwa sababu ya media tu. Hilo ni jambo analosema kwa sababu wanajaribu kuonesha ukweli. Kila anapoona amebanwa, anasema media ni adui. Lakini watu tumemfuatilia toka siku nyingi. Jamaa ni tapeli thru and thru.
Angalia pia bibi huyo mmoja kwenye hiyo clip, hamwamini mtu yeyote isipokuwa Trump. Really?
Trump ana mbagua nani? Mtu mweusi? Sasa kule ni Marekani ni nchi yao weupe.
Tukisema Trump hatashinda kisa ubaguzi, population ya US itatuumbua. Ratio Kati ya blacks na whites.
Watu wengi saivi dunia, nchi kibao zinaingia kwenye Neo-nationalism, ndio kutokea kwa brexit etc...kwa mfumo huo wa sasa, watu kuweka nchi zao mbele kwanza inatosha kuleta picha kuwa Trump atashinda tho media zinambana na kumwekea bad coverage ila box la kura halitadanganya.