Mlalahoi
JF-Expert Member
- Aug 31, 2006
- 2,182
- 883
Majjid,
Nilikuwa nakuheshimu kama mchambuzi mahiri sana lakini napata walakini kama si njaa imekubadilisha basi kuna kitu ambacho si kizuri kimetawala moyo wako badala ya uzalendo kwa nchi yako! Ni vyema ukatulia kuandika habari zinazohusu uchaguzi huu na utumie muda wako kuandika habari zisizohusu uchaguzi ili reputation yako ibaki lakini vinginevyo utajishushia hadhi yako sana mbele ya jamii!
Nchi hii vitu viwili vinaanza kututafuna; 1. kupenda kuchumia tumbo 2. udini! tukiachana na hivi tutakuwa wazalendo wa kweli na mengine yatafuata!
Hapo mkuu umepiga msumari pale unapostahili.Mchanganyiko wa njaa na udini ni kichocheo kikubwa cha wanaojikomba kwa mafisadi.