Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Mjadala: Nini kingetokea Serikali isingeingilia biashara ya zao la korosho?
Kumekuwa na mjadala mkubwa tangu serikali ilipotangaza kuzuia wanunuzi wa zao la korosho ambao walijipanga kulipa wakulima wastani wa shilingi 1,500-1,700/- kwa kilo badala ya bei ya angalau shilingi 3,300 ambayo serikali inaamini wakulima wanapaswa kulipwa.
Ikumbukwe, kabla ya serikali kuingilia kati waliibuka wanasiasa wakiongozwa na Zitto Kabwe wakipaza sauti wakiitaka serikali inunue korosho kutoka kwa wakulima ili kuwakinga na hasara kutokana na wafanyabiashara waliotaka kuwanyonya wakulima. Japo kwa sasa ameibuka na kuyapinga maneno yake ya mwanzo.
Hoja kubwa ya kujadili ni nini kingetokea kama serikali isingeingilia biashara ya korosho? hali za wakulima ingekuwaje? wanasiasa leo wangesema nini dhidi ya serikali?
Ni kweli kuwa zoezi la serikali kununua korosho limekuwa taratibu kuliko ilivyokadiriwa. Lakini, ukweli unabaki wakulima na wadau halali wa korosho wananufaika zaidi na hatua ya serikali kuliko wangeachwa wanyonywe na walanguzi.
Zaidi ya wakulima kunufaika, unamuzi wa serikali umeweka nidhamu kwa walanguzi na wanunuzi wa korosho kutotumia mwanya wa kuungana na kupotosha soko kwa kutoa bei zisizo halisi.
Pamoja na wengi kupiga ramli kuwa ''katika msimu ujao wanunuzi wa korosho hawatakuja'' ulozi huu hautatimia kwani hata sasa baadhi ya wanunuzi halisi wanaoomba serikali na wako tayari kulipa bei iliyopendekezwa ambayo itamnufaisha mkulima, kinyume na ramli za akina Zitto kuwa serikali inapoteza dola milioni 600.
Hitimisho, Wakulima wangekuwa na hali mbaya zaidi kama serikali isingeingilia kati biashara ya korosho.
Rejea;
Wafanyabiashara waiomba Serikali inunue korosho za wakulima - JamiiForums
Kumekuwa na mjadala mkubwa tangu serikali ilipotangaza kuzuia wanunuzi wa zao la korosho ambao walijipanga kulipa wakulima wastani wa shilingi 1,500-1,700/- kwa kilo badala ya bei ya angalau shilingi 3,300 ambayo serikali inaamini wakulima wanapaswa kulipwa.
Ikumbukwe, kabla ya serikali kuingilia kati waliibuka wanasiasa wakiongozwa na Zitto Kabwe wakipaza sauti wakiitaka serikali inunue korosho kutoka kwa wakulima ili kuwakinga na hasara kutokana na wafanyabiashara waliotaka kuwanyonya wakulima. Japo kwa sasa ameibuka na kuyapinga maneno yake ya mwanzo.
Hoja kubwa ya kujadili ni nini kingetokea kama serikali isingeingilia biashara ya korosho? hali za wakulima ingekuwaje? wanasiasa leo wangesema nini dhidi ya serikali?
Ni kweli kuwa zoezi la serikali kununua korosho limekuwa taratibu kuliko ilivyokadiriwa. Lakini, ukweli unabaki wakulima na wadau halali wa korosho wananufaika zaidi na hatua ya serikali kuliko wangeachwa wanyonywe na walanguzi.
Zaidi ya wakulima kunufaika, unamuzi wa serikali umeweka nidhamu kwa walanguzi na wanunuzi wa korosho kutotumia mwanya wa kuungana na kupotosha soko kwa kutoa bei zisizo halisi.
Pamoja na wengi kupiga ramli kuwa ''katika msimu ujao wanunuzi wa korosho hawatakuja'' ulozi huu hautatimia kwani hata sasa baadhi ya wanunuzi halisi wanaoomba serikali na wako tayari kulipa bei iliyopendekezwa ambayo itamnufaisha mkulima, kinyume na ramli za akina Zitto kuwa serikali inapoteza dola milioni 600.
Hitimisho, Wakulima wangekuwa na hali mbaya zaidi kama serikali isingeingilia kati biashara ya korosho.
Rejea;
Wafanyabiashara waiomba Serikali inunue korosho za wakulima - JamiiForums