Ni yule niliyemshauri mda mwingi tukiwa sehemu za starehe kitambaa cheupe tukipata K vant kubwa na Windhoek za Kopo baridi, mda mwingi tuliwaza pesa na kula bata ila mwenzangu akawa busy kukusanya pesa za Mahali. Nilikwambia hiyo million mbili bora twende kidimbwi tuagize kuku wa kuchoma na jack Daniel kubwa ila akasema mimi sio mtu mzuri namfudisha upumbavu
Vijana nawasihi mjipende wenyewe kwanza, hawa wanawake siku hizi wamekuwa tooo cheap Sasa unaowa ili iweje. Unaleta stress za ajabu tu nakujaza majukumu ndani ya Familia unakosa hata pesa ya kula kitumbua barabarani mda wote unawaza bajeti ya kula na kusomesha watoto
Sasa kwakumalizia jamaa kaja kwangu Jana usiku analia anaomba msaada mke wake kamtoroka alimtumia meseji akasema hawezi ishi na JITU ambalo halina pesa. Ona Sasa haya mambo, kabla ya sasa jamaa alikuwa yupo vzr ila mke ndokamfilisi. Jamaa kawajengea wakwe zake ila wazazi wake wa kumzaa wanaishi kwenye banda la nyasi na kuta la Mavi ya punda. Mke wake waliyeachana saizi yupo Kwa wazazi wake anakaa kwenye mjengo mpyaa ambao jamaa aliwajengea
Finally, jamaa yupo hapa kwangu mda huu Hana hata pakulala mke ameuza kila kitu kodi ya nyumba anadaiwa. Linakoroma tu sijui nilipake mafuta


🥱