SaintErick
Member
- Aug 7, 2013
- 95
- 61
- Thread starter
- #21
Waalimu ni zao la waliofeli😕
Labda n sahihi kua n zao la walofeli!! ila itaniuma saaaana km hilo zao la waliofeli ndo walikufundisha mpaka leo unajua haya unayoyaju
Waalimu ni zao la waliofeli😕
Japo kuna sababu nyingi za kwa nini ualimu ni taaluma inayotazamwa kama ya chini kimaslahi, sababu kubwa kabisa ni walimu wenyewe wanaifanya taaluma idharaulike. Mfano: walimu wengi ni wapambe wapambe wa mambo ya hovyo.hovyo ya serikali, yaani hutumika katika kazi hata zisizokuwa za profession zao. Pili, wengi hawajiamini kiuchumi, kitaaluma na kimaamuzi (waoga). Tatu, kama taaluma imekosa dira kutokana na kutawaliwa na watu wanaokata tamaa ya maisha (labda sasa hivi ambapo wengi wameanza kujikwamua kwa kufanya shughuli binafsi za kiuchumi). Nne, kukosa maamuzi ya kimsimamo wa pamoja katika kuamua mambo yanayowahusu, mfano: masuala mtambuka yanayohusu kada hii yanaamuliwa na tume ya utumishi wa umma ama TSD alhali hakuna chombo rasmi cha kuamua kuhusu masuala nyeti ya kitaaluma na kimaslahi ya walimu.
Mbali na sababu za ndani ya taaluma, sababu zingine kubwa ni utashi wa kisiasa katika kuboresha taaluma hiyo na mazingira yake ya kazi toka kwa watawala.
Yapo mengi tu lakini kwa kumalizia nikwambie adui wa mwalimu ni mwalimu mwenyewe na mfumo. CWT haitokaa imkomboe mwalimu maana matatizo yanayowakabili walimu yakiisha, wale waajiriwa wa CWT waishi vipi? Ni kwa nini walimu wanapambana kuajiriwa kama makatibu wa wilaya na mikoa wa CWT? Kwa nini maslahi ni mazuri CWT tofauti na kazi ya ualimu?
Nukuu: "Ukioa Mwalimu una tabu kwelikweli" (Kikwete, J. M., 2015, May 1st. Mwanza)
fanya kazi mkuu kwa bidii jikomboe kiuchumi hayo mengine utajipa pressure tu