Mizigo yapungua bandari ya DSM

Mizigo yapungua bandari ya DSM

Mimi sababu ya msingi ni za kiujanjaujanja tu mfano bandari ya BEIRA malawi kuna haikuwepo mwanzon kwa nin sasa waone ndio yenye unafuu , nimegundua bandari ya daa ilikuwa inaficha sana wakwepa kodi wengi sana na kwa sasa hiyo mianya imebanwa
Kama umesoma vizuri na kwa kina utagundua mabadiliko hayo hayajasababishwa na bandari ya Beira bali kukamilika kwa reli ya kisasa ambayo imeleta unafuu katika usafirishaji wa shehena.

Hebu kasome tena.
 
Tanzania tumebahatika kijiografia,lakini watawala wetu wameshindwa kuitumia hiyo fursa.kama tungeweza ku invest nguvu zetu nyingi bandarini kama ndio chanzo kikuu cha mapato,basi huko kwingine tungekuwa tunamalizia tu.Lazima watawala wetu watambue kuwa tuko kwenye ksrne ya ushindani mkubwa sana wa kibiashara
Tuko kwenye ,tuweke siasa pembeni kwanza
Na hao watawala wetu tumeletewa na Mungu au tumewapenda wenyewe na tumewachagua wenyewe?
 
Ngoja kwanza tumalize kutumbua majipu. Yakishaisha tutaanza ujenzi wa reli. Majipu kwanza ujenzi baadae
Ujenzi wa reli kwenda wapi wakati watu wanamalizia na wataanza kupiga kazi
 
Hata kama bandari ikipata trilioni tano kwa siku hakuna mabadiliko ya moja kwa moja nitakayoyapata kama mwananchi wa kawaida. kwa kuwa imekuwa kawaida rasilimali ya umma inakuwa na maslahi kwa watu wachache. Nchi jirani endeleeni kutumia miundombinu mbadala. walivyobunya hapo bandari inatosha.
 
Kwenye kampeni walikuwa wanadanganya watu kuwa wakichaguliwa watejenga reli ya kisasa,baada ya kuchaguliwa wameruka kimanga kwamba kujenga reli ya kisasa ni ngumu na haiwezekani,kwa mapato ya serikali itachukua miaka 30 ili kukamilisha ujenzi.Sasa wanaanza kukiona kwa uongo wao
 
Tanzania tumebahatika kijiografia,lakini watawala wetu wameshindwa kuitumia hiyo fursa.kama tungeweza ku invest nguvu zetu nyingi bandarini kama ndio chanzo kikuu cha mapato,basi huko kwingine tungekuwa tunamalizia tu.Lazima watawala wetu watambue kuwa tuko kwenye ksrne ya ushindani mkubwa sana wa kibiashara
Tuko kwenye ,tuweke siasa pembeni kwanza
Reli huwa inahujumuwa na Wamiliki wa Magari makubwa ya mizigo na mafuta , wanajua Reli ikifanya kazi watalala njaa hivyo huwatuma watu kwenda kuharibu reli na vichwa vyake .
 
Kwenye kampeni walikuwa wanadanganya watu kuwa wakichaguliwa watejenga reli ya kisasa,baada ya kuchaguliwa wameruka kimanga kwamba kujenga reli ya kisasa ni ngumu na haiwezekani,kwa mapato ya serikali itachukua miaka 30 ili kukamilisha ujenzi.Sasa wanaanza kukiona kwa uongo wao
Wafanyabiashara wakubwa Wamiliki wa Magari ya mizigo na mafuta ambao wengi ni wafadhili wa ccm hawataki kusikia Reli inaanza kazi kabsa wanajua kuwa ikianza kazi wataathilika sana .
 
mnasema wageni wanakwepa kodi ya transit au...TRA wamekua wakipiga mnada ile mizigo ya wageni iliyokaa hapo kwa muda mrefu kwa makosa ya Ma Agent Durban ukikosewa baada ya kutoa leo kesho unatoka ni mara chache sans kusikia upigwe mnada mzigo wa mgeni mpaka mahakama ndio uamua sio hapo wageni wameuziwa magari kwa kosa linalolekebishika leo tunalia hawaji..
 
Usafiri wa Reli umetushinda. Wa Anga pia umetushinda..... Na bado tunawapenda wenyewe na tunawachagua wenyewe. Acha tuisome namba. Hamna jinsi tena
Wafanyabiashara Wamiliki wa Magari ya mizigo na mafuta hawataki kusikia Reli inafufuliwa milele.
 
TRA mpunguzeurasimu kwanini utaratibu wa kuhakiki mizigo unachukua muda mwingi sana bila sababu za msingi, hembu jaribuni kwenda na kasi ya Magufuli.
 
Niliuchukia utawala wa Mkwere kwasababu ya kuiua miundombinu ya reli,kwani waliua kiungo muhimu cha uhai wa uchumi wa taifa hili.
 
mnasema wageni wanakwepa kodi ya transit au...TRA wamekua wakipiga mnada ile mizigo ya wageni iliyokaa hapo kwa muda mrefu kwa makosa ya Ma Agent Durban ukikosewa baada ya kutoa leo kesho unatoka ni mara chache sans kusikia upigwe mnada mzigo wa mgeni mpaka mahakama ndio uamua sio hapo wageni wameuziwa magari kwa kosa linalolekebishika leo tunalia hawaji..
Bandari ya Dsm kuna Usumbufu wa Uzembe wao wenyewe , usumbufu mwingi hufanywa makusudi ili mzigo uchelewe uingie kwenye storage wapate pesa , wenye Bandari kavu hucheza dili na wafanyakazi wa Bandari kuu kuchelewesha makusudi ili wapate sababu ya kudai storage . na Kama kuna pesa inapotea bila Kodi ni hiyo pesa ya storage inaliwa na wajanja wachache , lazima wateja wakimbie kuna usumbufu na magumashi mengi , hata Wamiliki wa Meli hawataki kuja Bandari ya Dsm wanadai Meli zinakaa foleni kwenye maji mpaka siku 40 au zaidi, wanapenda Bandari zingine ambao huenda na kushusha na kupakia wanaondoka mara moja.
 
TRA mpunguzeurasimu kwanini utaratibu wa kuhakiki mizigo unachukua muda mwingi sana bila sababu za msingi, hembu jaribuni kwenda na kasi ya Magufuli.
Mkuu ofisi za TRA na Bandari zenyewe zipo zig zaga , hakuna mpangilio , Kwa mtu mgeni kutoa mzigo bila wakala ni shida sana , kule Mombasa Ofisi zimejipanga sehemu moja ukianza 1,2,3,4...... Mpaka mwisho unaenda kutoa mzigo wako bila Dalali , hawana usumbufu wa ajabu Kama Dsm.
 
dah, pigo jingine tena
tulitakiwa kujenga reli ya kisasa badala ya kukomaa na mabarabara ya mwendokasi yasiyo na tija
 
Wasi wasi wangu ujenzi wa reli ya kisasa kutoka mombasa hadi congo ukikamilika tutakosa wateja wengi mno wa bandari hivyo kupelekea kuyumba kwa uchumi.tatizo viongozi wa tanzania wamekalia ulaji tu hawafikirii kubuni njia za kiushindani na nchi jirani.
Mkuu ubunifu ulibakia kwenye kuongeza ada za uwezeshaji mkopo.
 
Kweli sasa tutaisoma namba maana wafadhili washaondoa ufadhili wao bandari ndio hiyo imedoda,doooo kweli sheeni umeamua kututesa
Shein Safari hii atabeba Laana nyingi maana njaa ya Tanganyika ni lawama kwake , inabidi Hazina wapunguze pesa zinazopelekwa Zanzibar kuwatunza na kuwalea wote , pesa ya kubembeleza muungano nayo ipunguzwe kufidia Machungu huku Tanganyika .
 
Wafanyabiashara Wamiliki wa Magari ya mizigo na mafuta hawataki kusikia Reli inafufuliwa milele.
Kwa lugha nyepesi unataka kusema hawa wafanyabiashara wameiweka serikali mfukoni. Wananchi tumlaumu nani?
 
Hizo ni changamoto serikali ikijipanga inaweza kuzitatua, tumelala sana kwa sababu sisi ni wazuri kwenye plan na strategy ikifika kwenye utekelezaji ni zero, mfano reli toka dar- Bujumbura-DRC ilikua ijengwe tangu enzi za kikwete lakini hadi sasa hakuna kinachoendelea. Kenya kwa kuona hiyo fursa ambayo wameicopy toka hapa TZ tayari wanajenga reli. Labda tusubiri hii awamu huenda ikafanya kitu ingawa tutakua tumechelewa.
 
Back
Top Bottom