Nenda Kawe kapokee Miujiza ndugu,,, Mimi nilikuwa mbishi hivyo hivyo,, siku Moja nikiwa Sina hili Wala lile naelekea zangu beach kawe,,, Kuna karoho kakaniambia pita apo arise and shine dakika Moja. Nikaenda nimekuta watu wanatoa sadaka hasa wale sijui waliochelewa ,, nilitoa elfu mbili tuu maana mfukoni nilikuwa na elfu 5 pekee. Huwezi amini jamaa alisema Kila mtu anyanyue simu yake kabla ya kuondoka lazima utapokea habari njema. Kabla ibada haijaisha Kuna mtu nilikuwa nishasahau deni linakaribia miaka 2 muamala ulisoma pale pale. Shuhuda ya pili Ile siku nikanunua mafuta ya buku pia home alikuja sista angu tangu 2020 anasaka ajira ,,, nikamwambia fatilia arise and shine andika maombi 12 uvuke mwaka na ajira yako. Dogo saivi yupo zake ameshapata ajira Tena salary amenizidi mpk braza kaka. Kwa hiyo maswala ya Imani siyo ya kubeza ACHA watu waamini kama inawasaidia wasipangiwe namna ya kuendea madhabahu.