gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,272
- 20,714
- Thread starter
- #121
Kama una ma house girl watatu halafu unajifanya kuishi maisha ya juu unafikiri ndugu atakubali kuingia kwenye banda la kuku kuokota mayai ay hata kumwagilia maji michongoma?
Nakumbuka nikiwa mdogo walikuwa wakija wageni kulala asubuhi baada ya chai mama huyo anaingia zake shambani.
Majembe yalikuwepo ya kutosha hakuna kisingizio hata kama umetokea town.
Huku sie tunapangiwa kazi weee mpaka mtu unaanza kufikiri hivi hawa wageni wataondoka lini tupumue?
Kumbe hapo wageni walikuwa wanaonyeshwa kuwa hii nyumba kazi ndiyo mpango mzima bila kujali mkubwa, mdogo au mgeni.
Wageni walikuwa wanatumiwa ipasavyo mpaka kwenda kuteka maji, kukata majani ya ng'ombe na kuokota kuni ati.
mmmh!,,,,,,,,,,,, hivi unawajua ndugu wa mume?