Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Ni pale ilipofikia hatua ya 5 bora ndipo ghafla kwa mshangao wa wengi,majaji wa mashindano hayo wakiongozwa na Gideon Chipungahelo walipoanza kuzozana na kutupiana makonde ya rejareja.Chanzo cha ugomvi huo inasemekana ni baadhi ya majaji kutaka washiriki fulani ambao wanahusiana nao kimapenzi washinde.Hata hivyo licha ya ugomvi huo,bwana Gideon Chipungahelo alifanikiwa kutaja majina ya washindi watatu bora.