GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,568
- 108,911
Kwa idadi hii tu ya Watu 66 ( hasa wana CCM ) waliojitokeza mpaka sasa kutaka Kugombea Uspika ni Zuzu ( Hambe ) pekee ndiyo hatoweza Kugundua kuwa ndani ya CCM ya sasa ( ya Rais Samia ) kuna Tatizo Kubwa, lakini pia ile Misingi imara ya iliyokuwa CCM ya Mwanzilishi ( na Role Model wangu GENTAMYCINE Kisiasa na Kimaisha ) Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere imeshaachwa na kuifanya CCM ya sasa ionekane kama Guest House / Lodge ambapo kila Mtu ( hasa Wahuni na Malaya ) wanaweza Kuingia muda Wowote wajisikiapo.
Kwa Sisi akina GENTAMYCINE ambao ndiyo Wafuasi na Warithi Tukuka wa Siasa za Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na iliyokuwa CCM yake Imara kuanzia Kimaadili na Kiutekelezaji tunaamini kuwa CCM ile ile ya Mwalimu ingethaminiwa mpaka leo hii idadi ya hawa Wagombea Uspika isingefikia hawa 66 sana sana wangejitokeza Watu ( wana CCM ) makini Watatu ( 3 ) au Watano ( 5 ) tu na ambao hakuna Mtu angekuwa na Mashaka nao.
Kwa Jicho la mbali hii siyo dalili njema ndani ya CCM na Siasa zake na huenda sasa taratibu ile CCM iliyokuwa ya Kipuuzi, ya Madili na Usanii ya mwaka 2005 hadi 2015 ikarejea na kibaya zaidi hata aliyeko anapenda kuonekana ni Mama au Bibi na siyo Kiongozi na Mtendaji ili aogopwe na aheshimiwe na Wanafiki walioanza Kumjaribu na Kumsanifu baada ya Kumsoma na kuijua Pumzi yake Kiuongozi.
Najua mtaninunia, ila nawapenda mno!!
Kwa Sisi akina GENTAMYCINE ambao ndiyo Wafuasi na Warithi Tukuka wa Siasa za Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na iliyokuwa CCM yake Imara kuanzia Kimaadili na Kiutekelezaji tunaamini kuwa CCM ile ile ya Mwalimu ingethaminiwa mpaka leo hii idadi ya hawa Wagombea Uspika isingefikia hawa 66 sana sana wangejitokeza Watu ( wana CCM ) makini Watatu ( 3 ) au Watano ( 5 ) tu na ambao hakuna Mtu angekuwa na Mashaka nao.
Kwa Jicho la mbali hii siyo dalili njema ndani ya CCM na Siasa zake na huenda sasa taratibu ile CCM iliyokuwa ya Kipuuzi, ya Madili na Usanii ya mwaka 2005 hadi 2015 ikarejea na kibaya zaidi hata aliyeko anapenda kuonekana ni Mama au Bibi na siyo Kiongozi na Mtendaji ili aogopwe na aheshimiwe na Wanafiki walioanza Kumjaribu na Kumsanifu baada ya Kumsoma na kuijua Pumzi yake Kiuongozi.
Najua mtaninunia, ila nawapenda mno!!