JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 3,177
- 7,472
“Wanaohamasisha maandamano kwa kutumia akaunti feki wasifikiri hawawezi kutambulika, watatambulika tu, Watanzania wengi ambao ni wema wanaoipigania amani watatuambia tu huyu siyo.
“Tukio kama hilo lilishawahi kutolewa siku za nyuma na walitambulika na wakachukuliwa hatua.”
Hiyo ni kauli ya Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), David Misime wakati akihojiwa na Kituo cha UTV, Oktoba 14, 2025.
Ameongeza “Suala la kutambua huyu ni muandamanaji na huyu ni mpiga kura tutawajua tu, uzuri ni kuwa mfumo wetu umeenda hadi ngazi ya chini kwenye levo ya Balozi.
“Tumetengeneza mfumo mzuri sana ambao siwezi kuuweka wazi muda huu.
“Mitandao ya Kijamii ni mizuri na inatusaidia kwenye shughuli mbalimbali, ikitumika vizuri inaweza kusaidia katika shughuli za kiuchumi na kijamii na mambo mengine mbalimbali, ikiwemo kujiendeleza kielimu na kupokea taarifa.”
“Tukio kama hilo lilishawahi kutolewa siku za nyuma na walitambulika na wakachukuliwa hatua.”
Hiyo ni kauli ya Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), David Misime wakati akihojiwa na Kituo cha UTV, Oktoba 14, 2025.
Ameongeza “Suala la kutambua huyu ni muandamanaji na huyu ni mpiga kura tutawajua tu, uzuri ni kuwa mfumo wetu umeenda hadi ngazi ya chini kwenye levo ya Balozi.
“Tumetengeneza mfumo mzuri sana ambao siwezi kuuweka wazi muda huu.
“Mitandao ya Kijamii ni mizuri na inatusaidia kwenye shughuli mbalimbali, ikitumika vizuri inaweza kusaidia katika shughuli za kiuchumi na kijamii na mambo mengine mbalimbali, ikiwemo kujiendeleza kielimu na kupokea taarifa.”