ndege JOHN
JF-Expert Member
- Aug 5, 2015
- 19,554
- 44,723
Sijui kwanini nahisi kama msiba wa watu Hawa wawili umefutika mapema mno mioyoni mwa wengi. Nilitaka angalau kuendelea kusikia Mambo mbalimbali ya kujifunza, kuhamasika, kujikumbusha n.k kuhusiana na maisha Yao na Chanzo Cha vifo vyao.
Lakini kinyume na hapo nimeona kila mtu ni kama ameshapotezea, yaani unaweza kufikiria msiba Ni wa mwaka jana kumbe umetokea mwezi uliopita tu.
Shida ni nini watanzania tumekuwa na Mambo mengi na story nyingi au ndo kila mtu apambane na Hali yake kwa Sasa.
Anyway Mambo yasiwe mengi tukumbushane kufanya mema na kushika zile amri na maagizo tulizoachiwa. We ambaye huamini kuna kifo tambua kipo na kila kunapokucha siku ya kufa inakaribia.
Lakini kinyume na hapo nimeona kila mtu ni kama ameshapotezea, yaani unaweza kufikiria msiba Ni wa mwaka jana kumbe umetokea mwezi uliopita tu.
Shida ni nini watanzania tumekuwa na Mambo mengi na story nyingi au ndo kila mtu apambane na Hali yake kwa Sasa.
Anyway Mambo yasiwe mengi tukumbushane kufanya mema na kushika zile amri na maagizo tulizoachiwa. We ambaye huamini kuna kifo tambua kipo na kila kunapokucha siku ya kufa inakaribia.